Utata wa Kifo Cha Sheikh Bura: Yasemekana "Alitoka Kwenye Mkutano wa ex-CAG Prof Assad"
Katika zama hizi za #WatuWasiojulikana ni muhimu kuangalia kila tukio kwa jicho la tatu. Na katika hili, naomba kukiri kwamba hata niliposikia taarifa ya kifo cha mfanyabiashara maarufu Ali Mufuruki nafsi ilihisi “huenda kuna mkono wa mtu.”
Na majuzi nilipokutana na habari ya kifo cha Sheikh Rashid Bura, hisia zangu zilipelekea kudhani huenda kuna mkono …