Barua Ya Chahali

Barua Ya Chahali

Share this post

Barua Ya Chahali
Barua Ya Chahali
Uchambuzi wa kiintelijensia: kauli tete za Jenerali Muhoozi, mtoto wa Rais Museveni wa Uganda ni mzaha tu au ni ishara za mambo yajayo?
Copy link
Facebook
Email
Notes
More
Simulizi za Jasusi

Uchambuzi wa kiintelijensia: kauli tete za Jenerali Muhoozi, mtoto wa Rais Museveni wa Uganda ni mzaha tu au ni ishara za mambo yajayo?

Evarist Chahali's avatar
Evarist Chahali
Nov 12, 2022
∙ Paid
3

Share this post

Barua Ya Chahali
Barua Ya Chahali
Uchambuzi wa kiintelijensia: kauli tete za Jenerali Muhoozi, mtoto wa Rais Museveni wa Uganda ni mzaha tu au ni ishara za mambo yajayo?
Copy link
Facebook
Email
Notes
More
Share

Read Barua Ya Chahali in the Substack app
Available for iOS and Android

Oktoba 3 mwaka huu, mtoto wa Rais Yoweri Museveni, Jeneral Muhoozi Kainerugaba, alititwi kwamba ingechukua wiki 2 tu kwa yeye na jeshi lake kuiteka Nairobi

Twitter avatar for @mkainerugaba
Muhoozi Kainerugaba @mkainerugaba
It wouldn't take us, my army and me, 2 weeks to capture Nairobi.
1:02 PM ∙ Oct 3, 2022
20,736Likes3,960Retweets

Japo Jenerali huyo anafahamika kwa kauli zake tete katika mtandao huo wa kijamii, twiti hiyo ya kutishia kuvamia Kenya ilizua taharuki mtandaoni na nje ya mtandaoni.

Lakini kabla ya tishio hilo, Muhoozi alishazua tafaruku nyingine kwa “kumlaumu” Rais wa zamani wa Kenya, Uhuru Kenyatta, kwamba alipaswa kubadili katiba ya nchi hiyo ili atawale muhula wa tatu. Na akaenda mbali zaidi na kudhihaki katiba na utawala wa sheria akidai huko Uganda wanajali mapinduzi tu.

Kana kwamba alichofanya kilikuwa tukio la kishujaa, siku chache baadaye, afande huyo aliyekuwa na cheo cha luteni jenerali alipandishwa cheo na baba yake kuwa jenerali kamili. Hata hivyo, kupandishwa cheo huko kuliambatana na Muhoozi kuondolewa kwenye ukamanda wa jeshi la nchi kavu.

Baadaye baba yake, Rais Museveni, aliwaomba radhi Wakenya kwa kauli za mwanae, na baadaye tena Muhoozi mwenyewe alimuomba radhi Rais mpya wa Kenya William Rutto.

Je tukio hilo - na mengineyo kadhaa huko Twitter - ni utani tu wa Muhoozi (huwa pia anafanya “utani” kuhusu mabinti warembo) au ni kiashiria cha “yajayo mbeleni”?

Makala hii inafanya tathmini ya kiintelijensia kwa kutumia mbinu inayofahamika kama “Analysis of Competing Hypotheses” (ACH), mbinu inayoaminika kuwa ni bora zaidi katika kufanya uchambuzi wa kiintelijensia. Mbinu hiyo inashindanisha dhana mbalimbali kabla ya kubaki na dhana moja inayohitimisha uchambuzi.

This post is for paid subscribers

Already a paid subscriber? Sign in
© 2025 Evarist Chahali
Privacy ∙ Terms ∙ Collection notice
Start writingGet the app
Substack is the home for great culture

Share

Copy link
Facebook
Email
Notes
More