Barua Ya Chahali

Share this post
Watu Wasiojulikana Wajitokeza Hadharani
www.baruayachahali.com

Watu Wasiojulikana Wajitokeza Hadharani

Afisa Usalama Kumtisha Zitto Kabwe Ni Mwanzo Tu wa Yajayo

Evarist Chahali
Jan 21, 2019
13
Share this post
Watu Wasiojulikana Wajitokeza Hadharani
www.baruayachahali.com

Je upo kwenye mitandao ya kijamii mingapi? Mie nipo sehemu nyingi lakini ninayoitembelea kila siku (kutoka naotembelea sana to ninaotembelea sio sana) ni Twitter, Insta, Facebook, Jamii Forums, Reddit na Medium. Nipo pia huko LinkedIn, Pinterest, Google+, Blogger, Wordpress, nk japo siendi huko kila siku.

Kwanini Twitter sana? Kwa sababu mtandao huo wa kijamii ni kama chombo cha habari. Na watu mbalimbali wamekuwa wakiutumia kutoa matamko/taarifa mbalimbali.

Na Ijumaa Januari 18, kupitia mtandao huo wa kijamii, Kiongozi Mkuu wa Chadema cha ACT-Wazalendo Zitto Kabwe alitwiti kwamba ametishiwa maisha na Afisa Usalama wa Taifa akiwa Bungeni Dodoma.

Twitter avatar for @zittokabweZitto Kabwe Ruyagwa @zittokabwe
Leo mchana nimetishiwa kuuwawa na Afisa Usalama wa Taifa hapa Bungeni ukumbi wa Msekwa mara baada ya Mwenyekiti wa Kamati kuniondoa kikaoni Kwa kuwa sio mjumbe ( kinyume na kanuni za Bunge ). Afisa huyo alinifuata nje na kuniambia ‘ dawa yako wewe ni kukuua’. #BungeMfukoni

January 18th 2019

355 Retweets1,735 Likes

Twitter avatar for @zittokabweZitto Kabwe Ruyagwa @zittokabwe
Hakika nilikasirika sana na nikamwambia yeye na hao waliomtuma ni wapumbavu watakufa wao kwanza. Kama si Mbunge David Silinde kutokea ninaamini jambo baya lingetokea. Nimeandika Barua kwa Spika kutoa malalamiko rasmi ya Tabia za watumishi wa TISS kuwatisha Wabunge

January 18th 2019

162 Retweets709 Likes

Twitter avatar for @zittokabweZitto Kabwe Ruyagwa @zittokabwe
Serikali imejaza maafisa wa TISS hapa Bungeni kutisha Wabunge wasiwe huru kufanya kazi zao. Nimeambiwa kuwa mbunge @ZubbySakuru pia kakumbana na kadhia hii ya kutishwa ndani ya ukumbi Kamati Zikiendelea. Bunge la Wananchi limetiwa mfukoni na Serikali ( executive) #BungeMfukoni

January 18th 2019

171 Retweets840 Likes

Twitter avatar for @zittokabweZitto Kabwe Ruyagwa @zittokabwe
Nimemwambia huyo kijana wa Usalama akome kunifuatilia na kunitisha na aache upumbavu kwani mimi siwaogopi.

January 18th 2019

158 Retweets1,057 Likes

Twitter avatar for @zittokabweZitto Kabwe Ruyagwa @zittokabwe
Kama anayejiita Afisa Usalama wa Taifa ananitishia maisha mbunge ndani ya viwanja vya Bunge tena kwa kunifuata nje baada ya kutii amri ya kutoka kwenye Kikao na kinyume cha sheria, tunaposema TISS Ndio wamempiga risasi Lissu wanakataaje? Tumekuwa United Republic of Gangsters

January 18th 2019

203 Retweets1,298 Likes

Twitter avatar for @zittokabweZitto Kabwe Ruyagwa @zittokabwe
Spika anaacha watu wa usalama wa Taifa wanazagaa Bungeni. Sasa wanatisha Wabunge. Hadhi ya Bunge ipo wapi? Uhuru wa Bunge Upo wapi? Usalama wa wabunge guaranteed by Katiba na sheria ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge upo wapi? Wakati wa Msekwa, Sitta na Makinda haikuwa hivi. BAD

January 18th 2019

181 Retweets1,131 Likes

Twitter avatar for @zittokabweZitto Kabwe Ruyagwa @zittokabwe
Barua yangu kwa Spika wa Bunge kulalamika kuhusu kutishiwa na anayejiita Afisa Usalama wa Taifa ndani ya Viwanja vya Bunge, ukumbi wa Msekwa. Nimeiwasilisha leo ili hatua zichukuliwe
Image
Image
Image

January 18th 2019

175 Retweets910 Likes

Twitter avatar for @BenMembeBERNARD K. MEMBE @BenMembe
Kitendo alichofanyiwa Mhe. Zitto Z. Kabwe leo Bungeni na Afisa wa TISS, ni cha uadui, ni cha hatari na cha aibu kwa Idara ya Usalama wa Taifa. Adhabu ya kufanya fujo Bungeni haiwezi kuwa kifo na haiwezi kutolewa na TISS. Mamlaka husika imtumbue haraka!

January 18th 2019

192 Retweets1,318 Likes

Unaweza kudhani hizi ni porojo tu za kisiasa. Hapana. Baadhi yetu tumeshwahi kukumbana na kadhia kama hizi, si mara moja, au mara mbili, bali mara kadhaa kwa miaka kadhaa. Na waweza kupuuzia kuwa “hawawezi kunifanya lolote” kisha “ukapotezwa” kama Ben Saanane. Au wakataka kukuua kama Tundu Lissu. Au wakakubambikia kesi kama Sugu, na sasa Mbowe na Matiko.

Waweza kujidanganya kuwa “mie nani hasa mpaka hao mbwa wa Usalama wa Taifa wanitishie uhai?” Ukweli mchungu ni kwamba, kama wanaweza kumtishia Mbunge kama Zitto ambaye ni sio tu ni mwanasiasa mwenye jina kubwa bali pia ni Kiongozi Mkuu wa chama cha ACT-Wazalendo, wewe mwenzangu na mimi ni nani hasa usibughudhiwe?

Hoja yangu hapa ni kwamba, kama wanaweza kufanya hivyo kwa mtu muhimu kama huyo, kwanini washindwe kufanya hivyo kwako?

Ndio hivyo tena, hatimaye “Watu Wasiojulikana” wamejitokeza hadharani. Ama kwa hakika yajayo yanatafakarisha.

Tukutane wiki ijayo.

Take care!

Evarist

Nilikuwa nimemaliza kuandika barua hii kwenu lakini kabla sijaituma kwako, nikakumbana na kituko cha karne. Kituko hiki kitabaki kwenye historia ya taifa letu MILELE.

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
#Tanzania: opposition @ACTwazalendo youth wing outs "intelligence officer-cum-ruling party @ccm_tanzania cadre." How on earth is this happening? As ex-TISS officer, I take this as insult to the noble profession. The idiot (pictured) threatened @zittokabwe with assassination

ACT VIJANA TAIFA @ActVijana

Tumeweza kumtambua afisa wa TISS aliyemtisha kiongozi wetu wa Chama. Taarifa tulizonazo Afisa wa TISS aliyemtishia Kiongozi wetu anaitwa Thobias Mwesiga. Pamoja na kuwa TISS lakini pia ni kada wa @ccm_tanzania na aligombea Uenyekiti @UVCCMTAIFA TISS sasa mnaajiri Vijana wa CCM? https://t.co/PCKgQ2MwGx

January 20th 2019

12 Retweets24 Likes

Twitter avatar for @ActVijanaACT VIJANA TAIFA @ActVijana
Tumemtambua Afisa Usalama Aliyemtishia Kiongozi Wetu wa Chama Ndugu @zittokabwe Ngome ya Vijana Taifa ya ACT Wazalendo kwa kushirikiana na Kamati yetu ya Ulinzi na Usalama tumefanya uchunguzi wa kina juu ya tukio la kutishiwa kuuawa kwa Kiongozi wetu wa Chama.
Image

January 20th 2019

50 Retweets181 Likes

Twitter avatar for @ActVijanaACT VIJANA TAIFA @ActVijana
Tumeweza kumtambua afisa wa TISS aliyemtisha kiongozi wetu wa Chama. Taarifa tulizonazo Afisa wa TISS aliyemtishia Kiongozi wetu anaitwa Thobias Mwesiga. Pamoja na kuwa TISS lakini pia ni kada wa @ccm_tanzania na aligombea Uenyekiti @UVCCMTAIFA TISS sasa mnaajiri Vijana wa CCM?
Image

January 20th 2019

33 Retweets68 Likes

Naomba nisiongee sana, niweke kiporo hadi wiki ijayo, kwani nahisi kati ya sasa na wiki ijayo kuna mengi ya kujadili.

Comment
Share
Share this post
Watu Wasiojulikana Wajitokeza Hadharani
www.baruayachahali.com

Create your profile

0 subscriptions will be displayed on your profile (edit)

Skip for now

Only paid subscribers can comment on this post

Already a paid subscriber? Sign in

Check your email

For your security, we need to re-authenticate you.

Click the link we sent to , or click here to sign in.

TopNewCommunity

No posts

Ready for more?

© 2022 Evarist Chahali
Privacy ∙ Terms ∙ Collection notice
Publish on Substack Get the app
Substack is the home for great writing