Barua Ya Chahali

Share this post
Mtume Aliyesababisha Vifo 20 Hakukamatwa. Kwanini Serikali ya Magufuli Inawaongopea Kuwa Alikamatwa Na Sasa Kapewa Dhamana?
www.baruayachahali.com

Mtume Aliyesababisha Vifo 20 Hakukamatwa. Kwanini Serikali ya Magufuli Inawaongopea Kuwa Alikamatwa Na Sasa Kapewa Dhamana?

Nchi Inaendeshwa Kama Kampuni ya Genge la Kihalifu

Evarist Chahali
Feb 6, 2020
1
Share this post
Mtume Aliyesababisha Vifo 20 Hakukamatwa. Kwanini Serikali ya Magufuli Inawaongopea Kuwa Alikamatwa Na Sasa Kapewa Dhamana?
www.baruayachahali.com

Tangu mwanzo wa tukio la vifo 20 (bado naambiwa kuwa idadi ya waliofariki ni kubwa zaidi) hisia yangu ya sita ilikuwa inaniambia “hapo kuna namna.”

Kwenye ushushushu inasisitizwa kutoamini COINCIDENCE (matukio mawili au zaidi yanayotokea kwa wakati mmoja au mfululizo). Ukweli kwamba tukio la vifo hivyo huko Moshi lilijiri masaa machache tu baada ya Marekani kutangaza kuwa imempiga marufuku Bashite kukanyaga nchi hiyo, ulinifanya “nichezwe na machale.”

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Narudia tena: kwenye ushushushu hakuna COINCIDENCE.
Image

February 2nd 2020

9 Retweets32 Likes
Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Kwenye ushushushu hakuna COINCIDENCE. Yaani matukio mawili au zaidi yakitokea kwa wakati mmoja, shushushu (sio #MATAGA) anapaswa kuchezwa na machale. Kuna hisia inanisumbua, naomba niiweke wazi: I suspect kuna uhusiano kati ya ishu ya Bashite na hivyo vifo vya waumini 20 Arusha
Image
Image
Image
Image

February 2nd 2020

3 Retweets33 Likes
Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Kindly read between the lines.
Image
Image

February 4th 2020

10 Likes

Anyway, kwa kifupi, taarifa kwamba “Mtume” aliyehusika na vifo ameachiwa kwa dhamana ni za UONGO.

Twitter avatar for @MwananchiNewsMwananchi Newspapers @MwananchiNews
Jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro limewaachia kwa dhamana watu wanane akiwemo Mtume na Nabii, Boniface Mwamposa wanaotuhumiwa kuendesha kongamano lililosababisha vifo vya watu 20 mjini Moshi. Msemaji wa Polisi, David Misime amethibitisha #MwananchiUpdates
Image

February 4th 2020

39 Retweets342 Likes

Ni uongo kwa sababu mtu hawezi kuachiwa kwa dhamana kama hakukamatwa in the first place. Naam, “Mtume” aliyesababisha vifo hivyo 20 sio tu hakukamatwa lakini bali pia amri ya kutomkamata ilikuwa “maagizo kutoka ngazi za juu.” Na ndio maana hakuna picha ah video inayomuonyesha “Mtume” huyo akiwa mikononi mwa polisi.

Lakini hata tukiweka kando suala la picha, taarifa ya Waziri Simbachawene kuwa polisi walikuwa wamemkamata “Mtume”

Twitter avatar for @MwananchiNewsMwananchi Newspapers @MwananchiNews
Waziri wa Mambo ya Ndani, George Simbachawene amesema Nabii na Mtume, Boniface Mwamposa amekamatwa na jeshi la polisi Dar es Salaam #MwananchiUpdates
Image

February 2nd 2020

51 Retweets417 Likes

sio tu ilikuwa urongo maana “Mtume” aliendesha ibada kama kawaida,

Twitter avatar for @WateteziTVWateteziTV @WateteziTV
MTUME MWAMPOSA AIBUKIA DSM AKIENDESHA IBADA LEO JUMAPILI. Ikiwa ni saa chache tangu Jeshi la Polisi nchini Tanzania litangaze kumtafuta bila mafanikio, Mtume Boniface Mwamposa, kiongozi huyo wa dini ameonekana katika kanisa lake lililopo Kawe jijini DSM akiendesha ibada.
Image

February 2nd 2020

2 Retweets5 Likes

bali pia IGP Sirro alidai wanamtafuta “Mtume” huyo.

Twitter avatar for @MwananchiNewsMwananchi Newspapers @MwananchiNews
Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Simon Sirro amesema juhudi za kumtafuta na kumkamata Mtume Boniface Mwamposa zinaendelea baada ya kumfuatilia bila mafanikio katika viwanja vya ndege na kama ametumia usafiri wa barabara #MwananchiUpdates
Image

February 2nd 2020

50 Retweets499 Likes

Haihitaji uelewa wa utendaji kazi was polisi kubaini kuwa mtu akikamatwa na polisi hawezi kutafutwa na polisi.

Kwanini “Mtume” huyo anakingiwa kifua?

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Kwanini Mzee Meko anamkingia kifua huyo "Mtume" aliyesababisha vifo 20? Is it because of mwanae Bashite? Can you now connect the dots re my suspicion kuhusu uhusika wa Bashite kwenye janga hilo? Nchi inaendeshwa na genge la Mafia
Image

February 4th 2020

2 Retweets27 Likes

Pamoja na sababu nyingine, kuu ni kwamba “Mtume” huyo ni “mtu wa Kamati ya Ufundi” ya Jiwe na mwanae.

Nadhani wengi wenu mnafahamu kuwa baadhi ya haya makanisa mapya yanatumia “nguvu za giza.”

Na “wambeya” wanadai kuwa hata hivyo vifo 20 ni “kafara ya baba na mwanae baada ya upepo wa kisulisuli kuvuma kutoka Marekani.”

Jiwe kwa mara ya kwanza amegundua kuwa “anawindwa na mabeberu,” na anajua bayana kuwa mabeberu hao wakiamua kwa dhati asirudi Ikulu hapo Oktoba, HATORUDI.

Lakini hata kama “Mtume” angekuwa amekamatwa kweli, kwanini aachiwe kwa dhamana ilhali anakabiliwa na kosa kubwa zaidi ya akina Eric Kabendera ah Tito Magoti wanaonyimwa dhamana kila kukicha ilhali makosa tao ni ya kutungwa tu?

Nimalizie kwa kuwakumbusha kuwa Tanzania ya Magufuli inaendeshwa kama kampuni ya genge la Mafia. Kuna uvunjifu mkubwa wa haki za binadamu. Kuna dharau kubwa dhidi ya Katiba. Kuna jeuri dhidi ya hisia zenu walalahoi, kwamba hata mkifanywa nini hamna jeuri ya “kulianzisha.”

Nimalizie pia kwa kubashiri kutokea kwa tukio jingine kubwa katika wiki hii. Sintoshangaa kusikia Membe amevuliwa uanachama, au “breaking news “ kama hizo.

Ndimi jasusi wako,

Evarist Chahali

Comment
Share
Share this post
Mtume Aliyesababisha Vifo 20 Hakukamatwa. Kwanini Serikali ya Magufuli Inawaongopea Kuwa Alikamatwa Na Sasa Kapewa Dhamana?
www.baruayachahali.com

Create your profile

0 subscriptions will be displayed on your profile (edit)

Skip for now

Only paid subscribers can comment on this post

Already a paid subscriber? Sign in

Check your email

For your security, we need to re-authenticate you.

Click the link we sent to , or click here to sign in.

TopNewCommunity

No posts

Ready for more?

© 2022 Evarist Chahali
Privacy ∙ Terms ∙ Collection notice
Publish on Substack Get the app
Substack is the home for great writing