Barua Ya Chahali

Share this post
Siasa Za Makundi CCM: Kiongozi Mmoja wa Dini Na Mikakati Yake Dhidi ya Mama Samia
www.baruayachahali.com

Siasa Za Makundi CCM: Kiongozi Mmoja wa Dini Na Mikakati Yake Dhidi ya Mama Samia

Evarist Chahali
Dec 22, 2021
1
Share this post
Siasa Za Makundi CCM: Kiongozi Mmoja wa Dini Na Mikakati Yake Dhidi ya Mama Samia
www.baruayachahali.com

Taarifa za ndani ya chama tawala CCM zinaeleza kwamba kiongozi mmoja wa dini ambaye pia ana nafasi ya uongozi katika chama hicho yupo kwenye jitihada kubwa za kutanua upinzani dhidi ya Mama Samia.

Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
#Tanzania: an influential pentecostal cleric-cum-ruling party @ccm_tanzania politician is persuing "multi-track strategies" to (a) derail @SuluhuSamia's presidency (b) if that fails, bring her down in 2025 election. A bloodless religio-political civil war never seen before
Tanzania GIF

December 20th 2021

7 Likes

Tafsiri ya twiti hiyo kwa Kiswahili ni kwamba kiongozi mmoja maarufu wa kidini ambaye pia ana wadhifa huko CCM ana mikakati kadhaa ya (a) kukwamisha urais wa Mama Samia (b) endapo hilo litafeli, basi kumzuwia Mama Samia katika uchaguzi mkuu ujao mwaka 2025.

Barua Ya Chahali haitomtaja kiongozi huyo wa kidini na kisiasa kwa sasa.

Kwa mujibu wa taarifa, kiongozi huyo “anatumika” na yeye pia ana “anaowatumia.” Katika kutumika, yeye kwa sasa ndio “sura ya hadharani” (public face) ya genge la kisiasa linalofahamika kama “Chato Gang.” Genge hili linaundwa na wanufaika wa utawala wa marehemu John Magufuli, na linapigana kufa na kupona kuhakikisha kuwa himaya iliyoanza kujengwa Kanda ya Ziwa inarudi kushika hatamu za uongozi.

Lakini pengine CCM isingefika hapa endapo ingezingatia tahadhari ambazo baadhi yetu tumekuwa tukitoa kitambo

Barua Ya Chahali
Makala Ya Wazi: Kuchanganya Dini Na Siasa Kutaligharimu Taifa
Read more
3 years ago · 3 likes · Evarist Chahali
Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Hili la "kuruhusu DINI kwenye SIASA" halina mwisho mzuri. Ni kama kumlea chatu. Usipomlisha vizuri, njaa ikimkamata, atakugeuza mlo wake. Ukimlisha vizuri, atanawiri, na kupata nguvu za kukumeza kirahisi. Naomba twiti hii ibaki kama kumbukumbu kwa vizazi vijavyo... #MarkThisTweet
Image

August 19th 2020

7 Retweets31 Likes
Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Askofu @jgwajima anakemea @usembassytz kuongelea suala la @freemanmbowetz kuvamiwa, lakini hajikemei yeye kama mtumishi wa Mungu kuvamia siasa. Kipi cha hatari zaidi kati ya tamko la ubalozi wa Marekani na viongozi wa dini kujigeuza wanasiasa? Dini + siasa = 💣
Image

July 5th 2020

1 Retweet16 Likes
Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Dini na siasa

Tanzania Updates @TanzaniaUpdates

PICHA: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na waumini wengine wa Kanisa Katoliki la Mtakatifu Petro Parokia ya Oysterbay leo ameshiriki Ibada ya Jumapili ya Familia Takatifu katika Kanisa hilo la jijini Dar es Salaam. https://t.co/13sUpmGjZp

December 31st 2017

5 Likes

Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Kwanini dini + siasa = 💣? Both zinagusa imani na hisia za watu. Unfortunately, both imani na hisia zina kasumba ya kuwa mbele ya busara, Waingereza wanasema "emotions in front of common sense." Na kibaya zaidi, both are monolithic in character ie changu ndo cha kweli, not chako

Jasusi @Chahali

Askofu @jgwajima anakemea @usembassytz kuongelea suala la @freemanmbowetz kuvamiwa, lakini hajikemei yeye kama mtumishi wa Mungu kuvamia siasa. Kipi cha hatari zaidi kati ya tamko la ubalozi wa Marekani na viongozi wa dini kujigeuza wanasiasa? Dini + siasa = 💣 https://t.co/vZ1VqsLmJB

July 5th 2020

1 Retweet11 Likes
Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Mwezi wa Ramadhan ni kielelezo kizuri cha umoja na upendo miongoni mwa Watanzania bila regardless of dini zetu. Tusiruhusu siasa ibomoe hilo

July 9th 2013

6 Retweets1 Like
Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Tutasubiri wahuni waingize dini kwenye siasa na siasa kwenye dini hadi pale kibanda chetu kianze kuungua, ndo tukurupuke na "marufuku"

March 5th 2017

18 Retweets29 Likes
Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Halafu utawaskia wakisema "msichanganye dini na siasa..." #Hovyooo
Image

April 9th 2014

2 Retweets
Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Kardinali Pengo akijipendekeza kwa JPM sio kuchanganya dini na siasa. Kakobe akimkosoa JPM ndio dini na siasa? Hamna maana ninyi

Tanzania Updates @TanzaniaUpdates

"Hivi karibuni kumekuwepo na tabia ya baadhi ya viongozi wa jumuiya kutumia mahubiri yao wakati wa ibada kuchambua masuala ya siasa kinyume na Katiba zao. Hakuna jumuiya iliyosajiliwa chini ya sheria ya jumuiya ili kufanya siasa" ~ K/Mkuu Mambo ya Ndani Meja Jenerali Rwegasira https://t.co/IVr0T6ikFo

December 28th 2017

6 Retweets24 Likes
Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
#Tanzania: Ni marufuku kuchanganya dini na siasa... au ni marufuku kuchanganya dini na chama kingine cha siasa isipokuwa @ccm_tanzania?
Image

February 4th 2018

13 Retweets113 Likes
Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
"Tuepuke kuchanganya dini na siasa...." Ah wapi, nani kasema hivyo? [Read between the lines, tafadhali]
Image

August 23rd 2016

4 Retweets5 Likes
Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
2/2 Kuchanganya dini na siasa: kwa minajili ya kumbukumbu

November 18th 2019

1 Retweet14 Likes
Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Kama ambavyo ni hatari mno kuchanganya dini na siasa, ndivyo ambavyo tunapaswa kulaani kwa nguvu wakuu wa vyombo vya dola kuingilia siasa
Image

September 14th 2017

23 Retweets121 Likes

Kama twiti hizo zinavyoonyesha, ni dhahiri CCM na serikali zake haiwezi kuja siku moja kulalamikia suala la kuchanganya dini na siasa kwa sababu yenyewe imekuwa ikiongoza jitihada za kutumia dini katika kufanya siasa zake.

Kimsingi, hata hivyo, ni muhimu kutambua kuwa both siasa na dini ni vitu vizuri vikitumika ipasavyo. Dini, kwa tafsiri nyepesi, ni mahusiano binafsi kati ya binadamu na mola wake (whatever that means to them). Na siasa, katika moja ya tafsiri zake nyingi, ni mahusiano kati ya mtu na dola. Kwahiyo, both dini na siasa vinamhusu mtu.

Hakuna tatizo kwa viongozi wa dini kuwakumbusha waumini wao kuhusu wajibu wao kama waumini. Na miongoni mwa waumini hao ni viongozi wa kisiasa. Kwahiyo, dini ikitumika vizuri, inaweza kutoa malezi mazuri kwa viongozi kisiasa ambao ni waumini wa dini husika. Unfortunately, kwa Tanzania yetu, it never works that way. Mara nyingi inakuwa kinyume chake, yaani viongozi wa kisiasa ndio wanaotoa mwongozo kwa viongozi wa dini.

Kibaya zaidi, miongozo hiyo hujikita kwenye maslahi binafsi ya viongozi hao wa kisiasa.

Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Another #ChaguoLaMungu or Shetani amefanikiwa?
Image

July 29th 2015

1 Retweet1 Like
Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
.@jmkikwete Si #Magufuli wala #Lowassa ambao ni CHAGUO LA MUNGU. Mungu hakushiriki ktk vikao vya kuwapitisha. Tusimzushie wala kumchokoza.

August 20th 2015

14 Retweets9 Likes
Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
"Padre ampigia kampeni Magufuli" -
jamiiforums.com/showthread.php… Yaleyale ya 2005 #ChaguoLaMunguMapadre waanza rasmi kumpigia Magufuli kampeniKatika kile kinachoonyesha viongozi wa dini kuingilia mambo ya siasa, padre Mbano akihubiri ktk Ibada ya leo j2 kwenye Kanisa kuu Katoliki Songea Mjini amesema ujio wa Magufuli ndio jembe haswa lililokuwa linasubiriwa. Akaendelea kusema kuwa anawaomba radhi wapinzani safari hii waachane na...jamiiforums.com

July 19th 2015

1 Like

Na ndivyo ilivyotawala katika zama za marehemu Magufuli.

Viongozi wa kidini walikuwa na nafasi ya kipekee kwenye utawala wake, ambapo walipita huku na kule, baadhi yao wakikufuru na kudai “Magufuli ni chaguo la Mungu.”

Lakini pengine jambo la kukera zaidi na lililopaswa kukemewa mapema ni kitendo cha Magufuli kugeuza makanisa kuwa majukwaa ya kisiasa. Takriban kila Jumapili aligeuka mhubiri wa siasa makanisani.

Siku moja tunaweza kufahamu ni kwa jinsi gani kampeni za Magufuli dhidi ya ugonjwa wa korona zilivyochangia vifo vya maelfu ya Watanzania. Viongozi wa dini waliompa mwanasiasa huyo jukwaa la kuhubiri porojo zake nao wana damu mikononi mwao ya wenzetu waliokufa kwa korona kwa kuamini porojo hizo.

Uhusiano baina ya Magufuli na viongozi wa dini ulikuwa katika namna kwenye Baiolojia wanaita “symbiotic,” yaani uhusiano wa kutegemeana. Kwa upande mmoja, viongozi wa dini waliomnyenyekea Magufuli walipewa sapoti ya kifedha na upendeleo kwenye maeneo kama ya ulipaji kodi. Nao kwa upande wao, walimnufaisha Magufuli kwa kumtukuza kama “mungu-mtu” sambamba na kutumia nyumba zao za ibada kama majukwaa ya kisiasa kwa kiongozi huyo na chama chake.

Turudi kwa kiongozi huyo wa dini ambaye pia ni kiongozi wa CCM. Kama ilivyoelezwa awali, amekuwa akitumika kama “public face” ya Chato Gang. Unaweza kujiuliza, “anapata ujasiri huo? Je hahofii kufukuzwa huko CCM?”

Kwa upande mmoja, ujasiri wa kiongozi huyo unatokana na nguvu zilizo nyuma yake. Katika utumishi wake kwa taifa, hasa akiwa Waziri wa Ujenzi, Magufuli “alivuta” watu wengi wanaohusiana nae, mostly wa kabila lake. Na moja ya Wizara zenye “ulaji wa nguvu” ni Ujenzi. Kwahiyo, watu hao waliovutwa na Magufuli wachuma fedha nyingi katika nafasi zao. Kwa mfano, waziri mmoja mwandamizi enzi za Magufuli, alikabidhiwa jukumu la kununua “bombadia” za ATCL kwa fedha taslimu. Huyu jamaa alitengeneza mamilioni ya dola kama kamisheni kwenye ununuzi wa ndege hizo.

Na nguvu walizonazo Chato Gang ni moja ya sababu kuu ya kuhangaika kumhujumu Mama Samia kwani bila kuwa na mtu wa kuwalinda kama Magufuli, hawana amani na utajiri mkubwa waliochuma kupitia uswahiba wao na kiongozi huyo aliyefariki Machi mwaka huu.

Lakini pia utawala wa Magufuli ulipaswa kudumu milele. Tayari maandalizi yalikuwa yameanza kubadili katiba ili atawale milele. Na hili sio jambo lililotokea kwa bahati mbaya. Hapana. Ulikuwa mkakati uliopangwa muda mrefu ukishirikisha watu mbalimbali katika kada mbalimbali nchini Tanzania.

Hii ilikuwa himaya. Na Chato Gang wanahangaika kuirejesha himaya hiyo ambayo bila uwepo wa Magufuli, inaelekea kuanguka.

Kwa upande mwingine, anachofanya kiongozi huyo wa kidini na kisiasa ni dalili tu za tatizo lililodumu miaka kadhaa nchini Tanzania: UDINI. Makala hii haitoshi kueleza kwa kirefu kuhusu tatizo hilo lakini kwa kifupi, kila mara Tanzania inapokuwa chini ya rais Muislam, huwa kunaibuka “chokochoko” za kidini.

Utawala wa Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi ulikabiliwa na changamoto kubwa ya udini iliyotishia kusambaratisha amani na mshikamano wa Watanzania. Alipokuja Rais mstaafu marehemu Benjamin Mkapa, “chokochoko” hizo zilitulia, kabla ya kuibuka tena wakati wa utawala wa Rais mstaafu Jakaya Kikwete. Lakini Magufuli alipoingia madarakani, “chokochoko” hizo zilitulia tena.

Hata hivyo, ujio wa Mama Samia umeziibua tena “chokochoko” hizo. Na kwa kiasi kikubwa tu, vita ya Chato Gang dhidi ya Mama Samia ina chembechembe za udini pia.

“Adui” mwingine wa Mama Samia ni “uzanzibari” wake. Kama ilivyokuwa wakati wa utawala wa Rais mstaafu Mwinyi, kuliibuka harakati kubwa dhidi ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar uliozaa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania. Ni kipindi hicho ambako kuliibuka kundi maarufu la G-55 la wabunge wa Tanzania Bara waliotaka mabadiliko kwenye muundo wa muungano.

Kadhalika, ukweli kwamba Mama Samia ni mwanamke unawanyima baadhi ya wanasiasa waumini wa “mfumo dume” ambao hadi muda huu hawaamini kuwa nchi ipo chini ya Rais mwanamke.

Taarifa kuhusu kiongozi huyo wa dini na siasa zinaeleza kuwa kwa upande mmoja yeye na kundi lake wamefanikiwa kukiweka mkononi chama kimoja cha upinzani ambacho “kiliahidiwa na Magufuli kuwa kingepewa viti vya ubunge kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2020, na kukiwezesha kuwa chama kikuu cha upinzani.”

Vilevile, kundi hilo limefanikiwa kuwanasa baadhi ya viongozi wa chama kingine cha upinzani. Haikuwa nguvu kwa kundi hilo kufanikisha azma yao kutokana na “chuki iliyopo kati ya chama hicho na Mama Samia.”

Inaelezwa pia kuwa kundi hilo limejiweka karibu na wanaharakati walio karibu na chama hicho kwa minajili ya kutimiza ajenda hiyo.

Kesi dhidi ya Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Mheshimiwa Freeman Mbowe, imekuwa mtaji muhimu kwa kundi hilo, ambalo linaona kesi hiyo kama fursa adimu ya kuthibitisha kuwa “Mama Samia ni dikteta.” Kundi hilo linaamini kuwa kuna fursa ya kusambaza chuki zaidi dhidi ya kiongozi huyo.

Mwisho, kuna taarifa kuwa Idara ya Usalama wa taifa nayo imekuwa sehemu muhimu katika hujuma hizo, na inadaiwa kuwa “Mama Samia alihudhuria vikao vya CCM huko Dodoma hivi majuzi kwa kulazimisha, kinyume na ushauri wa Idara hiyo iliyomshauri asihudhurie.”

Katika hili, Mama Samia hana wa kumlaumu zaidi ya yeye mwenyewe kwani anaendelea kuwa “Rais wa ajabu” kurithi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa. Utamaduni usio rasmi katika nchi nyingi duniani ni kwa Rais mpya kuteua mkuu mpya wa Idara ya Usalama wa Taifa, kwa sababu huyo ndiye haswa “ameshikilia urais wa rais husika.”

Jumatano njema.

Sapoti Barua Ya Chahali

Share this post
Siasa Za Makundi CCM: Kiongozi Mmoja wa Dini Na Mikakati Yake Dhidi ya Mama Samia
www.baruayachahali.com
TopNewCommunity

No posts

Ready for more?

© 2022 Evarist Chahali
Privacy ∙ Terms ∙ Collection notice
Publish on Substack Get the app
Substack is the home for great writing