Barua Ya Chahali

Share this post
#UziwaTwita Kuikaribisha Julai Na Neno Kuhusu #Uchaguzi2020
www.baruayachahali.com

#UziwaTwita Kuikaribisha Julai Na Neno Kuhusu #Uchaguzi2020

Evarist Chahali
Jul 2, 2020
Share this post
#UziwaTwita Kuikaribisha Julai Na Neno Kuhusu #Uchaguzi2020
www.baruayachahali.com

Kwanza, nina furaha kuwajulisha kuhusu ujio wa jarida la mtandaoni la JASUSI ambalo litajikita zaidi kuhusu masuala ya intelijensia. Vilevile litagusia masuala ya usalama wako mtandaoni na kukufundisha mbinu mbalimbali za kuwa salama. Kupitia jarida hilo natarajia pia kuendesha kozi ya awali ya udukuzi wa kimaadili. Nitawaletea maelezo zaidi hivi punde.

Awali niliomba maoni huko Twitter kuhusu jina la tovuti itakayobeba jarida hilo.

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Nawashukuru nyote 106 mlioshiriki. Ushauri wenu kuwa aidha "ujasusi dot com" au "intelijensia dot com" na kidogo "lolote linafaa" utazingatiwa. Nitawapa mrejesho. Endelea kufuatilia alama ya reli #KwaMtazamoWako
Image

Evarist Chahali @Chahali

#KwaMtazamoWako: Ungekuwa unataka kuanzisha chapisho (gazeti/kijarida/makala mfululizo aka series, nk) linalohusu masuala ya ushushushu/ujasusi/intelijensia ungependelea jina la tovuti husika liwe lipi kati ya haya matatu?

July 1st 2020

Pia nina furaha kuwafahamisha kuwa vitabu vyangu sasa vinauzwa kwa SHILINGI YA TANZANIA badala ya awali ambapo bei ilikuwa kwenye paundi ya Uingereza.

Anza Julai hii vema kwa kijipatia kopi yako HAPA

Niende kwenye #UziWaTwita. Bingirika nao hapa

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
#UziwaTwita wa kwanza kwa mwezi huu "mpya" wa Julai.
Image

July 1st 2020

4 Retweets11 Likes
Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Happy July everyone
Image

July 1st 2020

2 Likes
Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Nina ishu mbili tatu za kuongelea. Moja ni kutanabaisha kuwa kila siku naitupia jicho kalenda yangu. Na leo asubuhi imeniambia kuwa tumesalia na takriban miezi mitatu hivi kabla ya #uchaguzi2020. Japo ni mapema kutoa hukumu, maandalizi ya vyama vya upinzani hayaleti matumaini

July 1st 2020

6 Likes
Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Kwa mtazamo wangu unaoweza kuwa sio sahihi, ili kuing'oa CCM kunahitajika mikakati mizito na endelevu, na si kukurupuka miezi michache kabla ya uchaguzi. Wapinzani wanapaswa kujua kuwa CCM wana advantage ya "miundombinu ya kisiasa" inayostawishwa na "miundombinu ya kiserikali."

July 1st 2020

5 Likes
Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na viongozi wengine wa serikali katika ngazi mbalimbali ni makada wa CCM, na shughuli mbalimbali za kiserikali ni sehemu ya kampeni kwa ajili ya chama hicho. Hivyo ni wazi kwa upinzani kusubiri kipyenga cha kampeni kuanza rasmi wanachelewa

July 1st 2020

9 Likes
Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Kuna ishu ya #TumeHuru. Hii iliongelewa sana na vyama vya upinzani huko nyuma. Cha ajabu, miezi mitatu kabla ya uchaguzi, hakuna chama chochote kinachoongelea suala hilo. Unfortunately, wapinzani watapoteza tu muda wao kushiriki uchaguzi huo bila Tume Huru

July 1st 2020

9 Likes
Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Kilichifanyika kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa sio tu kitajirudia kwenye uchaguzi mkuu bali kitakuwa kibaya zaidi. Ifahamike tu kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania, mwaka huu uchaguzi mkuu upo mikononi mwa Idara ya Usalama wa Taifa.

July 1st 2020

7 Likes
Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Hawa wahuni wamekabidhiwa jukumu la kuhakikisha sio tu @MagufuliJP anashinda kwa kishindo bali pia kuahakikisha @ChademaTz haipati mbunge hata mmoja huku @ACTwazalendo ikilengwa kuhujumiwa Bara kwa vile ina msingi imara huko Zanzibar. Wenye masikio na wasikie

July 1st 2020

6 Likes
Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Otherwise, kwa upande wangu, kuelekea #uchaguzi2020 nitajibidiisha kufanya chambuzi za matukio mbalimbali yatakayojitokeza kabla ya the big day. Kadhalika nitafanya "ubashiri" katika "nani ataibuka kidedea" huko @ChademaTz na CCM Zanzibar. Endelea kutembelea ukurasa huu

July 1st 2020

5 Likes
Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Panapo majaliwa natarajia pia kuchapisha kitabu kama hiki pichani kwa minajili ya kuweka kumbukumbu kwa ajili ya vizazi vijavyo japo ni Watanzania wachache wenye muda wa kusoma vitabu vya siasa.

July 1st 2020

6 Likes
Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Nimalizie kwa matangazo mawili. La kwanza ni kuukaribisha utembelee duka la mtandaoni la vitabu vyangu
bit.ly/DukaLaChahali na ujipatie kopi yako/zakoVitabu Vya ChahaliDuka la mtandaoni la vitabu vya kielektroniki vya Evarist Chahalibit.ly

July 1st 2020

1 Retweet3 Likes

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Na tangazo la pili ni kuhusu kampuni ya usadi ya @AdelPhilConsult ambayo Julai hii itaanza kutoa huduma za #UsalamaWaMtandaoni (Cybersecurity) ikiwa ni pamoja "penetration testing" yaani uhakiki wa usalama wa miundombinu ya kompyuta kwa watu binafsi na taasisi
Image

July 1st 2020

3 Likes
Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Je akaunti zako mtandaoni - baruapepe, mitandao ya kijamii, nk - ni salama kiasi gani? Njia rahisi ni kumkabidhi mdukuzi wa kimaadili jukumu la kuhakiki kiwango cha usalama, ambapo "atashambulia" katiia namna ileile mdukuzi mhalifu angefanya. Maelezo zaidi yatafuata baadaye
Image

July 1st 2020

3 Likes
Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Kwa vile inatarajiwa kuwa mtandao utakuwa jukwaa muhimu la kampeni za #uchaguzi2020, huduma za @AdelPhilConsult zinaweza kuwa mkombozi kwa wengi, vyama vya siasa, wanasiasa binafsi, nk.
Image

July 1st 2020

5 Likes
Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
That's all for now. Again, Julai njema. Good evening!
Image

July 1st 2020

3 Likes

Ndimi jasusi wako,

Evarist Chahali

Comment
Share
Share this post
#UziwaTwita Kuikaribisha Julai Na Neno Kuhusu #Uchaguzi2020
www.baruayachahali.com

Create your profile

0 subscriptions will be displayed on your profile (edit)

Skip for now

Only paid subscribers can comment on this post

Already a paid subscriber? Sign in

Check your email

For your security, we need to re-authenticate you.

Click the link we sent to , or click here to sign in.

TopNewCommunity

No posts

Ready for more?

© 2022 Evarist Chahali
Privacy ∙ Terms ∙ Collection notice
Publish on Substack Get the app
Substack is the home for great writing