Safu ya #MAISHA [Episode 14]: Mfahamu Balozi Togolani Mavura (@tonytogolani), mwanadiplomasia mahiri, mwanabusara nguli kupitia nukuu za '@SikilizaTogolani', na kiongozi mwenye utu kwelikweli
Endapo ni mara yako ya kwanza kukutana na Balozi Togolani Edriss Mavura, inaweza kukuwia vigumu kuamini kuwa sio tu kwamba yeye ni mwakilishi wa Tanzania nchini Korea na Kusini bali pia ni mtumishi mzoefu wa umma ambaye pamoja na nyadhifa muhimu mbalimbali alizoshika ni pamoja na kuwa msaidizi wa Rais.