Safu ya #MAISHA [Episode 11]: Mfahamu Mhe Nape Nnauye (@Nnauye_Nape) mbobezi wa siasa za Tanzania aliyerithi kipaji cha uongozi kutoka kwa baba yake, Brig Jen Moses Nnauye, mmoja wa wapigania uhuru
Licha ya kushiriki harakati za kupigania uhuru, Brig Jen Nnauye alikuwa mmoja wa makamanda walioongoza Vita ya Kagera kama mwanajeshi huku akiwa Naibu Waziri wa Ulinzi pia.
Yayumkinika kuamini kuwa hakuna Mtanzania ambaye hajawahi kusikia jina la Mheshimiwa Nape Nnauye, mwasiasa ambaye sio tu ana historia ndefu ya uongozi ndani ya chama tawala CCM na utumishi wa umma, bali pia ni mmoja wa wanasiasa wabobezi na ambaye amekuwa na mchango mkubwa kwa ushindi wa wagombea urais kupitia tiketi ya CCM.