Barua Ya Chahali

Share this post
Tamko la Lissu Kuwa Yeye na Lema Watarejea Tanzania Mwezi Machi Linamaanisha Masharti Aliyoipa Serikali Kuhusu Usalama Wake Yametimizwa?
www.baruayachahali.com

Tamko la Lissu Kuwa Yeye na Lema Watarejea Tanzania Mwezi Machi Linamaanisha Masharti Aliyoipa Serikali Kuhusu Usalama Wake Yametimizwa?

Evarist Chahali
Jan 3
Share this post
Tamko la Lissu Kuwa Yeye na Lema Watarejea Tanzania Mwezi Machi Linamaanisha Masharti Aliyoipa Serikali Kuhusu Usalama Wake Yametimizwa?
www.baruayachahali.com

Katika hotuba yake kwa taifa kuaga mwaka 2021 na kuukaribisha mwaka 2022, Makamu Mwenyekiti wa Chadema Taifa, na mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020, Mheshimiwa Tundu Lissu, alieleza kuwa yeye aliyepo Ubelgiji kwa sasa, na kiongozi mwenzie wa chama hicho, Mheshimiwa Godbless Lema, aliyepo Canada, watarejea Tanzania mwezi Machi mwaka huu.

Twitter avatar for @mshambuliajiMaulid Kitenge @mshambuliaji
“Kamati Kuu imeazimia miye na mwenzangu Lema kurejea nyumbani Tanzania mwezi March Mwaka 2022 kuendeleza mapambano ya kisiasa nchini” Makamu Mwenyekiti wa Chadema Tundu Lissu, akitoa hotuba ya kufunga mwaka 2021 ya Chama hicho na kutoa mwelekeo wa Chadema mwaka 2022.
Image

December 31st 2021

121 Retweets1,648 Likes

Hata hivyo, Desemba 8 mwaka jana, mwanasiasa huyo alinukuliwa na gazeti la Mwananchi akitanabaisha kuwa serikali inapaswa kumhakikishia usalama wake ili aweze kurudi nchini Tanzania. Alisisitiza serikali ikitoa kauli ya kuhakikisha usalama wake, yeye hatukuwa na sababu ya kuendelea kuishi Ubelgiji.

Je yawezekana serikali imetoa tamko la siri kwa Mheshimiwa Lissu kumhakikishia usalama wake hadi kufikia hatua ya kutangaza kuwa atarudi Tanzania mwezi Machi, pamoja na Mheshimiwa Lema?

Japo sina shaka na maelezo ya Mheshimiwa Lissu kuwa Kamati Kuu ya chama hicho imewataka yeye na Mheshimiwa Lema kurudi lakini napata shida kuelewa Kamati Kuu hiyo imewezaje kuhakikisha kuwa kurudi kwa viongozi hao wawili hapo mwezi Machi hakutoathiri usalama wao.

Nihitimishe kwa kutanabaisha kuwa sitarajii kama jibu la swali hilo liitapatikana, lakini natumaini litaamsha tafakuri kuhusu “siasa za hadharani” na “siasa za faraghani.”

Heri ya mwaka mpya

Tangazo: Kozi mbalimbali zilizokuwa zinatolewa na chuo changu cha mtandaoni cha AdelPhil Online Academy sasa zitakuwa zinapatikana katika ukurasa huu wa Barua ya Chahali. Karibuni sana 🙏

Share this post
Tamko la Lissu Kuwa Yeye na Lema Watarejea Tanzania Mwezi Machi Linamaanisha Masharti Aliyoipa Serikali Kuhusu Usalama Wake Yametimizwa?
www.baruayachahali.com
TopNewCommunity

No posts

Ready for more?

© 2022 Evarist Chahali
Privacy ∙ Terms ∙ Collection notice
Publish on Substack Get the app
Substack is the home for great writing