Uchunguzi Wa Kiintelijensia Kuhusu Wahusika Wa Udukuzi Mkubwa Kabisa Katika Historia ya Tanzania Mei 20, 2025: Waliofanya Udukuzi Huo Hawa Hapa
Muhtasari wa Kiintelijensia
Tarehe 20 Mei 2025, Tanzania ilikumbwa na shambulizi kubwa la kimtandao lililolenga taasisi muhimu za serikali na sekta binafsi. Akaunti rasmi ya Jeshi la Polisi Tanzania katika mtandao wa X (zamani Twitter) ilidukuliwa na kutumika kusambaza taarifa za uongo, zikiwemo madai ya kufariki kwa Rais Samia Suluhu Hassan, pamoja na picha za matusi na maudhui machafu.
Shambulizi hilo, ambalo lilitokea kwa mkondo wa awamu kadhaa, liliacha maswali mazito kuhusu nani hasa waliohusika. Ripoti hii inaweka bayana kuwa mhusika wa ndani hana uwezo wa kiteknolojia kutekeleza oparesheni ya kiwango hicho. Kama mhusika hakuwa wa ndani, ni nani basi? Endelea kusoma.