Barua Ya Chahali

Share this post
Uchambuzi Kuhusu Mashinji Kuhama Chadema Na Kujiunga na CCM
www.baruayachahali.com

Uchambuzi Kuhusu Mashinji Kuhama Chadema Na Kujiunga na CCM

Kuna Tatizo Ndani Ya Chadema Lakini Kama Ilivyo Dhambi Kuikosoa CCM Ndivyo Ilivyo Pia Kwa Chadema

Evarist Chahali
Feb 19, 2020
10
Share this post
Uchambuzi Kuhusu Mashinji Kuhama Chadema Na Kujiunga na CCM
www.baruayachahali.com

Kwamba Mashinji angehama wala halikuwa jambo la “if” (endapo) bali “when” (lini). Na hatimaye jana mwanasiasa huyo aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama kikuu cha upinzani, Chadema, alitangaza kuhama rasmi chama hicho na kujiunga na CCM.

Na kama ilivyo kawaida, wafuasi wa Chadema, wakarejea kauli yao maarufu kila mmoja wao anapowakimbia, kudai “Mashinji alikuwa pandikizi la CCM.”

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
This doesn't sound too good. Nitakueletea analysis fupi kesho panapo majaliwa. Ila kwa kifupi tu, kama CDM walijua kuwa Sumaye na Mashinji ni mapandikizi, why wait until "waunge mkono jitihada" ndo watuambie "we knew it"? Something somewhere isn't right. Kesho, inshallah!

millardayo @millardayo

Aliyekuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA Dkt.Vincent Mashinji ametangaza rasmi kuondoka CHADEMA na kuhamia CCM leo February 18, 2020 na kupokelewa na Humphrey Polepole katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba DSM. #MllardAyoUPDATES https://t.co/CsNAO2CXQJ

February 18th 2020

3 Retweets57 Likes

Wengine wakajaribu kugeuza tuio hilo la kuhama kwa Mashinji kuwa ni ushindi kwa Chadema kwa vile hivi karibuni chama hicho kilipata Katibu Mkuu John Mnyika aliyechukua nafasi ya Mashinji. Ndugu yangu Ansbert Ngurumo akaandika haya

Twitter avatar for @ngurumoAnsbert Ngurumo @ngurumo
Kunyamaza maana yake si kutojua. Haikuwa bahati mbaya Mashinji kunyang'anywa ujaribu mkuu, akapewa John Mnyika. Mpango ulikuwa hivi: Mwenyekiti awe Sumaye au Mwambe, katibu mkuu awe Mashinji. Leo wote wangekuwa wamehamia CCM, eti "kuua Chadema!" Tuheshimu silent operations!
Image

February 18th 2020

106 Retweets1,404 Likes

Namheshimu sana Bwana Ngurumo lakini ninafadhaika kuona watu wenye uelewa mkubwa kama yeye, na ambao huenda wakitoa ushauri watasikilizwa, nao wanafanya siasa.

Haihitaji akili kubwa kubaini kuwa lolote “baya” litakalosemwa na Chadema muda huu, hata liwe na ukweli mkubwa kiasi gani, litatafsiriwa kuwa ni sawa na simulizi ya “sizitaki mbichi hizi” ya sungura aliyeshindwa kufikia ndizi mkunguni.

Image result for sizitaki mbichi hizi

Kwamba sungura kila alipojaribu kurukia ndizi mkunguni hakuzifikia, na “alipokubali yaishe” akajifanya kusema “sizitaki mbichi hizi.” Stori hii hutumika kueleza kutapatapa kwa mtu aliyekosa kitu flani kisha akaishia kukiponda. Ndio wanachofanya ndugu zetu wa Chadema kila wanapopatwa na pigo la kuondokewa na viongozi/wanachama wao maarufu.

Mtu pekee ambaye hadi leo Chadema wanashindwa kumponda ni Lowassa, na ni kwa sababu za wazi. Aliwaingiza mkenge vibaya. Aliwapa matumaini hewa. Walimgeuza mungu-mtu. Na yayumkinika kuhisi kuna baadhi ya wana-Chadema hawaamini kama kweli Lowassa amewaacha kwenye mataa.

Na japo ni kweli kwamba Chadema kama vyama vingine vya upinzani imekuwa inahujumiwa vya kutosha na CCM kwa kushirikiana na Idara ya Usalama wa Taifa, kasoro kadhaa ndani ya chama hicho kinarahisisha hujuma hizo.

Kama kuna kosa ambalo linaweza kabisa kugharimu uhai wa Chadema ni uamuzi wake wa kumpokea Lowassa mwaka 2015. Ni hivi, huhitaji kuwa mwelewa wa stadi za siasa kama mie mtumishi wako kubaini kwamba ni ukosefu wa busara wa hali ya juu kwa Chadema kumwandama Lowassa tangu Februari 2006 hadi Julai 2015 - miaka tisa hiyo - huku wakimtaja kama “papa la ufisadi,” kisha kumpokea takriban miezi mitatu tu kabla ya uchaguzi mkuu na kumfanya mgombea wao wa nafasi ya urais.

Kibaya zaidi, Lowassa huyo waliyempokea alikuwa “makapi” ya CCM. Again, haikuhitaji busara kubwa kufahamu kuwa kama hata CCM na ubovu wake ilimwona Lowassa hawafai, sijui Chadema walikuwa wanategemea nini kutoka kwake.

Wanufaika wakubwa wa uamuzi huo mbovu ni

(a) Lowassa mwenyewe: hebu fikiria, watu waliokuandama kwa miaka tisa mfulizo, wanapohangaika kuzunguka nchi nzima kukanusha kilekile walichokuwa wakikutuhumu…Naam, badala ya kusaka urais, kampeni ya Lowassa huko Chadema ilitawaliwa na ajenda moja kuu: Lowassa sio fisadi. Na waliokuwa wakisema hayo ni hao hao waliokuwa wakimuita fisadi. Kwahiyo Chadema walimchafua Lowassa na kisha wakalazimika kumsafisha, tena kwa gharama kubwa, kwani tangu chama hicho kililazimika kuitosa ajenda yake muhimu ya kupinga ufisadi.

(b) CCM: Kiongozi mmoja wa ngazi za juu wa chama hicho aliniambia, namnukuu, “Bwana Chahali, uchaguzi huu ungekuwamgumu sana kwetu kutokana na skandali za miaka 10 tunayomaliza. Lakini jamaa zetu wameturahisishia kwa kukwepa kuzungumzia ufisadi baada ya kumpokea mwanasiasa aliyekuwa kama nembo ya ufisadi kwenye chama chetu…”

Kwa kuitelekeza ajenda ya vita dhidi ya ufisadi, sio tu CCM walipata ahueni bali pia wakaipora ajenda hiyo na kuifanya sera muhimu ya mgombea wao Magufuli.

(c) Kitengo: Idara ya Usalama wa Taifa imekuwa ikivihujumu vyamavya upinzani nonstop. Lakini kwa Lowassa (ambaye kitambo alikuwa na “mahusiano mazuri” na taasisi hiyo) kuhamia Chadema, ilitoa fursa kubwa kwa Idara hiyo kuingiza lundo la watu wao, sambamba na kutengeneza mazingira ya kujenga mtandao wa watoa habari ndani ya chama hicho. Hiindio athari kubwa zaidi ya uamuzi wa kumpokea Lowassa: Chadema imesheheni mapandikizi yanayopigana kufa na kupona kukiangamiza chama hicho kutokea ndani.

Lakini hata tukiamua kusema “yaliyopita si ndwele, tugange yajayo,” bado kuna maswali magumu ambayo Chadema wanapaswa kujiuliza lakini wanayakwepa makusudi kwa sababu hawataki “kumuudhi Mbowe.” Maswali hayo ni pamoja nahilo kubwa zaidi la ujio wa Lowassa. Kwa mfano, ni kweli kwamba Lowassa “alinunua” nafasi hiyo? Ni wazi kuwa kama ni kweli, lazima mtu flani alipaswa kung’oka na Lowassa.

Twitter avatar for @IddUpeteIdd Amiri Upete @IddUpete
Na Lowassa aliletwa na Mbowe anakuwaje pandikizi. Uwezo wetu wa kufikiri ni mdogo. Tatizo chama ni cha mtu mmoja analeta watu halafu wapoondoka inatafutwa sababu isiyo sababu.

Evarist Chahali @Chahali

Ndo hapo sasa! https://t.co/DX2F8W2KRJ

February 18th 2020

1 Retweet

Lakini hata tukiamua kumsahau Lowassa, je nani alimfikisha Mashinji kwenyenafasi ya Ukatibu Mkuu? Je kama tunakubaliana na “sizitaki mbichi hizi” za Chadema kuhusu Mashinji, kwamba ni “pandikizi la CCM,” je ni nani aliyelifikisha “pandikizi hilo” hadi kwenye nafasi nyeti na muhimu wa Ukatibu Mkuu wa chama? Na je kama Mashinji ni pandikizi, huyo “aliyembeba” mpaka kufikia ukatibu mkuu nae sio “pandikizi” pia?

Twitter avatar for @hajimtete1Haji Mtete @hajimtete1
@Chahali Dr Vicent Mashinji aliletwa na @freemanmbowetz anakuaje pandikizi ,au alikua anajipandia mbegu .

February 18th 2020

Kitambo, mie nimekuwa nikionyesha kutoridhishwa na utendaji kazi wa kitengo cha intelijensia cha chama hicho (kama bado kipo hai)

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
1/2 Meya wa jiji la Arusha ahamia CCM: I know tutasikia usual reaction ya "acha aondoke" lakini this doesn't look good. Arusha ni moja ya ngome kuu za Chadema and this is a huge loss. Two things: 1. Intelijensia ya CDM is dead, hence failure to pre-empt matukio kama haya...2/2
Image

November 19th 2019

1 Retweet17 Likes
Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Ni hivi, aidha intelijensia ya Chadema imekufa au imeenda likizo au labda hii #hamahama ni mkakati wao au hakuna anayejali alimradi ruzuku inaendelea kuingia kwenye chama. Subiri wimbi la wabunge wa viti maalum kwenye hiyo #hamahama, naambiwa wapo kwenye majadiliano ya bei

Ng'wanangwa @Mugaka_N

Mzazi atabeba lawama zake, japo wakati mwingine atakuwa amezidiwa mbinu na mabinti na washirika wao. Naona ni wakati mwafaka wa Mzazi kukubali kuzidiwa na kutafuta msaada wa jinsi ya kukabiliana na hali hiyo. https://t.co/gpvwwj2Art

October 7th 2018

2 Retweets12 Likes
Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Hivi nyie Chadema hamna kabisa intelijensia? Nimepewa taarifa zimenichefua sana. Mtoa habari anasema bayana "Kaka hivi hao Chadema hawayajui haya au wameshazowea kuonewa mpaka wanapuuzia uhuni wa aina hii?" Mkiambiwa "chama dhaifu" mnakuwa wakali. Huu ndo udhaifu wenyewe

September 12th 2018

5 Retweets62 Likes
Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Kuna kikao kimefanyika Dar na uthibitisho upo wa jinsi ya kuwezesha ushindi wa mgombea wa CCM huko Ukonga. As I'm writing tweet hii, mmeshalizwa kwenye kura kichobaki ni voting siku ya uchaguzi kama kutimiza wajibu. Kwanini mnaruhusu uhuni huu? Au you part of this nasty game?

September 12th 2018

2 Retweets21 Likes

Ni muhimu kukumbuka kuwa moja ya sababu zilizopelekea Chadema kuwa ilipo leo ni kuibua skandali mbalimbali za ufisadi zilizogubika utawala wa Jk, kuanzia Richmond, EPA, Kagoda, Buzwagi, Kiwira, nk. Na kilichowezesha chama hicho kuwa kinara wa kuibua slandali hizi ni intelijensia ya chama hicho ambayo sio tuilikuwa nzuribali pia iliaminiwa na baadhi ya watumishi wa Idara ya Usalama wa Taifa waliofikia hatua ya kujitoa mhanga kukipa chama hicho siri za serikali.

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
"Maafisa wa Idara ya Usalama wa Taifa walivujisha taarifa nyeti (kuhusu ufisadi) kwangu." ~ Dkt Slaa

Sarah Hermitage @Chomachomp

Tiss Officials Leaked Sensitive Documents to Dr Slaa https://t.co/JTbr9AXfzr via @allafrica

February 7th 2018

4 Retweets9 Likes

Lakini yaelekea sasa intelijensia pekee iliyobaki ya Chadema ni ramli za “jasusi” Yeriko

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
JASUSI wa CDM kazini 🤣🤣M0R
Image

February 16th 2020

1 Retweet37 Likes

Ungetegemea “jasusi” akiwezeshe chama chake kufanya kile majasusi hukifanya: PREEMPTION. Yaani kabla Lowassa hajatangaza kuhama, majasusi wa chama hicho wangeweka hilo hadharani, na pengine kumtimua kabla hajahama. Kabla Waitara, sijui Meya wa Arusha, kabla ya Mr Zero Sumaye hajahama, na jana, kabla Mashinji hajahama, wao ndio wangechukua first step.

Kusubiri mtu atangaze kuhama ndio waje na porojo za “oh ndio maana hatukumpa tena Ukatibu Mkuu,” ni kutufanya - ashakum si matusi - mafala.

Lakini hii hama hama ina atahri zozote kwa Chadema? Well, tofauti na majigambo kuwa hamahama haina athari zozote, kwamba “acha tu waondoke,” ukweli ni kwamba hama hama hiyo ina athari kubwa lakini sio za hapo kwa hapo.

Hebu jiulize katika muda huu, ukimsikia Mbunge flani wa Chadema akidai kuwa kamwe hawezi kuhamia CCM, UTAMWAMINI? Kuwa mkweli. Maana hata akina Lowassa,

Twitter avatar for @UdakuSpeciallyUdaku Special @UdakuSpecially
Lowassa: "Ujumbe wa Magufuli ni kunitaka nirejee CCM, ila nilikataa"
dlvr.it/QBHw9g
Image

January 15th 2018

Sumaye

Twitter avatar for @darmpya_Darmpya @darmpya_
"Mimi nilipotoka CCM nilitoka kwa hiyari yangu. Siwezi kurudi kwa kushurutishwa na mtu yeyote. Siyo maneno tu yanayotutaka turudi huko, bali yapo mambo mengi tunatendewa ili turudi lakini kila mtu ana uamuzi wake" Mhe. Fredrick Sumaye, Mwenyekiti wa CHADEMA kanda ya Pwani
Image

March 5th 2019

66 Retweets489 Likes

na Mashinji

Twitter avatar for @Vicent_mashinjiDr. Vincent Mashinji @Vicent_mashinji
Napokea simu nyingi eti nahamia CCM, mi si MJAMAA. Mi ni mlengo wa kibepari. Siamini kwenye “zidumu fikra za mwenyekiti” Ninaamini katika “nguvu na mamlaka ya umma” Naomba ndugu zangu muwe na amani kabisa! Nitaendelea kutumikia CHADEMA kwa makini na kutimiza ndoto za Watanzania.
Image

November 22nd 2017

33 Retweets335 Likes

walisema kamwe hawawezi kuhamia CCM, lakini baadaye wakahamia huko.

Kwahiyo moja ya athari za harakaharaka ni kwamba kwa sasa ni vigumu kumwamini mwanasiasa yeyote yule wa Chadema anayedai hatohama chama hicho/hatojiunga na CCM.

Lakini kubwa zaidi ni sintofahamu waliyonayo Watanzania wengi kuhusu mustakabali wa chama hicho kikuu cha upinzani hasa swali hili muhimu: WHO IS NEXT? NANI ANAFUATA (baada yaMashinji)?

In long run, hata wafuasi wa damu wa chama hicho wanaweza kupoteza imani kwa sababu hawajui “kesho nani atatangaza kuunga mkono jitihada.”

Pengine athari kubwa zaidi ya zote ipo kwenye ukweli kwamba kundi muhimu - na kubwa zaidi - la wapiga kura nchini Tanzania ni watu wasio wanachama wa chama chochote. Hawa ndio wanaopaswa kushawishiwa kukisapoti chama husika na/au mgombea wake. Ni hivi, CCM haihitaji kuwashawishi wafuasi wake kukipigia kura chama hicho. Na CCM haihitaji kuwashawishi wafuasi wa upinzani wakipe kura chama hicho. Kadhalika, vyma vya upinzani navyo havihitaji kuwashawishi wana-CCM wavipigie kura. Vilevile havihitaji kuwashawishi wafuasi wao wavipigie kura vyama hivyo. Kundi linalohitaji kushawishiwa kutoa kura ni hilo la wasio na vyama. Na hawa kwa sasa wanaweza kuwa wameanza kupoteza matumaini kwa Chadema. Inafikia mahala watu wanasema “kukipigia kura chama hiki ni kupoteza kura yangu.”

Kadhalika, japo Mashinji amehama akiwa Katibu Mkuu wa zamani, ukweli ni kwamba huyu ni katibu mkuu wa pili wa chama hicho “kukimbia.” Na kibaya zaidi, MASHINJI ANAJUA MENGI. Mark these words: Tutamsikia sana huyu bwana. Na yawezekana akawa mtu hatari kabisa aliyetoka Chadema. Time will tell.

Nimalizie uchambuzi huu kwa kutanabaisha kuwa ni wazi utawakera wahusika kwa sababu kama wenzao wa CCM, hawataki kabisa kukosolewa. Lakini kuuchukia ukweli hakuufanyi kuwa uongo. Sie wengine tutaendelea kusema ukweli hata kama itamaanisha kudhihakiwa na akina Yeriko.

Ushauri wangu kwa Chadema ni kutambua kuwa kuna tatizo la MAPANDIKIZI, na linahitaji kufanyiwa kazi haraka. Maana ili kuweza kutatua tatizo, hatua ya kwanza na ya muhimu kabisa ni kutambua uwepo wa tatizo. Unfortunately hadi muda huu, Chadema hukumbuka tu suala la mapandikizi pindi mmoja wao anapowakimbia. Hakuna anayehangaika kujiuliza WHO IS NEXT?

Ndimi mtumishi wako,

Evarist Chahali

Comment
Share
Share this post
Uchambuzi Kuhusu Mashinji Kuhama Chadema Na Kujiunga na CCM
www.baruayachahali.com

Create your profile

0 subscriptions will be displayed on your profile (edit)

Skip for now

Only paid subscribers can comment on this post

Already a paid subscriber? Sign in

Check your email

For your security, we need to re-authenticate you.

Click the link we sent to , or click here to sign in.

TopNewCommunity

No posts

Ready for more?

© 2022 Evarist Chahali
Privacy ∙ Terms ∙ Collection notice
Publish on Substack Get the app
Substack is the home for great writing