Rai kwenu Chadema na ACT-Wazalendo: kama "mnavyowapigania Watanzania kuhusu Katiba mpya" mnapaswa pia kuwapigania kukomesha mgao wa maji, umeme
Jasusi anaomba kuwa mkweli, kwamba japo anatambua mapungufu lukuki yaliyomo kwenye Katiba iliyopo na haja ya mabadiliko ya katiba hiyo, bado anaamini kwamba katiba mpya pasipo mabadiliko katika “psyche” ya Watanzania ni kazi bure.
Jasusi hana tafsiri sahihi ya neno pysche lakini kwa lugha nyepesi, ni “namna watu wanavyofikiri, wanavyotazama mambo, vipaum…