Barua Ya Chahali

Share this post
Ujumbe Maridhawa Kutoka Kwa Mtumishi wa Mungu Dkt Bagonza
www.baruayachahali.com

Ujumbe Maridhawa Kutoka Kwa Mtumishi wa Mungu Dkt Bagonza

Evarist Chahali
Jan 4, 2020
3
Share this post
Ujumbe Maridhawa Kutoka Kwa Mtumishi wa Mungu Dkt Bagonza
www.baruayachahali.com
Twitter avatar for @darmpya_Darmpya @darmpya_
"Wakati wa utawala wa makaburu wenye sera za ubaguzi wa rangi huko Afrika Kusini, mwanamke mmoja nweusi, aitwaye Zindiwe, jumapili moja akiwa amechelewa kwenda kanisani aliamua kusali kanisa la wazungu(weupe). Ndilo lilikuwa karibu na mahali alipoishi" Askofu Dkt. Benson Bagonza
Image

January 3rd 2020

5 Retweets13 Likes
Twitter avatar for @darmpya_Darmpya @darmpya_
"Aliingia kanisani na kuketi katika moja ya benchi na ibada ilianza. Ndani ya kanisa ilionekana wazi, ni yeye peke yake alikuwa mweusi. Taharuki ya kimya kimya iliendelea na kuvuruga uchaji ndani ya ibada" Askofu Dkt. Benson Bagonza #DARMPYABLOGUPDATES
Image

January 3rd 2020

4 Retweets9 Likes

Twitter avatar for @darmpya_Darmpya @darmpya_
"Mzee wa kanisa mmoja aliamua kumwendea, akamnong'oneza ainuke na kumfuata. Walifuatana hadi mlangoni. Yule mzee wa kanisa alimwambia Zindiwe kuwa amekosea kuingia hilo kanisa na kumtaka aondoke. Zindiwe aligoma na ndipo askari polisi walifika na kumwondoa" Dkt. Benson Bagonza
Image

January 3rd 2020

4 Retweets13 Likes

Twitter avatar for @darmpya_Darmpya @darmpya_
"Alipofika nyumbani, alipiga magoti kwa uchungu na kuanza kuomba. Ghafla alisikia sauti ikimtokea na kusema, " USILIE, HATA MUNGU HAYUMO NDANI YA KANISA HILO. Ushuhuda huu umechukuliwa kutoka kumbukumbu za Kanisa la Kimethodist la Afrika Kusini" Askofu Dkt. Benson Bagonza
Image

January 3rd 2020

1 Retweet8 Likes

Twitter avatar for @darmpya_Darmpya @darmpya_
"Mungu hawezi kuwa mahali penye ubaguzi hata kama waliopo wanamwabudu na kumuimbia. Haki (Justice) yaweza tofauti na UKweli (Truth). Kuna wakati Haki inakubaliana na Ukweli lakini kuna mara nyingi haki (Justice) itolewayo mahakamani ni tofauti na ukweli" Askofu Dk. Benson Bagonza
Image

January 3rd 2020

4 Retweets17 Likes

Twitter avatar for @darmpya_Darmpya @darmpya_
"Utawala wa makaburu ulikuwa na mamlaka ya kutunga na kutekeleza sheria. Raia wa Afrika Kusini walipokea mausia hekaluni kutii mamlaka hiyo kwa mujibu wa misahafu" Dkt. Benson Bagonza, Askofu wa Dayosisi ya Karagwe ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT)
Image

January 3rd 2020

4 Retweets18 Likes

Twitter avatar for @darmpya_Darmpya @darmpya_
"Zipo mamlaka zitokazo kwa Mungu na zisizotoka kwa Mungu. Misahafu inatutaka kutii kila mamlaka itokayo kwa Mungu. Nani atujulishe kuwa mamlaka fulani ndiyo inatoka kwa Mungu? Kwa hakika si mamlaka yenyewe. Haiwezi kutoka kwa Mungu kisha ikajitangaza" Askofu Dkt. Benson Bagonza
Image

January 3rd 2020

9 Retweets28 Likes

Twitter avatar for @darmpya_Darmpya @darmpya_
"Tamko la katiba ya nchi linalosema mtu hana hatia mpaka mahakama itakapomhukumu kuwa na hatia, linatiwa kasoro pale mtuhumiwa anapoanza kutumikia adhabu "isiyo rasmi", kukosa haki za kiraia, kukosa haki za kiutu, kukosa haki za kibinadamu." Askofu Dkt. Benson Bagonza
Image

January 3rd 2020

5 Retweets22 Likes

Twitter avatar for @darmpya_Darmpya @darmpya_
"Dola ya Mungu ina mihimili mitatu: Unabii, Ukuhani na Ufalme. Kila mhimili ulikuwa huru ili hata mwenye dhambi asihukumiwe bila kusikilizwa au kuonywa. Kuchanganya mihimili ni kumfukuza Mungu katika uwanja wa haki" Dkt. Benson Bagonza, Askofu wa Dayosisi ya Karagwe ya KKKT.
Image

January 3rd 2020

13 Retweets48 Likes

Mtumishi wa Mungu Dkt Bagonza a naendelea kuwa moja ya sauti adimu kabisa katika zama hizi za utawala wa kidikteta wa Jiwe aka “Dkt Evil.”

Tatizo ambalo Dkt Bagonza anajibidiisha kulishughulikia ni ukweli kwamba (a) kukaa kimya hakuwezi kumfanya Dkt Evil apatwe na huruma (b) actually ukimya wa wahanga wa udikteta unaweza kumpa moyo dikteta husika kuwa wanaafikiana nae (c) kukalia kimya jambo baya kunachangia ustawi wa jambo hilo.

Unaweza kuungana na Dkt Bagonza kwa kufanya sala/dua binafsi kwa Mola wako kuomba alete mwisho wa udhalimu unaoendelea.

Nimalizie kwa matangazo mawili. Kwanza nina furaha kuchapisha vitabu vitano vya bure. Vitabu hivi ni mkusanyiko wa twiti za kumhamasisha mtu katika mazingira mbalimbali sambamba na kusaidia kumfanya awe mtu bora/kuboresha ubora wake, kwa kimombo tunaita “motivational tweets.”

Vitabu hivi vitakuwa vinachapishwa kila mwezi na vitaendelea kutolewa bure. Baadaye nitatangaza utaratibu wa kuvipata (baada ya ule wa awali kuwataka watu wajisajili kutokuwa na ufanisi).

Tangazo jingine ni kuhusu ofa hii ya kuanzia mwaka 2020

Ndimi mtumishi wako wako,

Evarist Chahali

Comment
Share
Share this post
Ujumbe Maridhawa Kutoka Kwa Mtumishi wa Mungu Dkt Bagonza
www.baruayachahali.com

Create your profile

0 subscriptions will be displayed on your profile (edit)

Skip for now

Only paid subscribers can comment on this post

Already a paid subscriber? Sign in

Check your email

For your security, we need to re-authenticate you.

Click the link we sent to , or click here to sign in.

TopNewCommunity

No posts

Ready for more?

© 2022 Evarist Chahali
Privacy ∙ Terms ∙ Collection notice
Publish on Substack Get the app
Substack is the home for great writing