'Nabii' wa Zimbabwe, Aliyetabiri 'Hujuma Dhidi ya JPM', Afanya 'Utabiri' Mwingine Kuhusu Mustakabali wa Mama Samia. Uchambuzi: Ni Maono Kweli au Uzushi tu?
Mdau mmoja aliyepo nchini Kenya alinitwiti jana kuhusu video yenye “unashiri kuhusu Mama Samia Suluhu.” Nilipobonyeza link ya video husika, nikamtambua mhusika kwenye video hiyo kuwa ni “nabii” maarufu wa Zimbabwe ambaye nilimkumbuka kutokana na “maono” yake mwaka 2019 na 2020 kuhusu mustakabali wa Rais Magufuli.