Barua Ya Chahali

Share this post
[#TumiaVPN Endapo Link Haifunguki]Mzaha wa Magufuli Kwenye Korona: Yajayo Yanatafakarisha.
www.baruayachahali.com

[#TumiaVPN Endapo Link Haifunguki]Mzaha wa Magufuli Kwenye Korona: Yajayo Yanatafakarisha.

Evarist Chahali
Jul 10, 2020
Share this post
[#TumiaVPN Endapo Link Haifunguki]Mzaha wa Magufuli Kwenye Korona: Yajayo Yanatafakarisha.
www.baruayachahali.com
GADO - Coronavirus and Events in Tanzania | The Elephant

Mtu mmoja alinitwiti majuzi akidai “siaminiki” kwa sababu “nilibashiri korona itamwondoa Magufuli” lakini kwa mujibu ya mtu huyo “si kweli.”

Mtu huyu alikuwa anaongelea ubashiri niliofanya kwenye “Uchambuzi wa Kiintelijensia Kuhusu Mustakabali wa Urais wa Magufuli Kutokana na Jinsi Alivyoshughulikia Janga la Korona.”

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Kitu mwafaka kusoma wikiendi hii 👉 "Uchambuzi wa Kiintelijensia (Kwa Kutumia Mbinu Mbalimbali Za Uchambuzi wa Kiintelijensia) Kuhusu Mustakabali wa Magufuli Kutokana na Anavyoshughulikia Janga la Korona"
docdro.id/2chH08B
Image

May 23rd 2020

10 Likes

Bado ninasimamia nilichokiandika katika uchambuzi huo wa kiintelijensia. Na sio kama ninakisimamia kwa vile tu nilikiandika mwenyewe au kwa kuchelea “kuiweka matatani heshima yangu kwenye jamii (kama ipo😊) bali kwa sababu uchambuzi huo haukutamka mahala popote kuwa urais wa Magufuli ungeisha siku au wiki kadhaa baada ya kuuchapisha.

Na licha ya kutahadharisha kuwa “intelijensia sio sayansi timilifu (intelligence is not exact science)” baadhi ya factors zilitegemea kutokea kwa factors nyingine. Kwa mfano, ubashiri kuwa baadhi ya “wapambe wa Magufuli” wangemgeuka ENDAPO idadi ya vifo kutokana na korona ingezidi kuongezeka, haujawa hivyo si kwa sababu idadi ya vifo vya korona haikuwa kubwa bali Magufuli amefanikiwa - angalau hadi muda huu - kuficha ukweli kuhusu janga hilo, kama alivyofanikiwa kuficha ukweli kuhusu idadi ya waliouawa na “kikosikazi” huko MKIRU (Mkuranga, Kibiti na Rufiji.

Na katika hilo la MKIRU, ninajisikia faraja kuwa Mtanzania pekee aliyejaribu kulitafutia ufumbuzi kwenye taasisi za kimataifa, kwa kuanzisha petition mtandaoni na “kupotea” kwa mwanahabari Azory Gwanda aliyekuwa akifuatilia suala hilo

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Video: These are documents I have enclosed with my #MKIRU and #AzoryGwanda petition to the UN Human Rights Commissioner | Hizi ndio nyaraka nilizoambatanisha kwenye #PetitionYaMKIRU na #AzoryGwanda niliyotumia leo kwa Kamishna wa Haki za Binadamu huko Umoja wa Mataifa
Image

July 9th 2018

3 Retweets33 Likes

Na japo nilikumbana na kikwazo, ukweli unabaki kuwa sio tu nilijaribu bali historia itanikumbuka kama Mtanzania pekee kufanya jitihada hiyo kimataifa.

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Eid Mubarak. Naomba kutumia fursa hii kutoa mrejesho kuhusu #PetitionYaMKIRU (kwa mnaokumbuka). Kwa kifupi, nimekumbana na kikwazo kidogo. Kwa bahati mbaya au makusudi, Tanzania haijasaini mkataba wa kimataifa ambao suala la watu "waliopotea" huko MKIRU …
ift.tt/2LgN7Nx
Image

August 22nd 2018

4 Likes

Turejee kwa Magufuli. Japo amefanikiwa katika hilo la kuficha idadi ya vifo vya korona, si kwa sababu yupo smati kwenye kuficha taarifa bali tuna Wapinzani “wanaoshikilia bango yale tu wanayoona yana umuhimu kwao kisiasa,” sambamba na Watanzania wanaodanganyika kirahisi kama ilivyokuwa kwenye ishu za Babu Ambi

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
#Flashback: Kabla ya Pierre na Dokta Shika kulikuwa na Babu Ambi. Aliyewaroga Watanzania nae karogwa, kapata kichaa, kagongwa na basi la Skandinavia, kafariki. Hamponi 😊

Evarist Chahali @Chahali

"Babu Ambi ateuliwa kuwa Mkemia Mkuu" #FutureTweet http://t.co/fkiNmy1WjF

April 7th 2019

1 Retweet24 Likes

Au ‘Dakta’ Shika

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Nitendee haki Ndugu Chambua. Hivi kweli kabisa wataka nikae chini kuandika kuhusu porojo za 'Dokta' Shika? Kitu pekee nachoweza kuandika ni hiki: ni rahisi mno kuwaghilibu Watanzania. Orodha ni ndefu Desi. Babu Ambi. Dkt Shika. Aliyewaroga Watz kafa kwa korona. Hakuna kupona

raymond chambua @rchambua

@Chahali @Chahali kiongozi Vipi!?..Ishu ya Dr.Shika iko je kiupelelezi!?..stahiki zake!!..Maana inaonekana Marekani walimtumia Urusi mpk akapoteza Mali zake,na wakafanikiwa kumtorosha kumleta Tanzania,na wakamtelekeza na kumuacha fukara!!.Tupe Uzi kama Mbobezi kwenye Mambo hayo..🙏

July 8th 2020

13 Likes

Ndio ukweli huo. Ni rahisi kuwalaumu wanasiasa wa Upinzani kwa kutoMbana Magufuli ipasavyo kwenye ishu kama ya MKIRU au hiyo ya Korona lakini ni muhumi kukumbuka kuwa wanasiasa hao -kama wale wa CCM - ni kielelezo cha jinsi Watanzania walivyo. Kasoro zilizopo kwenye familia, kabila, ukoo baadaye huishia kuwa kasoro KITAIFA.

Nirejee kwenye uchambuzi wangu wa kiintelijensia kuhusu mustakabali wa urais wa Magufuli. Nilitanabaisha kuwa anguko lake linaweza kutokana na factors za KIUCHUMI, ndani na nje. Bila haja ya kurudia nilichaondika, uchumi wa nchi hutegemea both soko la ndani na la nje. Na masoko hayo mawili yanahusiana kwa karibu.

Moja ya mifano hai ni huu

Twitter avatar for @bbcswahiliBBC News Swahili @bbcswahili
Je Covid19 imeathiri vipi wakulima Tanzania? Wakulima wa ufuta Kusini mwa Tanzania sasa wanalazimika kuuza kilo moja ya ufuta kwa kama dola senti 56 tu - takribani nusu ya bei waliyouza ufuta msimu uliopita. Sammy Awami alizuru Lindi, Kusini mwa Tanzania. #Tanzania #ukulima
Image

July 9th 2020

9 Retweets86 Likes

Na kwenye soko la kimataifa, inaweza kuwa vigumu kwa mnunuzi anayetaka kununua bidhaa kutoka Tanzania kufanya hivyo baada ya kukutana na takwimu zisizopendeza kama hizi

Na licha ya athari za korona kwa utalii kwa takriban kila nchi, kwa Tanzania athari hizo zachangiwa na hiyo hatua ya Magufuli kuficha takwimu za korona

Naomba ieleweke kuwa kubashiri kuwa mustakabali wa urais wa Magufuli ni tete - na hata KUTAMANI aondoke madarakani - haimaanishi kuichukia Tanzania. Tofauti na mzaha wa MATAGA wa kumfanya “Magufuli ndio Tanzania,” au “hakuna Tanzania bila Magufuli,” ukweli ni kwamba Tanzania ilikuwepo, ipo na itaendelea kuwepo hata kama Magufuli asingekuwepo. Uhuru ulitafutwa na akina Nyerere, si Magufuli. Na hata huko kuifikisha Tanzania kwenye uchumi wa kati, ni jitihada za Watanzania kwa ujumla na si za mtu mmoja.

Nihitimishe makala hii kwa taarifa kuhusu jarida jipya la UJASUSI.

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Jarida la Ujasusi - la kwanza duniani kwa machapisho ya mtandaoni kwa lugha ya Kiswahili kuhusu intelijensia hususan ujasusi na usalama wa mtandaoni hususan udukuzi. Linatoka kila wiki. Habarika na elimika kuhusu UJASUSI na UDUKUZI hapa
ujasusi.com
Image

July 8th 2020

2 Retweets9 Likes

Ndimi mtumishi wako,

Evarist Chahali

Share
Share this post
[#TumiaVPN Endapo Link Haifunguki]Mzaha wa Magufuli Kwenye Korona: Yajayo Yanatafakarisha.
www.baruayachahali.com
TopNewCommunity

No posts

Ready for more?

© 2022 Evarist Chahali
Privacy ∙ Terms ∙ Collection notice
Publish on Substack Get the app
Substack is the home for great writing