Barua Ya Chahali

Share this post
Mgogoro NCCR-Mageuzi: Kada wa Chadema Martin Maranja adai "mradi wa kumuondoa Mbatia ni wa Zitto na dola". Amtuhumu Naibu Msajili Nyahoza kuwa anakamilisha kazi ya Zitto. Amhusisha pia Evarist Chahali
www.baruayachahali.com

Mgogoro NCCR-Mageuzi: Kada wa Chadema Martin Maranja adai "mradi wa kumuondoa Mbatia ni wa Zitto na dola". Amtuhumu Naibu Msajili Nyahoza kuwa anakamilisha kazi ya Zitto. Amhusisha pia Evarist Chahali

Evarist Chahali
May 23
1
Share this post
Mgogoro NCCR-Mageuzi: Kada wa Chadema Martin Maranja adai "mradi wa kumuondoa Mbatia ni wa Zitto na dola". Amtuhumu Naibu Msajili Nyahoza kuwa anakamilisha kazi ya Zitto. Amhusisha pia Evarist Chahali
www.baruayachahali.com

Kada wa Chadema Martin Maranja Masese ametoa tuhuma nzito dhidi ya Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo, Mheshimiwa Zitto Kabwe kuhusiana na jaribio la mapinduzi dhidi ya Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi Taifa, Mheshimiwa James Mbatia.

Read Barua Ya Chahali in the new Substack app
Now available for iOS

Katika bandiko lake kwenye ukurasa wake kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter lililochapishwa jana Mei 22 mnamo saa 9 na dakika 55 kwa majira ya hapa Uingereza, kada huyo alidai kwamba, namnuku,

Mradi wa kumuondoa James Mbatia ni mradi wa Zitto Kabwe na dola. Tunajua jambo la Zitto ni lako (mimi Evarist Chahali) pia. Zitto aliwalipia wajumbe wa NCCR kwenda Dodoma kwenye TCD ili kumkomoa Mbatia aliyesusia. [Sisty] Nyahoza (Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa Tanzania) anakamilisha kazi ya Zitto. Chadema hatuna ugomvi na NCCR. Tunaitaka NCCR imara.

Twitter avatar for @IAMartin_Martin Maranja Masese @IAMartin_
Mradi wa kumuondoa James Mbatia ni mradi Zitto Kabwe na dola. Tunajua jambo la Zitto ni lako pia. Zitto aliwalipia wajumbe wa NCCR kwenda Dodoma kwenye TCD ili kumkomoa Mbatia aliyesusia. Nyahoza anakamilisha kazi ya Zitto. CHADEMA hatuna ugomvi na NCCR. Tunaitaka NCCR imara. https://t.co/a9zhJuYnJl

๐‰๐š๐ฌ๐ฎ๐ฌ๐ข @Chahali

Naona kuna jitihada kubwa miongoni mwa baadhi ya wana-CDM kumnusuru Mbatia. Ushirikiano baina ya vyama ni jambo jema. However, Mbatia anavuna alichopanda. I guess wanaomsapoti wamesahau "mkataba baina ya Mbatia na Mwendazake" 2020, only that the latter took the former for a ride https://t.co/2Wnk3wH6Yg

May 22nd 2022

54 Retweets413 Likes

Kada huyo mwenye wafuasi 355,131 alitoa tuhuma hizo nzito alipojibu hii ya twiti yangu (Evarist Chahali)

Twitter avatar for @Chahali๐‰๐š๐ฌ๐ฎ๐ฌ๐ข @Chahali
Naona kuna jitihada kubwa miongoni mwa baadhi ya wana-CDM kumnusuru Mbatia. Ushirikiano baina ya vyama ni jambo jema. However, Mbatia anavuna alichopanda. I guess wanaomsapoti wamesahau "mkataba baina ya Mbatia na Mwendazake" 2020, only that the latter took the former for a ride
Image

May 22nd 2022

2 Retweets11 Likes

Twiti hiyo yangu kama Evarist Chahali ilikuwa ikizungumzia twiti ya Meya wa zamani wa Manispaa ya Ubungo, Boniface Jacob aliyekuwa akieleza kuhusu mgogoro unaoendelea wa chama cha NCCR-Mageuzi

Image

Twiti hiyo ya tuhuma za kada huyo ilipata ritwiti ya mwanaharakati maarufu mtandaoni Maria Sarungi mwenye wafuasi zaidi ya milioni moja (ikimaanisha kuwa imeonwa na watu wengi)

Image

Hadi wakati makala hii inachapishwa, twiti hiyo ilikuwa na ritwiti 54 na โ€œlikesโ€ 410.

Barua Ya Chahali
Uchambuzi wa kiintelijensia kuhusu mkutano wa majadiliano kati ya Mama @SuluhuSamia na viongozi wakuu wa Chadema
Rais Samia Suluhu Hassan jana alikutana na viongozi wakuu wa Chadema wakiongozwa na Mwenyekiti wa taifa wa chama hicho, Mheshimiwa Freeman Mbowe, katika mkutano wa majadiliano ulifanyika Ikulu ya Chamwino huko Dodoma. Kama ilivyokuwa kwenye matukio mawili ya Rais Samia kukutana na Mheshimiwa Mbowe, Machi 4 mwaka huu na majuzi Mei 9, taarifa za mkutano wa jana hazikufahamika hadi baada ya mkutano huo kukamilikaโ€ฆ
Read more
20 days ago ยท Evarist Chahali

Jitihada za kumpata Mheshimiwa Zitto kuongelea tuhuma hizo hazikuzaa matunda lakini mimi kama Evarist Chahali bado natafakari hatua stahili za kuchukua kutokana na uzito wa tuhuma hizo.

Barua Ya Chahali
Dear Mama @SuluhuSamia, mabalozi hawa wawili wanakuhujumu
Inatanabaishwa kuwa moja ya dhambi kuu kwenye taaluma ya intelijensia ni kushindwa kutahadharisha. Hii inachangiwa na ukweli kwamba taaluma hiyo inatarajiwa zaidi kubaini matishio ya kiusalama kabla hayajasababisha madhara. Makala hii ya kiintelijensia inaeleza kuhusu hujuma za mabalozi wawili wa Tanzania wanavyomhujumu Rais Samia Suluhu pamoja na Tanzania kwa ujumlaโ€ฆ
Read more
19 days ago ยท 1 like ยท Evarist Chahali

Tuhuma hizi zinakuja siku chache tu baada ya Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Mheshimiwa Freeman Mbowe, kuwakemea vikali vijana wa chama hicho na kuwataka wawe na heshima na staha hata kwa watu wanaotofautiana nao kifikra.

Twitter avatar for @darmpya_Darmpya Blog @darmpya_
@freemanmbowetz amekiri kwamba kuna wakati Vijana wa @ChademaTz huwakosea heshima hususani mitandaoni watu ambao wanakuwa na mawazo tofauti na mawazo yao, Mbowe amewakemea vikali vijana wa chama hicho na kuwataka wawe na heshima na staha hata kwa watu wanaotofautiana nao kifikra
Image

May 11th 2022

13 Retweets122 Likes

Kadhalika, Mheshimiwa Mbowe alisisitiza kuhusu heshima kwa viongozi wa vyama vingine

Wakati hayo yakitokea, kada huyo wa Chadema alimtuhumu Mbunge wa Viti Maalum kwa tiketi ya CCM, Mheshimiwa Neema Lugangira, kumtumia twiti ambazo kwa maelezo ya mbunge huyo ni twiti feki

Twitter avatar for @IAMartin_Martin Maranja Masese @IAMartin_
Mkimuona @neemalugangira mshtueni, kama ombi dogo hili amezima data, tukihamia CCM anavyotaka, atatusaidia kutimiza hayo malengo? Sasa hivi anasoma Twitter kama anaaga maiti.. kwa mbaaali!๐Ÿ˜
Image
Image

May 22nd 2022

37 Retweets611 Likes
Twitter avatar for @neemalugangiraNeema Lugangira @neemalugangira
@IAMartin_ Namshukuru aliyetengeneza tweet hiyo maana amedhihirisha hatari kubwa zaidi ambayo sisi Wabunge Wanawake tupo ya kutengenezewa taarifa za uongo na kudukuliwa jambo nililosema Bungeni juzi 20/5/2022 ila amesahau Twitter for iPhone ๐Ÿ˜… @Nnauye_Nape @wizarahmth @MsigwaGerson @TCRA_Tz

May 22nd 2022

18 Likes
Twitter avatar for @IAMartin_Martin Maranja Masese @IAMartin_
@neemalugangira @Nnauye_Nape @wizarahmth @MsigwaGerson @TCRA_Tz Sasa nani yule aliyekuja kuleta ofa ya mimi kuhamia CCM kutimiza malengo yangu? Una parody lako?

May 22nd 2022

1 Retweet45 Likes
Twitter avatar for @neemalugangiraNeema Lugangira @neemalugangira
@IAMartin_ @Nnauye_Nape @wizarahmth @MsigwaGerson @TCRA_Tz Kaka yangu @IAMartin_ wewe sio mgeni kuona Tweet zangu hivyo ninaamini kabisa ulipaswa ushangae maana hiyo sio lugha yangu. Aidha, kwakuwa wewe sio mgeni Twitter ulipaswa kufanya due dilligence ndogo ujiridishe kama ni AUTHENTIC. Ila namshukuru kaipa hoja yangu uzito bila kujua.

May 22nd 2022

7 Likes

Jitihada za kumpata Mheshimiwa Neema kusikia reaction yake kuhusiana na twiti hizo zinaendelea.

Makala hii ni endelevu

Siku na wiki njema.

Share Barua Ya Chahali

Share this post
Mgogoro NCCR-Mageuzi: Kada wa Chadema Martin Maranja adai "mradi wa kumuondoa Mbatia ni wa Zitto na dola". Amtuhumu Naibu Msajili Nyahoza kuwa anakamilisha kazi ya Zitto. Amhusisha pia Evarist Chahali
www.baruayachahali.com
TopNewCommunity

No posts

Ready for more?

ยฉ 2022 Evarist Chahali
Privacy โˆ™ Terms โˆ™ Collection notice
Publish on Substack Get the app
Substackย is the home for great writing