Barua Ya Chahali

Share this post
Siku 90 Za Mbowe Gerezani: Inasikitisha Mno Lakini Pia Inatafakarisha Sana.
www.baruayachahali.com

Siku 90 Za Mbowe Gerezani: Inasikitisha Mno Lakini Pia Inatafakarisha Sana.

Evarist Chahali
Oct 19, 2021
Share

Jana, Oktoba 19 ya mwaka huu, zimetimia siku 90 kamili tangu Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Mheshimiwa Freeman Mbowe, akamatwe na kufunguliwa mashtaka ya ugaidi na uhujumu uchumi. SIKU TISINI.

Inasikitisha sana. Kwa sababu moja kubwa. Haki hupaswa sio tu kutendeka bali pia ionekane imetendeka. Sasa katika kesi hii ya Mheshimiwa Mbowe, sio tu kwamba haki haijatendeka bali pia imekuwa ikisiginwa waziwazi. Bila haja ya kurejea kila uhuni uliofanywa dhidi ya Mheshimiwa Mbowe, viongozi kadhaa wa Chadema na wananchama wa chama hicho kwa ujumla, mwelekeo mzima wa kesi hiyo unaonyesha bila chenga jinsi chama tawala CCM kwa kutumia vyombo vya dola kinavyofanya siasa za upinzani kuwa mithili ya uhalifu.

Inasikitisha kwa sababu kama CCM kwa kutumia vyombo vyake vya dola inaweza kufanya haya kwa mtu mwenye hadhi kubwa kitaifa kama Mheshimiwa Mbowe, wewe kapuku mwenzangu upo katika hali gani?

Inasikitisha kwa sababu kama ilivyo kwa Mheshimiwa Mbowe, sie wengine ni wahanga wa udhalimu wa CCM, ambao mamia na pengine maelfu ya Watanzania wasio na hatia wananyanyaswa na kudhulumiwa haki zao huku wahalifu kama akina Bashite “wakitesa” huko mtaani. Inasikitisha na inauma pia. Na inakasirisha.

Hata hivyo, suala la Mheshimiwa Mbowe lina pande mbili. Watesi, yaani CCM na vyombo vyake kandamizi, na Mheshimiwa Mbowe, Chadema, na Upinzani kwa ujumla. Haihitaji kujadili uhuni wa CCM kwa sababu unahitaji vitabu lukuki.

Kwa upande wa wahanga wa uhuni wa CCM, bado kuna tatizo ambalo kwa bahati mbaya ni dhambi kulizungumzia. Unaweza kujiuliza, “hivi nini kimefanywa na viongozi na wanachama wa Chadema katika siku hizo 90 za Mheshimiwa Mbowe kuwa gerezani?”

Jibu fupi ni TwitterSpaces za wanaharakati wamtandaoni. Au Clubhouse za wanaharakati wa mtandaoni. Kwanini hili ni tatizo? Sababu ni nyingi lakini kuu za msingi ni kama ifuatavyo.

Hakuna sababu ya msingi kwanini chama kikubwa zaidi kwa upande wa upinzani -Chadema hiyo - kitegemee majukwaa ya watu wasiohusiana na chama hicho kufanya shughuli zake. Kwa sababu moja ya athari ya kutumia jukwaa la mtu mwingine ni tofauti katika malengo husika. Lengo la chama cha upinzani ni kushika dola, lengo la wanaharakati, well, ni kupigania masuala wanayoona yana vipaumbele kwao, lakini pia kuna fedha za wafadhili humo.

Sasa huhitaji kuwa na akili kubwa kubaini kuwa ushirikiano kati ya taasisi yenye dhamira ya kushika dola na kundi lenye maslahi binafsi ikiwa ni pamoja na ya kiuchumi, hauwezi kuzaa matokeo chanya.

Tmueshuhudia suala la Didier Abdallah Mlawa aka Kigogo, ambaye aliitumia Chadema kama jukwaa lake la kudhalilisha watu, sambamba na “kuvuta mpunga mrefu” akijifanya kupigani Katiba Mpya. Chadema walikuwa wanafahamu fika kuwa Kigogo sio tu ni jambazi aliyetoka kifungo cha miaka 15 jela kwa kosa la wizi bali pia yayumkinika kumtaja kama mdalilishaji mkubwa kuliko wote katika historia ya Tanzania, ambaye hakuwezi kuandika twiti mbili tatu bila kutukana matusi ya nguoni. How on earth, watu bora kama Chadema walijenga uswahiba na haramia huyo?

Kuna watakaosema “ah sasa Kigogo si ameshajiondoa, tatizo lipo wapi?” Tatizo ni kwamba waliomuwezesha Kigogo kufika alipofika leo bado ni maswahiba wakubwa wa Chadema, na ukilogwa kukitahadharisha chama hicho, unaishia kutukanwa.

Twitter avatar for @RealHauleGluckGoodluck 用心服務人類 @RealHauleGluck
Walipoanza kelele za #KatibaMpya kwa kutumia ‘Team Ubuyu’ na uvyama mbele tuliwaambia wasahau Katiba 2021-2025. Wakatukana wee mwisho wa siku mmoja wa ‘Team Ubuyu’ akajitegua mchana kweupee na kuwazodoa. Sasa Team Ubuyu mwingine anaendesha Spaces nao wapo tu. Taifa la Porojo 😁

October 18th 2021

6 Retweets29 Likes

Unaweza kujiuliza, kwanini wanaharakati waliokuwa bega kwa bega na Kigogo katika “uswahiba wao na Chadema,” leo hii wapo kimya kukemea hujuma kubwa zaidi zinazofanywa na jambazi huyo dhidi ya chama hicho? Kwake, Mheshimiwa Mbowe ni gaidi, na alijaribu kuwahadaa watu kuwa “kuna suahidi wa sauti na text ambao Tigo watawasilisha mahakamani.” Amekwenda mbali zaidi na kuwaita Chadema INTARAHAMWE, yaani kundi la kigaidi.

Ukweli mchungu ni kwamba sio tu kuwa wanaharakati hao na Kigogo bado ni damu damu, ila tu “wanakula kimkakati,” bali pia “wanatumika.”

Haya hayawezi kueleweka muda huu lakini amin nawaambia, kuna siku ndugu msomaji utarudi hapa na kusema “ah lakini Jasusi aliandika haya.” Muda utaongea.

Siku 90 za Mheshimiwa Mbowe gerezani zimetawaliwa na porojo mfululizo huko TwitterSpaces na Clubhouse. Hakuna ubaya kwa watu kujadili mustakabali wa chama chao lakini busara kidogo tu inapaswa kutumika na kutambua kuwa “hili ni suala letu binafsi.”

That aside, siku tisini za Mheshimiwa Mbowe gerezani zimesaidia tu kuonyesha jinsi gani uovu unavyoweza kushamiri pasi kuchelea matokeo. Mie si muumini wa vurugu, na kamwe siwezi kuhamasisha vurugu. Hata hivyo, hatua stahili dhidi ya uonevu sio lazima zihusishe vurugu. Kinachohitajika ni vitendo zaidi kuliko porojo. Ukandamizwaji hauwezi kukabiliwa kwa kujazana upepo TwitterSpaces/ClubHouse na watu ambao hata siku moja hawajatokea mahakamani kumpa sapoti Mheshimiwa Mbowe.

Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Inasikitisha. Lakini pia inatafakarisha. Kwamba kiongozi mkuu wa chama kikubwa zaidi cha upinzani anaweza kuwekwa ndani kwa uonevu kwa SIKU 90. Think that again. Kama serikali inaweza kufanya hivi kwa Mbowe, how about you? On other hand, seriously reaction pekee ni TwitterSpaces?
Image

October 18th 2021

14 Retweets123 Likes
Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Mkoloni hakuondoka kwa vile watu walilalamika kuhusu udhalimu wake. Nduli Iddi Amin pia hakukimbia kwa vile watu walichukizwa na unyama wake. Na makaburu hawakuacha mfumo wao kwa vile tu Mandela hakukata tamaa. It took ACTIONS kuleta mabadiliko kusudiwa. Hope is not a strategy.

Gerry Mshana @mshana_gerry

@Chahali Nikiri kuwa sijui mikakati yao, kwa kuwa si mndani wa chama wala mwana mikakati. Ila kama historia ni mwalimu, na nadhani ni hivyo, kama mikakati ni kitu kilicho wazi kwa umma wote kuona na kutambua, basi hiyo si mikakati tena. SA baada ya kumfunga Mandela walidhani wameiua ANC

October 18th 2021

1 Retweet3 Likes
Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Suala sio kupitia mateso bali kuwa na mikakati thabiti ya kukomesha mateso hayo. Kinachojiri sasa sio kipya, kilianza 1992 mara baada ya kuruhusiwa vyama vingi. Hebu tuelimishe, nini kimefanyika muda wote huo kukomesha mateso yaliyodumu miaka 29 sasa?

Gerry Mshana @mshana_gerry

@Hunmass @Chahali @Hunmass hii narrative yako haioani na historia ya mapambano ya vyama vya siasa duniani, Afrika, Asia, Ulaya Mashariki, Amerika Kusini. Vyama ambavyo viongozi wao wamepitia mateso, vilibadili mbinu na hatimaye kuwa na nguvu zaidi. Sioni tofauti kubwa sana na kinachoendelea sasa.

October 18th 2021

1 Retweet10 Likes
Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
What needs to be done? Couple of suggestions. One is ushirikishwaji wa umma katika mkakati thabiti dhidi ya uonevu. Hili sio suala la Chadema au Mbowe pekee. Ni la kila Mtanzania. However si kila Mtanzania ni mwanasiasa. So rai kwenu wanasiasa kutushirikisha tusio wanasiasa.

Jasusi @Chahali

Inasikitisha. Lakini pia inatafakarisha. Kwamba kiongozi mkuu wa chama kikubwa zaidi cha upinzani anaweza kuwekwa ndani kwa uonevu kwa SIKU 90. Think that again. Kama serikali inaweza kufanya hivi kwa Mbowe, how about you? On other hand, seriously reaction pekee ni TwitterSpaces? https://t.co/helhmdup39

October 18th 2021

14 Likes
Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Kesi hii ina athari kadhaa, lakini nitaje kubwa mbili. Ya kwanza ni kuwapa imani watesi kuwa no matter what they do vs wasio na hatia, hawapaswi kuchelea matokeo...because there's none whatsoever. Pili, ongezeko la political apathy, yaani watu kupoteza matumaini kwa siasa.

Jasusi @Chahali

Inasikitisha. Lakini pia inatafakarisha. Kwamba kiongozi mkuu wa chama kikubwa zaidi cha upinzani anaweza kuwekwa ndani kwa uonevu kwa SIKU 90. Think that again. Kama serikali inaweza kufanya hivi kwa Mbowe, how about you? On other hand, seriously reaction pekee ni TwitterSpaces? https://t.co/helhmdup39

October 18th 2021

1 Retweet11 Likes
Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
The hopelessness lies in the fact that Chairman @freemanmbowetz's fate lies in the hands of same thugs who put him in the ordeal in first place. The proverbial "kesi ya nyani hakimu ngedere." I'm not inciting violence but surely kulalamika spesiz is not strategy. Unfortunately!

Jasusi @Chahali

Inasikitisha. Lakini pia inatafakarisha. Kwamba kiongozi mkuu wa chama kikubwa zaidi cha upinzani anaweza kuwekwa ndani kwa uonevu kwa SIKU 90. Think that again. Kama serikali inaweza kufanya hivi kwa Mbowe, how about you? On other hand, seriously reaction pekee ni TwitterSpaces? https://t.co/helhmdup39

October 18th 2021

7 Likes

Yayumkinika kuhitimisha kuwa siku 90 za Mheshimiwa Mbowe gerezani zimeambatana na jabali huyo wa siasa za upinzani KUANGUSHWA na watu waliopaswa kuweka kando porojo TwitterSpaces/Clubhouse, na kukabiliana na ukandamizwaji wa haki za kisheria na kiraia.

Sitaki kubashiri kitakajiri kwenye hukumu ya Mheshimiwa Mbowe hapo kesho japo ni muhimu kujiandaa kisaikolojia. I just hope hukumu ya Sabaya iliyofurahiwa na wengi haitotumika kupindisha haki dhidi ya Mheshimiwa Mbowe. I could only hope for the best.

Mwisho, unakaribishwa kujiunga na kozi hizi za bure

Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Masomo mapya kwa mliojisajili. Kama hujajisajili, fanya hivyo hapa
adelphil.official.academy. Kozi zote ni bure buleshi 🙏

October 18th 2021

4 Likes

Good day👍

ShareShare
TopNewCommunity

No posts

Ready for more?

© 2022 Evarist Chahali
Privacy ∙ Terms ∙ Collection notice
Publish on Substack Get the app
Substack is the home for great writing