Barua Ya Chahali

Share this post
Ukimya wa Lissu Masaa 36 baada ya Mbowe na wenzake kuachiwa huru; mustakabali wa ajenda ya katiba mpya
www.baruayachahali.com

Ukimya wa Lissu Masaa 36 baada ya Mbowe na wenzake kuachiwa huru; mustakabali wa ajenda ya katiba mpya

Evarist Chahali
Mar 6
Share this post
Ukimya wa Lissu Masaa 36 baada ya Mbowe na wenzake kuachiwa huru; mustakabali wa ajenda ya katiba mpya
www.baruayachahali.com

Hadi wakati makala hii inachapishwa - zaidi ya masaa 36 tangu Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Mheshimiwa Freeman Mbowe na wenzake watatu waachiwe huru na DPP - Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Mheshimiwa Tundu Lissu hajatwiti chochote kuhusiana na suala hilo.

Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Kwa minajili ya kumbukumbu: hadi muda huu, Lissu hajatamka lolote kuhusu kuachiwa huru kwa Mheshimiwa @freemanmbowetz. 👉Hajaskia taarifa hizo? 👉 Ni "ukimya wa kimkakati"? 👉 Yupo safarini kurudi Tz? 👉 Au "kuna namna"?
Image

March 5th 2022

6 Retweets82 Likes
Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Any updates? 🤔

Jasusi @Chahali

Lissu hajasikia kuhusu Mbowe kuachiwa huru? Naona yupo kimya 🤔

March 4th 2022

2 Retweets31 Likes
Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Lissu hajasikia kuhusu Mbowe kuachiwa huru? Naona yupo kimya 🤔

March 4th 2022

3 Retweets27 Likes

Kwa upande mmoja baadhi ya wana-Chadema walijitokeza kumtetea Mheshimiwa Lissu wakidai “hawezi kukurupuka kuongelea suala hilo.”

Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Hao walioongea kabla ya kusikiliza pointi zenu wamekurupuka? 🙄

Lazarö E. killu @LazemKillu

@Chahali @freemanmbowetz Anasubiri tumalize point zetu aje kuzungumzia tulizoacha kuzungumzia..

March 5th 2022

1 Like
Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Kwahiyo hao viongozi wengine wa CDM waliotoa matamko sio makini na wamekurupuka?

WEMBO OIS IDIAG @DrPycon

@Chahali @freemanmbowetz @TunduALissu ni mtu makini wala hakurupuki ndugu jasusi😏

March 5th 2022

1 Like

Lakini kama jasusi alivyojibu, hoja kwamba Mheshimiwa Lissu hawezi kukurupuka kuongelea suala hilo haina mashiko kwa sababu sio suala linalohitaji maandalizi makubwa kuliongelea.

Kwa upande mwingine, kuna wanajaribu kutafsiri ukimya huo wa Mheshimiwa Lissu kama “kuchukizwa na hatua ya DDP kumwachia huru na wenzake.”

Twitter avatar for @madukwapeter𝙼𝚊𝚍𝚞𝚔𝚠𝚊 𝙿𝚎𝚝𝚎𝚛 @madukwapeter
@Chahali @freemanmbowetz Itakuwa anaona WIVU au imekuwa suprise. Bwn LISSU hakutegemea kama Mbowe ataonana na Rais Ikulu pale jana. Na ukizingatia pia kwamba ajenda ya MBOWE siyo gaidi imeisha; hakuna hoja nyingine ya kutrend nayo. Ni kama mama SAMIA amepiga KNOCKOUT tena kwa suprise hivi😀

March 5th 2022

1 Like

Jasusi anahisi kuwa huenda Mheshimiwa Lissu amekumbwa na dharura inayomzuwia kuongelea suala hilo na si kwamba amekasirishwa na hatua ya DPP kumfutia mashtaka Mheshimiwa Mbowe na wenzake.

Kuhusu mustakabali wa ajenda kuu ya Chadema kwa sasa ya katiba mpya, kuna “scenarios” kadhaa.

Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Curious cat: Jasusi, je ajenda ya kudai katiba mpya itaendelea baada ya Mbowe kuachiwa, na kukutana na Mama Samia? Jasusi: Itategemea vitu kadhaa. Kimoja cha msingi ni "alichoambiwa Mbowe Ikulu." Kingine ni "wanaharakati" walioshikia bango ajenda hiyo kupitia CDM. Muda utaongea.

March 5th 2022

1 Retweet9 Likes

Kwa upande mmoja, hadi muda huu hakuna anayefahamu “walichoafikiana” Mama Samia na Mheshimiwa Mbowe walipokutana juzi baada ya mwenyekiti huyo wa Chadema taifa kufutiwa kesi na kuachiwa huru.

Hata hivyo, yayumkinika kuhisi kuwa “kuna maelekezo” aliyopatiwa Mheshimiwa Mbowe ambayo yanaweza kumfanya “aafikiane na msimamo wa Mama Samia kuwa suala hilo (la katiba mpya) lisubiri kwanza.”

“Maelekezo” hayo yanaweza kuwa yalitolewa kama “ushauri” lakini uwezekano mkubwa ni kwamba yalikuwa katika mfumo wa maagizo yanayohitaji kutelekezwa aka amri.

Huo ni udikteta? Hapana. Hivyo ndivyo siasa za kwenye viambaza vya utawala zinavyofanya kazi. Wakati hadharani watu hushauriwa kufanya/kutofanya hili au lile, kwenye viambazo hivyo lugha huwa katika namna Waingereza wanaita “thinly veiled threat”

Endapo “Mheshimiwa Mbowe atakuwa ameagizwa kuweka kando ajenda ya katiba mpya hadi baadaye,” kuna uwezekano akaingia kwenye mgogoro dhidi ya “wanaharakati wa mtandaoni” ambao wamekuwa mstari wa mbele kuitumia Chadema kama jukwaa la kudai katiba mpya.

Na moja ya changamoto zinazomkabili Mheshimiwa Mbowe ni pamoja na kuiondoa Chadema kutoka mwelekeo wa kuwa genge la harakati badala ya chama kikubwa cha upinzani.

Japo chama hicho kinapaswa kuunga mkono makundi mbalimbali yenye ajenda mtambuka kuhusu mustakabali wa Tanzania, kwa hadhi na historia yake, hakipaswi “kuendeshwa kwa rimoti” na makundi ya nje na hata ndani ya chama hicho.

Ikiamua, Chadema inaweza kurudi zama za “utatu mtakatifu” wa Mheshimiwa Mbowe, Mheshimiwa Lissu na Mheshimiwa Zitto Kabwe ambapo chini ya uongozi wa wanasiasa hao, chama hicho kiliweza kuibua lundo la skandali za ufisadi kama vile Richmond (iliyopelekea aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa kujiuzulu Februari 2008), Kagoda, EPA, Buzwagi, Tangold, Meremeta, Tegeta Escrow, nk.

Kilichowezesha chama hicho kufahamu kuhusu ufisadi huo mchango mkubwa wa baadhi ya maafisa wa Idara ya Usalama wa Taifa waliojitoa mhanga kuwapatia wanasiasa hao nyaraka za siri, kwa sababu walikuwa na imani nao na chama hicho.

Nihitimishe makala hii kwa kurejea nilichohitimisha kwenye makala iliyopita

Barua Ya Chahali
[Free Access] Uchambuzi wa kiintelijensia kuhusu Mbowe kuachiwa huru, na tafsiri pana ya mwaliko aliopewa Ikulu kwa maongezi na Mama Samia
Utangulizi: Jana, Machi 4, 2022, Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) alitangaza nia ya kutoendelea na kesi iliyokuwa ikimkabili Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Mheshimiwa Freeman Mbowe na wenzake watatu ambao walikuwa wanajeshi wa jeshi la wananchi wa Tanzania (JWTZ), Mohamed Ling'wenya, Halfan Bwire na Adam Kasekwa. Uamuzi huo kisheria unaitwa “nolle prosequi…
Read more
2 months ago · Evarist Chahali

kwamba chambuzi hizi kuhusu kuachiwa na Mheshimiwa Mbowe ni endelevu.

Jumapili njema.

Share
Share this post
Ukimya wa Lissu Masaa 36 baada ya Mbowe na wenzake kuachiwa huru; mustakabali wa ajenda ya katiba mpya
www.baruayachahali.com
TopNewCommunity

No posts

Ready for more?

© 2022 Evarist Chahali
Privacy ∙ Terms ∙ Collection notice
Publish on Substack Get the app
Substack is the home for great writing