#TanzaniaRoyalTour: tathmini ya kijasusi
Filamu ya Tanzania Royal Tour iliyorekodiwa katika maeneo mbalimbali ya Tanzania Bara na Zanzibar yenye lengo la kutangaza duniani vivutio vya utalii na fursa za uwekezaji zinazopatikana nchini Tanzania ilizinduliwa rasmi jijini New York, Marekani April 18 mwaka huu.
Filamu hiyo ilianza kurekodiwa Agosti 29, 2021 na muongozaji wa filamu wa kimataifa, Peter Greenberg aliyeambatana na Rais Samia Suluhu Hassan, ambapo kwa pamoja walitembelea vivutio mbalimbali ikiwemo Mji Mkongwe na hifadhi za Taifa zinazopatikana Tanzania bara.
Tathmini ya kiintelijensia ifuatayo inajikita yangu mwanzo wa wazo la filamu hiyo, maelezo ya awali kabla na wakati wa kurekodi, uzinduzi unaoendelea huko Marekani, na mapokeo miongoni mwa Watanzania na watu wasio Watanzania, ndani na nje ya Tanzania. Kadhalika, tathimini inaangalia fursa na changamoto kwa filamu hiyo na kuhitimisha kwa ushauri wa nini kifanyike ili filamu hiyo ifikie malengo kusudiwa badala ya kusahaulika siku chache baada ya uzinduzi.