Barua Ya Chahali

Share this post
Urais Zanzibar: Kwa Kurejea Hujuma Dhidi Yake 1995, 2000, 2005, 2010, 2015, Maalim Seif Ana Haki Kugombea Tena Kwa Mara ya Sita
www.baruayachahali.com

Urais Zanzibar: Kwa Kurejea Hujuma Dhidi Yake 1995, 2000, 2005, 2010, 2015, Maalim Seif Ana Haki Kugombea Tena Kwa Mara ya Sita

Evarist Chahali
Jun 29, 2020
1
Share this post
Urais Zanzibar: Kwa Kurejea Hujuma Dhidi Yake 1995, 2000, 2005, 2010, 2015, Maalim Seif Ana Haki Kugombea Tena Kwa Mara ya Sita
www.baruayachahali.com

Jana, mwenyekiti wa taifa wa ACT-Wazalendo Maalim Seif Sharif Hamad alitangza kuwa ataomba ridhaa ya chama chake kuwa mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya chama hicho.

Twitter avatar for @SeifSharifHamadSeif Sharif Hamad @SeifSharifHamad
Nina furaha kubwa leo kuwaambia wananchi wa #Zanzibar kuwa sasa nimeshafanya maamuzi na maamuzi yangu ni KWAMBA INSHA ALLAH NITAGOMBEA nafasi ya Urais wa Zanzibar kwa mara nyengine tena katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu wa 2020.
Image

June 28th 2020

61 Retweets668 Likes

Endapo atapitishwa, na kwa mtazamo wangu sioni cha kuzuwia yeye kupitishwa na chama hicho, itakuwa ni uchaguzi mkuu wa tano mfululizo kwa Maalim Seif kugombea nafasi hiyo. Historia ya kugombea kwake urais wa Zanzibar ni kama ifuatavyo:

  • Aligombea mwaka 1995 katika uchaguzi mkuu wa kwanza wa vyama vingi dhidi ya mgombea wa CCM Dkt Salmin Amour, alieshinda kwa asilimia 50.2 ilhali Maalim Seif alipata asilimia 49.8

  • Akagombea tena mwaka 2000 akichuana na mgombea wa CCM Amani Karume aliyeshinda kwa asilimia 67.04 huku Maalim Seif akipata asilimia 32.96

    Dr salmin amour katika ubora wake - YouTube
  • Alijaribu tena bahati yake mwaka 2005 dhidi ya mgombea wa CCM Amani Karume aliyeshinda kwa asilimia 53.2 huku Maalim Seif akifuatia kwa karibu kwa asilimia 46.1

    35th General Conference: Visit of Mr Amani Abeid Karume, President ...
  • Katika uchaguzi wa mwaka 2010 Maalim Seif alianguka tena akipata asilimia 49.14 huku mgombea wa CCM Ali Mohammed Shein ashinda kwa asilimia 50.11

    Dr Ali Mohamed Shein - Alumni and Supporters - Newcastle University
  • Na uchaguzi mkuu wa mwisho kabla ya huu wa mwaka huu ulifanyika mwaka 2015 ambapo katika kinachoweza kutafsiriwa kuwa hujuma za waziwazi dhidi ya Maalim Seif, Tume ya Uchaguzi wa Zanzibar ilifuta matokeo ya uchaguzi, na kuamuru urudiwe ambapo Maalim Seif alisusa, na Dkt Shein akatangazwa mshindi kwa asilimia 91.4 matokeo ambayo hadi leo Maalim Seif hayatambui.

Danni Mzena on Twitter: "KATUNI POLITIKS 3 @seifkabelele @bmachumu ...

Hata hivyo, uamuzi wa Maalim Seif kutangaza kuwania tena urais kwa mara ya sita mfululizo kumezua maswali ambapo baadhi ya watu wanadhani ingekuwa mwafaka apishe wanasiasa wengine kuwania nafasi hiyo, hasa kwa vile amekuwa akishindwa chaguzi zote alizoshiriki.

Twitter avatar for @RealHauleGluckĠoodluck🎙🔥 @RealHauleGluck
Mara ya kwanza 1995... Naomba tujiulize kuna watoto wangapi humu walizaliwa 1995? Wangapi wameshasoma kumaliza vyuo na wao wana watoto? Maaali Seif kwa hili mzee wangu hatuwezi kukusapoti, miaka 30 mfululizo unagombea tuu? 🙆🏻‍♂️!! #AmkaZanzibar #77Nyeupe https://t.co/q3T974QqeO

Mwanaharakati Mzalendo @MwanaharakatiMz

Mwenyekiti wa Chama Cha @ACTwazalendo Maalim Seif Sharif Hamad ametangaza nia ya kuomba ridhaa ya chama chake kugombea Urais wa Zanzibar katika Uchaguzi Mkuu 2020. Hii itakuwa mara ya 6 kwa Maalim kugombea nafasi hiyo. https://t.co/hmi645WjZs

June 28th 2020

3 Retweets68 Likes

Kwa mtazamo wangu -unaoweza kuwa sio sahihi - sidhani kama kuna tatizo kwa Maalim Seif kugombea tena ENDAPO wafuasi wa chama chake wanaamini ndio mtu sahihi kuwa mgombea wao. Ikumbukwe kuwa hakuna ushahidi wowote kuwa Maalim Seif au ACT-Wazalendo wamemzuwia mwanachama mwingine kujitokeza kuwania nafasi hiyo. Na huenda akajitokeza leo au kabla ya zoezi la kutangaza nia kufungwa.

Lakini jingine ni haki ya kikatiba kwa Maalim Seif kugombea nafasi hiyo na nyingineyo ambayo ana sifa stahili.

Kadhalika, yeye ni mzoefu wa siasa za Zanzibar pengine zaidi ya mwanasiasa mwingine yoyote yule na amekumbana na misukosuko mingi katika kupigania haki, hususan za Wapemba.

Pengine kubwa zaidi ni “siri ya wazi” kuwa Maalim Seif amekuwa akiporwa ushindi mfululizo. Kwahiyo wanaomlaumu kwa “kugombea kila uchaguzi” wanapaswa pia kufahamu kuwa “aliporwa haki yake katika kila chaguzi hizo.” Sasa kwa vile kukata tamaa dhidi ya wanaomhujumu hakutobadili chochote basi ni vema akajaribu tena mwaka huu.

Hata hivyo, kuwa mgombea ni kitu kimoja na kushinda kwenye uchaguzi ni kitu kingine kabisa. Na hakuna mtu anayelielewa hilo vema zaidi ya Maalim Seif kwani licha ya maandalizi ya kila hali, ameishia kushindwa kila uchaguzi si kwa vile “kura hzikutosha” bali “sanaa za kiza” zimekuwa zikutumika kupora ushindi wake. Naandika hili kwa sababu nilipokuwa Kitengo nilishuhudia kwa macho yangu hujuma zilizofanywa dhidi ya mwanasiasa huyo, na ndio maana nadhani ni sahihi kwake kujaribu tena “kudai haki yake.”

Nimeandika hapo awali kwamba kuwa mgombea ni jambo moja na kushinda ni jingine. Swali linalobaki ni kwamba endapo atapitishwa na chama chake, na hilo sina shaka nalo, je atafanikiwa kuwa Rais ajaye wa Zanzibar?

Naomba nihifadhi jibu hadi CCM itakapopitisha mgombea wake ambapo kwa jicho la kijasusi nadhani atakuwa kati ya Dkt Mwinyi na Prof Mbarawa (naomba usininyime pongezi zangu kwa ‘ubashiri wangu’ endapo mmoja wao atapitishwa😊 )

Lakini wakati mnasubiri jawabu langu kwa swali endapo Maalim Seif atashinda, niwafikirishe tu na kauli mbili zinazokinzana kutoka kwa mwanasiasa huyo.

Twitter avatar for @SeifSharifHamadSeif Sharif Hamad @SeifSharifHamad
OPINIONISTA: #Tanzania’s October elections will be neither free nor fair unless urgent reforms are introduced
OPINIONISTA: Tanzania’s October elections will be neither free nor fair unless urgent reforms are introducedThe current landscape does not bode well for the upcoming Tanzanian elections. The nation is fractured, our people are suffering and the country’s institutions are rudderless. This is especially true of the National Electoral Commission and the Zanzibar Electoral Commission, both of which are being …dailymaverick.co.za

June 18th 2020

65 Retweets576 Likes

Kisha

Twitter avatar for @kwanza_tvKwanza TV @kwanza_tv
"Hatutoingia kwenye uchaguzi kushiriki, tunaingia kwenye uchaguzi kushinda, Tarehe 28 nitatoa maamuzi yangu". - Seif Sharif Hamad @SeifSharifHamad #HATUCHUJI #KwanzaHabari
Image

June 20th 2020

11 Retweets54 Likes

Maana yake ni kwamba Maalim Seif anaamini kuwa yeye na chama chake wanaweza kushinda hata kama kasoro alizoongelea kwenye makala hiyo (ya gazeti la Daily Maverick la Afrika Kusini) hazitorekebishwa.

Nisingependa kuongelea sana hilo kwa sasa maana mada hii imejikita kwenye tangazo la Maalim Seif kuwania tena nafasi ya urais na sio uchambuzi wa kina kuhusu mwanasiasa huyo na/au uchaguzi wa Zanzibar kwa ujumla, ambao utakujia mara baada ya Maalim Seif kupitishwa rasmi na CCM kutangaza mgombea wake.

Nimalizie kwa tangazo kuhusu vitabu vyangu vinavyopatikana HAPA. Endapo utakumbana na usumbufu wowote, nishtue.

Ndimi jasusi wako.

Evarist Chahali

Comment
Share
Share this post
Urais Zanzibar: Kwa Kurejea Hujuma Dhidi Yake 1995, 2000, 2005, 2010, 2015, Maalim Seif Ana Haki Kugombea Tena Kwa Mara ya Sita
www.baruayachahali.com

Create your profile

0 subscriptions will be displayed on your profile (edit)

Skip for now

Only paid subscribers can comment on this post

Already a paid subscriber? Sign in

Check your email

For your security, we need to re-authenticate you.

Click the link we sent to , or click here to sign in.

TopNewCommunity

No posts

Ready for more?

© 2022 Evarist Chahali
Privacy ∙ Terms ∙ Collection notice
Publish on Substack Get the app
Substack is the home for great writing