Barua Ya Chahali

Share this post
Milipuko ya Mabomu Uganda, Tahadhari ya Ugaidi Kenya, Mashambulizi ya Kigaidi Msumbiji, DRC ni "Wake-up Call" kwa Mzaha wa Kesi ya "Ugaidi" Dhidi ya Mbowe
www.baruayachahali.com

Milipuko ya Mabomu Uganda, Tahadhari ya Ugaidi Kenya, Mashambulizi ya Kigaidi Msumbiji, DRC ni "Wake-up Call" kwa Mzaha wa Kesi ya "Ugaidi" Dhidi ya Mbowe

Evarist Chahali
Nov 16, 2021
Share

Kuna jamaa yangu mmoja alinitumia ujumbe majuzi kunipongeza kuwa napaswa nijivunie jitihada zangu kwenye sekta ya intelijensia hususan kutupia jicho habari/matishio ya ugaidi.

Nilimshukuru lakini nilikataa pongezi hizo kwa sababu moja kuu. Hupaswi kujivunia kuwa mzalendo, kwa sababu uzalendo sio sifa bali wajibu. Kama ambavyo hatujivuni tunapokula, kwa sababu ni wajibu wetu kufanya hivyo, ndivyo ambavyo uzalendo unapaswa kuwa suala la lazima.

Muda mfupi uliopita kumetokea milipuko miwili ya mabomu jijini Kampala, Uganda. Taarifa za awali zinaonyesha kuwa mtu mmoja amefariki, lakini huenda idadi ikawa ni kubwa zaidi. Milipuko hiyo imetokea mjini kati (city centre) jirani na jengo la bunge la nchi hiyo. Sijivunii kuwa miongoni mwa vyombo vya habar vya kwanza duniani kuripoti tukio hilo. Sijivunii kwa sababu huo ni wajibu, si suala la kujivunia.

Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Breaking News: Bomb Blasts in Central Kampala, Uganda
Breaking News: Bomb Blasts in Central Kampala, UgandaUpdate at 0812GMT Two explosions were Tuesday morning reported downtown Kampala. Photos and videos shared on social media showed heavy clouds of smoke and some cars burning near Jubilee Insurance along Parliamentary Avenue. Parliament has been sealed off by security. Another explosion was reported …ujasusi.org

November 16th 2021

2 Retweets4 Likes

Pengine blogu ya Ujasusi kuwa miongoni mwa vyombo vya habari vya kwanza duniani kuripoti habari hiyo ni sababu tosha kwako kujisajili ili utumiwe habari zinazochapishwa kila siku kuhusiana na ujasusi na majasusi. Jisajili HAPA.

Wakati hayo yakiendelea nchini Uganda, huko Kenya nako kumetolewa tahadhari kuhusu uwezekano wa mashambulizi ya kigaidi katika maeneo ya mpaka kati ya nchi hiyo na Somalia. Tahadhari hiyo imetolewa na Uingereza.

Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Kenya: UK Issues Travel Advisory Against Travelling to Lamu, Mandera and Garissa Counties over Al-Shaabab Attacks
ift.tt/3Dm3ZOW
Image

November 16th 2021

2 Likes

Wakati huo huo, kikundi cha kigaidi cha “wilaya ya Afrika ya Kati” ya kikundi cha kigaidi cha ISIS (Islamic State Central Africa Province, kwa kifupi ISCAP) kinaendelea na kampeni zake za kigaidi nchini Msumbiji na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Nimekuwa nikiripoti mfululizo kuhusu kikundi hicho. Kadhalika nimeandika chambuzi mbili za kiintelijensia kuhusu matishio yaliyopo kwa Tanzania kuhusiana na kikundi hicho.

Twitter avatar for @Jasminechic00Jasmine Opperman @Jasminechic00
#Tanzania Well-done @Chahali on the Insight: The Regionalization Of The Cabo Delgado Insurgency Leaves Tanzania Vulnerable Excellent comments.
Insight: The Regionalization Of The Cabo Delgado Insurgency Leaves Tanzania VulnerableInsight by Evarist Chahali [https://twitter.com/chahali], intelligence analyst. On 05 October 2017, well organized attacks in Cabo Delgado (Mozambique) gave way to warning calls that Southern Africa has crossed the threshold into an Islamist organized extremist footprint. The purpose of th insight …ujasusi.org

October 6th 2021

3 Retweets28 Likes

Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
How Politicisation of 'Tradecraft' - that's the Art of Intelligence - Could Hinder Tanzania Spy Agency’s Counter-Terror Capabilities.
ift.tt/3qfLok0
Image

November 7th 2021

3 Retweets25 Likes

Kwa muda mrefu, wanasiasa mbalimbali wa CCM wamekuwa wakitumia suala la ugaidi kama “mdoli” wa kuwanyanyasia wapinzani. Huko nyuma chama cha CUF kilituhumiwa kuwa cha kigaidi. Na sasa Chadema inazushiwa tuhuma hizo, huku Mwenyekiti wake Taifa, Mheshimiwa Freeman Mbowe, akiendelea kufanyiwa uonevu katika kesi ya kubambikiwa kwamba alipanga vitendo vya kigaidi.

Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Reflecting on what's happening in Uganda right now plus terror alert in Kenya, I'm getting deeply troubled by how authorities in my home country Tanzania are so fond of toying with "terrorism as a political tool vs the opposition" eg ongoing terror case vs @freemanmbowetz

Jasusi @Chahali

Breaking News: Bomb Blasts in Central Kampala, Uganda https://t.co/d0iR0ScOmR

November 16th 2021

6 Likes

Rai yangu kwa serikali ya Mama Samia, Idara ya Usalama wa Taifa, Jeshi la Polisi na CCM kwa ujumla ni fupi: ACHENI KUFANYIA MZAHA SUALA LA UGAIDI.

Mwisho, kuanzia wiki hii, ninawaletea mfululizo wa makala kuhusu suala la uzalendo, na jinsi kudidimia kwake kunavyoweza kuwa tishio kwa usalama kwa Tanzania yetu, Mfululizo huo unachapishwa katika gazeti la RAIA MWEMA kila Jumatano.

Twitter avatar for @ChahaliJasusi @Chahali
Kuanzia wiki hii, ktk gazeti bora kuliko yote TZ la #RAIAMWEMA, naongelea UZALENDO, or rather kuporomoka kwa uzalendo. Najikita zaidi kwenye "jinsi kuporomoka kwa uzalendo kunavyoweza kuwa tishio kwa usalama wa taifa letu." Nitakupeleka DRC, Msumbiji, Nigeria hadi Afghanistan 🙏
Image

November 15th 2021

4 Retweets26 Likes

Siku njema

ShareShare
TopNewCommunity

No posts

Ready for more?

© 2022 Evarist Chahali
Privacy ∙ Terms ∙ Collection notice
Publish on Substack Get the app
Substack is the home for great writing