[Tahadhari Ya Matusi Ya Nguoni] Huu Sio Unaharakati, Haya Ni Matusi Na Udhalilishaji Dhidi Ya Mama Samia.
“Kushindwa kuonya ni dhambi kubwa kabisa katika taaluma ya intelijensia.” Naam, sisi ambao bado tunaendelea kuwa wadau wa taaluma hiyo (hadi tunaingia kaburini) tunawajibika kuepuka dhambi hiyo.
Pia ni muhimu kwetu (maafisa wa zamani wa Idara ya Usalama wa Taifa) kutimiza wajibu huu kutokana na ukweli kwamba Idara yetu ya Usalama wa Taifa ipo hoi bin taa…