Barua Ya Chahali

Share this post
Asante Mheshimiwa Zitto kwa Maoni Yako Kuhusu Sekta ya Umeme, Mjiskie Aibu Mlotumia Lugha Isiyo ya Kistaarabu Kujibu Maoni Hayo.
www.baruayachahali.com

Asante Mheshimiwa Zitto kwa Maoni Yako Kuhusu Sekta ya Umeme, Mjiskie Aibu Mlotumia Lugha Isiyo ya Kistaarabu Kujibu Maoni Hayo.

Evarist Chahali
Nov 18, 2021
Share

Ninapenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa mchango wa Kiongozi Mkuu wa chama cha ACT-Wazalendo, Mheshimiwa Zitto Kabwe, kwa maoni yake kufuatia bandiko langu la jana kwenye kijarida hiki lililokuwa na kichwa cha habari “Tanesco Inahujumiwa. January Makamba Anahujumiwa. Mama Samia Pia Anahujumiwa by Proxy.”

Twitter avatar for @zittokabweZitto MwamiRuyagwa Kabwe @zittokabwe
@Chahali Siamini kuna hujuma. Ninaamini ni mambo ya kisera na madhara ya Miaka 5 unusu ya incompetence katika uendeshaji wa Uchumi. Tulidanganywa na tukaamini uongo huo. Sasa tunatumia uongo ule kuwapima wenye Mamlaka sasa. NCHI HAINA UMEME WA KUTOSHA. Hatujaongeza Hata 1MW kwa Miaka 5

November 17th 2021

8 Retweets69 Likes
Twitter avatar for @zittokabweZitto MwamiRuyagwa Kabwe @zittokabwe
@Chahali We lived a lie. Viongozi walikuwa wanadanganya makusudi. Badala wa kufanya uchambuzi wa kina tunaangusha gari bovu kwa @JMakamba. January anapaswa ku address Nchi na kusema ukweli halisi badala ya kubeba Hizi lawama. Ukila mbegu msimu ujao lazima uwe na njaa. Tulikula mbegu

November 17th 2021

4 Retweets22 Likes
Twitter avatar for @zittokabweZitto MwamiRuyagwa Kabwe @zittokabwe
@Chahali Mradi wa 300MW Mtwara ulisimama. Mradi wa 350MW Kilwa ulisimama. Mradi wa nyongeza Kinyerezi 185MW ulisimama. Mradi wa Kinyerezi 3 and 4 umesimama. Utapata wapi Umeme kulisha nyongeza ya shughuli za Uchumi baada kufungua Nchi?

November 17th 2021

4 Retweets46 Likes
Twitter avatar for @zittokabweZitto MwamiRuyagwa Kabwe @zittokabwe
@Chahali So ndugu yangu @Chahali I don’t subscribe to HUJUMA. Ukweli usemwe kuwa tulikuwa na Miaka 5 ya bila kuongeza uzalishaji wa Umeme, Miaka 5 ya bila kukarabati njia za Umeme na sasa tunavuna tulichopanda. Ni bahati mbaya sana aliyesababisha haya katangulia mbele ya Haki

November 17th 2021

5 Retweets26 Likes
Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Nashukuru kiongozi kwa mchango wako

Zitto MwamiRuyagwa Kabwe @zittokabwe

@Chahali So ndugu yangu @Chahali I don’t subscribe to HUJUMA. Ukweli usemwe kuwa tulikuwa na Miaka 5 ya bila kuongeza uzalishaji wa Umeme, Miaka 5 ya bila kukarabati njia za Umeme na sasa tunavuna tulichopanda. Ni bahati mbaya sana aliyesababisha haya katangulia mbele ya Haki

November 17th 2021

16 Likes

Kwa upande mmoja, kwa mwanasiasa mwenye wadhifa mkubwa kitaifa kama yeye kuchukua muda wake kusoma chapisho hilo na hatimaye kutoa maoni yake makes me feel quite privileged.

Kwa upande mwingine, inapendeza kuona wanasiasa kama Mheshimiwa Zitto wakishiriki kwenye mijadala muhimu kwa mustakabali wa taifa letu.

Na kama alivyo Waziri January Makamba huko CCM, kwa upande wa Upinzani, Mheshimiwa Zitto ni the most interactive politician, “anajichanganya” (mingling) na kila mtu bila kubagua. Kwa bahati mbaya, ukaribu aliojenga Mheshimiwa Zitto na takriban kila Mtanzania, hususan mtandaoni, umemfanya kuwa mmoja wa wanasiasa wanaotukanwa sana. Halafu bado tutawalaumu waheshimiwa wakiamua kujiweka mbali nasi?

Kwa bahati mbaya zaidi - pengine makusudi - baadhi ya waliotoa maoni yao kufuatia maoni ya Mheshimiwa Zitto walitumia lugha isiyo ya kistaarabu, ikiwa ni pamoja na matusi.

Matusi ni janga kama ubuyu. Janga hili linaathiri sana maongezi kwenye mitandao ya kijamii. Mara kadhaa nimepokea ujumbe kutoka kwa watu mbalimbali wanaoeleza kuwa japo wameguswa na mada, wanashindwa kutoa maoni yao kwa kuchelewa kutukanwa.

Janga la matusi linachangiwa na sababu kuu mbili. Ya kwanza ni akili duni. Takriban kila mtu anayejihusisha na matusi mtandaoni au hata mtaani, ana mapungufu ya kiakili. Kwao, matusi ni sawa na mkongojo wa kuwawezesha kufikisha ujumbe wao.

Sababu ya pili ni chembechembe za udikteta zinazotawala vichwani mwa baadhi ya Watanzania. Utakuta watu ni wepesi kulaumu “udikteta wa watawala wetu” ilhali nao wanafanya udikteta pindi wakikutana na hoja wasizoafikiana nazo.

Na hawa wapenda matusi huwa wa kwanza kulalamika wanapopigwa bloku.

Nihitimishe kwa kumshukuru tena Mheshimiwa Zitto na mchango wake wa maoni na ninawalaani vikali wote waliomjibu kwa lugha isiyo ya kistaarabu ikiwa ni pamoja na kutumia matusi. Twaweza kutofautiana kimtazamo pasi haja ya kutoboana macho.

Siku njema

Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Sign up for our #Ujasusi newsletter:
eepurl.com/gtDV6T
Image

November 17th 2021

13 Likes
ShareShare
TopNewCommunity

No posts

Ready for more?

© 2022 Evarist Chahali
Privacy ∙ Terms ∙ Collection notice
Publish on Substack Get the app
Substack is the home for great writing