Barua Ya Chahali

Share this post
[#TumiaVPN: 'Mwanaharakati Huru' Musiba Amchimba Mkwara @MagufuliJP, Aonya Endapo Jina Lake Litakatwa Kamati Kuu
www.baruayachahali.com

[#TumiaVPN: 'Mwanaharakati Huru' Musiba Amchimba Mkwara @MagufuliJP, Aonya Endapo Jina Lake Litakatwa Kamati Kuu

Evarist Chahali
Aug 20, 2020
1
Share this post
[#TumiaVPN: 'Mwanaharakati Huru' Musiba Amchimba Mkwara @MagufuliJP, Aonya Endapo Jina Lake Litakatwa Kamati Kuu
www.baruayachahali.com

Cyprian Musiba, mmoja wa “wapigadebe” mahiri wa Rais Magufuli, anayejiita “mwanaharakati huru,” na ambaye anawania kupata ridhaa ya CCM kuwania ubunge wa jimbo la Mwibara ametuma ujumbe mkali kwa mwenyekiti wa taifa wa chama hicho na Kamati Kuu yake.

Katika ujumbe wa twiti ambayo aliandika kisha akaifuta, Musiba ambaye amekuwa mstari wa mbele kuwachafua watu mbalimbali anaodai ni wapinzani dhidi ya Rais Magufuli, amemuonya kiongozi huyo kuwa endapo jina lake halitopitishwa basi “patachimbika.”

Baadhi ya wana-CCM sio tu wanaona hatua hiyo kama dharau ya waziwazi ya “mpambe” huyo kwa Rais, bali pia wanatafsiri vitisho hivyo kama kumfanya Rais mateka wa kisiasa, kwamba “kila kada aliyemtetea Rais basi apewe upendeleo maalum.”

Musiba, ambaye pia ni mmiliki wa magazeti kadhaa, amewatahadharisha pia Katibu Mkuu wa CCM, Dkt Bashiru, na Mwenezi, Humphrey Polepole, kuwa anafahamu “wamepanga kumhujumu, na ole wao kwani yeye si saizi yao.”

Habari hii ni endelevu.

Nimalizie kwa tangazo

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Pata nakala yako ya kitabu cha #Shushushu leo. Pia waweza kulipia #JaridaLaUjasusi kwa namba hiyo hiyo!
Image

August 19th 2020

1 Like
Share
Share this post
[#TumiaVPN: 'Mwanaharakati Huru' Musiba Amchimba Mkwara @MagufuliJP, Aonya Endapo Jina Lake Litakatwa Kamati Kuu
www.baruayachahali.com
TopNewCommunity

No posts

Ready for more?

© 2022 Evarist Chahali
Privacy ∙ Terms ∙ Collection notice
Publish on Substack Get the app
Substack is the home for great writing