Barua Ya Chahali

Share this post
Toleo Maalum: Ripoti Ya CAG Imethibitisha Tunalokwepa Kusema Kuhusu MAGUFULI
www.baruayachahali.com

Toleo Maalum: Ripoti Ya CAG Imethibitisha Tunalokwepa Kusema Kuhusu MAGUFULI

Awamu ya Tano Ya MAGUFULI inaweza kuwa ya kifisadi zaidi kuliko zote zilizotangulia

Evarist Chahali
Apr 11, 2019
23
Share this post
Toleo Maalum: Ripoti Ya CAG Imethibitisha Tunalokwepa Kusema Kuhusu MAGUFULI
www.baruayachahali.com

Hatimaye mkwara wa Mtu Mfupi Ndugai umeshindwa kumzuwia CAG Profesa Mussa Assad kuwasilisha ripoti yake ya ukaguzi na udhibiti wa fedha za serikali kwa mwaka wa fedha 2017/2018.

Twitter avatar for @NuktaTanzaniaNukta Tanzania @NuktaTanzania
Kikao cha saba cha Mkutano wa 15 wa Bunge la 11 kinachofanyika leo jijini Dodoma kimeanza kwa uwasilishaji wa Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kuhusu ukaguzi wa Mashirika ya Umma kwa mwaka wa fedha 2017/2018.
Image

April 10th 2019

Hilo dogo.

Kubwa ni (a) yayumkinika kuhitimisha kuwa jitihada za Mtu Mfupi Ndugai dhidi ya Profesa Assad kwamba “Bunge halitafanya kazi na CAG” zilikuwa zinafanywa kwa rimoti na Magufuli mwenyewe kwa sababu (b) ni dhahiri kuwa utawala wake sio tu umegubikwa na ufisadi mkubwa bali pia unaweza kuingia kwenye kumbukumbu za nchi yetu kama utawala wa kifisadi zaidi kuliko yote.

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
#IStandWithCAG: Ripoti Kamili ya CAG Kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 Kama Ilivyowasilishwa April 10, 2019
Ripoti Nzima ya CAG Kwa Mwaka wa Fedha 2017/2019 Iliyowasilishwa 10/04/2019Ripoti Nzima ya CAG Kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 iliyowasilishwa 10/04/2019. Nyaraka hii imeunganisha ripoti zifuatazo Korijenda ya ripoti ya serikali kuu Ripoti ya Serikali kuu Ripoti kuu ya miradi ya maendeleo Ripoti kuu ya Mamlaka za Serikali za Mtaa Ripoti kuu ya Mashirika ya Umma Ripoti y…bit.ly

April 11th 2019

Watanzania wanapaswa kumuomba msamaha Rais Kikwete. Na hata Rais Mkapa. Na pengine hata Rais Mwinyi. Hawa wote - na hasa JK- tuliwaandama mno kuhusu ufisadi. Ikumbukwe kuwa pamoja na mapungufu yao, angalau hawakufanya jitihada za kutunyima access ya habari kuhusu wanavyotuongoza.

Naam, sheria kandamizi dhidi ya vyombo vya habari ziliendelea kuwepo/kutumika, lakini hakuna mmoja wao anayefikia kiwango alichofikia Magufuli: sio tu amefanikiwa kuviziba mdomo vyombo vya habari bali pia ameanzisha “toilet papers” kadhaa zinazofanya kazi kuu mbili, kummwagia sifa kila kukicha na kutuandama tunaomkosoa kihalali.

Kwa bahati mbaya - au pengine makusudi - ishu hii nayo itakufa kimya kimya. Kwa upande mmoja, mbinu ya Magufuli kudhibiti vyombo vya habari itamkinga dhidi ya habari hii kuendelea kutawala vichwa vya habari. Kwa upande mwingine, “ukitaka kumficha kitu Mtanzania, kiweke kwenye maandishi. Na ushahidi mwepesi ni huu pichani

Angalia “idadi ya views” kisha linganisha na jitihada kubwa zinazofanyika kuhamaisha “views za YouTube” pindi wasanii wetu wanapotoa video zao. Aliyewaroga Watanzania alihakikisha wanapuuzia vitu vya muhimu na kuendekeza vitu vya ovyo ovyo. Bad news ni kwamba huyo aliyewaroga Watanzania naye alirogwa, akapata uchizi, akagongwa na basi la Skandinavia, akafariki papo hapo. What this means? HAMPONI (wanasema aliyekuroga akifa, huponi).

Lakini lawama hazijengi. Na mabadiliko huanza kwa hatua ndogo ndogo. Unaonaje badala ya kulaumu wengine, wewe binafsi ukawa mfano kwa kuanza kusoma taratibu ripoti hii kisha ukawaelewesha wengine ambao hawajabahatika kuisoma.

Ripoti hii ni muhimu sana kwa mustakabali wa taifa letu ambalo kwa hakika linaelekea kubaya. Magufuli anawahadaa Watanzania kuwa “vyuma vimekaza kwa sababu watu walizowea kupiga dili.”

Twitter avatar for @JamiiForumsJamii Forums @JamiiForums
Rais Magufuli: Ndugu zangu naomba niwahakikishie kuwa Serikali iko imara na ndio maana mmeanza kusikia kelele - Kelele hizo ni za wale waliokuwa wamezoea vya bure. Wapo wanaosema vyuma vimekaza, kama vimekaza si uende ukalime? #JFLeo #MagufuliMbinga

April 7th 2019

18 Retweets246 Likes

Lakini ukweli mchungu ni kwamba vyuma vimekaza kwa sababu kuna ufisadi mkubwa kabisa unaoendelea kimyakimya, unaomhusisha Magufuli na genge lake la Kanda ya Ziwa. Na kama unahangaika kutafuta mfano hai, angalia ishu hii ya LUGUMI ambayo ni mtu wa karibu wa Magufuli kama alivyo Bashite.

Kwahiyo wakati Wadanganyika mnakebehiwa kwamba vyuma vimekaza kwa vile nyie ni wapigadili, akina LUGUMI wanazidi kufakamia keki ya taifa.

Na hapa bado hatujui mpwa wa Magufuli pale Hazina safari hii amefisadi kiasi gani, lakini ni muhimu kukumbuka kuwa wakati awali tulidhani pesa iliyopigwa Hazina ni TRILIONI 1.5, baadaye ikabainika kwamba kiwango halisi ni TRILIONI 2.4.

Nimalizie toleo hili maalum kwa kukusihi tena na tena, soma ripoti ya CAG, kisha waelimishe wenzetu ambao kwa sababu moja au nyingine hawawezi kuisoma. Ombi langu jingine kwako ni kutafakari mustakabali wa nchi yetu kwa kuzingatia lindi hili kubwa la ufisadi wa kihistoria. Hatma ya Tanzania yetu ipo mkononi mwako.

Nakutakia siku njema, tukutane Jumatatu ijayo

Comment
Share
Share this post
Toleo Maalum: Ripoti Ya CAG Imethibitisha Tunalokwepa Kusema Kuhusu MAGUFULI
www.baruayachahali.com

Create your profile

0 subscriptions will be displayed on your profile (edit)

Skip for now

Only paid subscribers can comment on this post

Already a paid subscriber? Sign in

Check your email

For your security, we need to re-authenticate you.

Click the link we sent to , or click here to sign in.

TopNewCommunity

No posts

Ready for more?

© 2022 Evarist Chahali
Privacy ∙ Terms ∙ Collection notice
Publish on Substack Get the app
Substack is the home for great writing