Barua Ya Chahali

Share this post
Mgogoro Kati Ya Jiwe na Kimombo
www.baruayachahali.com

Mgogoro Kati Ya Jiwe na Kimombo

Kunahitajika Mjadala Wa Kitaifa Kuhusu Mustakabali Wa Kiswahili

Evarist Chahali
Jun 3, 2019
8
Share this post
Mgogoro Kati Ya Jiwe na Kimombo
www.baruayachahali.com

Nianze kwa kuwashukuru wengi mliojitokeza kujisajili upya kwa ajili ya muundo mpya wa kijarida hiki, ambapo kwa malipo kidogo tu ya sh 50,000 kwa mwaka, “mwanachama” (paid subscriber) atatumiwa sio tu kijarida hiki bali vijarida vingine vinne.

Idadi ya waliokwishajisajili ni watu 70. Pengine inaweza kuonekana ni idadi ndogo lakini kwangu ni bora niwatumikie watu wawili wanaothamini jitihada zinazowezesha utumishi wangu kwao kuliko lundo la mamia ya watu ambao miongoni mwao hawana hata muda wa kufungua baruapepe ninazowatumia.

Nimalizie utangulizi huu kwa kuwajulisha nyote mliojisajili kuwa nimewatumia toleo la kwanza la #BaruaYaShushushu.

Ninakaribisha maoni kuhusu kijarida hicho.

Twende kwenye mada ya leo. Lakini kabda ya kuingia kwenye mada hii, naomba kutumia twiti ifuatayo kama reference

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Mie ni mdau mkubwa wa Kiswahili na nilifundisha Kiswahili Chuo Kikuu hapa Uk. Nimechapisha vitabu 7 kwa Kiswahili. Nimekuwa mwandishi wa makala (zilizo kwa Kiswahili) kwa takriban miaka 20.Hata hivyo, napinga kutumia "mahaba kwa Kiswahili" kama kisingizio cha kutomudu Kiingereza

singolile osiah @MwabunguluOsiah

@Chahali @Kiganyi_ @kaccy24 @TitoMagoti Here my opinion is,English is a business language,Hapo twambiane ukweli wa Tanzania wenzangu,kama tuna promote kiswahili never mind,ila juwa kidogo lugha nyingine kwa ajili ya BIASHARA then we can win,Go UK alafu kaongee kiswahili kama utasikilizwa na mtu.

June 1st 2019

2 Retweets24 Likes

Niliandika twiti hiyo kama mchango wangu katika mjadala uliovuma wiki iliyopita kuhusu “Kiingereza za Jiwe” (Magufuli).

Kimsingi uwezo duni wa Kiingereza cha mkuu huyo wa nchi haukupaswa kuwa jambo la mjadala laiti wahuni wanaofahamika kama MATAGA (Make Tanzania Great Again) wasingelikoroga. Na uthibitisho ni huu hapa

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Dear @MagufuliJP Ndio nini hii sasa? Yaani Rais kuendesha mkutano kwa Kiingereza nayo ni habari? Hao #MATAGA hawana tofauti na wahujumu uchumi, maana licha ya fungu kubwa walilotengewa, akili ni nil, zip, zilch, nada, zero, sifuri
Image

May 28th 2019

12 Retweets128 Likes

MATAGA ni wababaishaji flani walioajiriwa huko Idara ya Usalama wa Taifa wakiwa hawajui A wala B kuhusu taaluma hiyo, na kwa vile ajira zao zilikuwa za upendeleo, wala hawakupelekwa “Malindi” (Mbweni ) kwenye chuo cha Idara hiyo ambapo kila afisa anayejiunga anatakiwa kufanya kozi inayofahamika kama JBC.

Sasa hao vichwapanzi wa MATAGA waliokotwa tu mtaani, kigezo muhimu kikiwa kutoka Kanda ya Ziwa kama Jiwe, na kukabidhiwa majukumu yaliyo nje kabisa ya uwezo wao. Matokeo yake wamekuwa wakitusumbua mitandaoni.

Jiwe mwenyewe amenukuliwa mara kadhaa akitanabaisha kuwa hao MATAGA ni watupu kabisa kichwani. Na jukumu pekee wanalolimudu ni kusifia hata visivyostahili kusifiwa. Ndio hawa wanaitwa “praise team.”

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Praise team ikijiandaa kuingia kwenye sosho midia kumtetea Jiwe
Image

June 2nd 2019

3 Likes

Turudi kwenye ishu ya “Kiingereza cha Jiwe.” Kwamba lugha hiyo inamsumbua Jiwe, hilo halina mjadala. Lakini halipaswi kuwa suala la maana sana hasa ikizingatiwa kuwa background ya Jiwe ni katika sayansi (Kemia), na si ajabu kwa wenzetu waliosoma masomo ya sayansi kusumbuliwa na Kiingereza.

Tatizo la MATAGA ni kwamba Jiwe alipooendesha “mkutano muhimu” kwa Kiingereza, ilikuwa ni habari ya kujivunia. Yaani “kuwananga wale wanaomtuhumu Jiwe kuwa anachapia kwenye lugha hiyo ya Malkia Elizabeth wa Pili.” Lakini Jiwe alipolikoroga kwenye dhifa ya kitaifa huko Zimbabwe ambapo alishindwa kuongea Kiingereza, na MATAGA kwa uchovu wao wakashindwa kuwa wakalimani, MATAGA hao hao wakaanza kukiponda Kiingereza kilekile walichomsifia Jiwe alipoongoza “mkutano muhimu.”

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Oh poor Jiwe. Mko wapi praise team mliomsifia juzi kuwa kaongoza mkutano muhimu kwa Kiingereza? Jiwe na Kiingereza = Jiwe na haki za binadamu/demokrasia
Image
Image
Image
Image

May 30th 2019

18 Retweets88 Likes

Tukiweka kando “ugomvi kati ya Jiwe na Kiingereza” na ubabaishaji wa praise team wa MATAGA, kuna haja ya msingi kwa sisi kama Taifa kuwa na mjadala mpana kuhusu mustakabali wa Kiswahili. Tatizo lililopo ni zaidi ya mapungufu ya akina Jiwe. Tatizo ni kwamba tupotupo tu. Kiingereza ni mgogoro kwa Watanzania wengi, lakini kwenye Kiswahili nako tunakutana na lundo la wababaishaji wanaojifanya hawawezi kuongea Kiswahili “full-time” na inawalazimu kuchanganya Kiswahili na Kiingereza. Sikiliza wabunge wwetu wanavyojifanya hawajui Kiswahili vizuri.

Jiwe ameahidi kupeleka walimu wa Kiswahili huko Afrika Kusini, Namibia na Zimbabwe lakini porojo hizo hazijaanza leo. Na kwa bahati mbaya, zitaendelea kwa muda mrefu.

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Eneo moja ambalo Kiswahili kina wakati mgumu sana ni katika sayansi na teknolojia. Kwa bahati mbaya, sayansi na teknolojia ni kama roho ya dunia ya sasa. Kiswahili ni muhimu lakini Kiingereza bado ni muhimu pia hasa katika nyanja ambazo ni ngeni kwetu au ambapo tunasuasua

Evarist Chahali @Chahali

Mie ni mdau mkubwa wa Kiswahili na nilifundisha Kiswahili Chuo Kikuu hapa Uk. Nimechapisha vitabu 7 kwa Kiswahili. Nimekuwa mwandishi wa makala (zilizo kwa Kiswahili) kwa takriban miaka 20.Hata hivyo, napinga kutumia "mahaba kwa Kiswahili" kama kisingizio cha kutomudu Kiingereza https://t.co/DjSZPPcp2r

June 1st 2019

1 Retweet5 Likes

Kuna mjadala ambao ulikufa kabla haujaanza kuhusu matumizi ya Kiswahili sekondari hadi chuo kikuu. Pengine ni muhimu kuufufua mjadala huu japo binafsi sidhani kama Kiswahili kinajitosheleza kiasi cha kuweza kutumika kama lugha ya kufindishia sekondari hadi chuo kikuu.

Tunatakiwa kama taifa tuamue moja, aidha Kiswahili ni muhimu kuliko Kiingereza na si kwa maneno tu bali kwa vitendo pia, au Kiingereza ni muhimu kuliko Kiingereza na akina Jiwe wafanye bidii kuboresha uwezo wao kwenye lugha hiyo, au - na hili kwangu naona ndio wazo zuri zaidi - kukipa kipaumbele Kiswahili kama lugha ya taifa lakini kutosahau nafasi ya Kiingereza hususan kwenye masuala ya kimtaifa na “maeneo mageni” kama ya sayansi na teknolojia.

Nikamilishe toleo hili kwa kuwakumbusha wanaohitaji kujisajili upya kuwa “wanachama” (paid subscribers) wa kijarida hiki, usajili unaendelea BONYEZA HAPA

Nakutakia siku na wiki njema.

Ndimi mtumishi wako

Evarist Chahali

Comment
Share
Share this post
Mgogoro Kati Ya Jiwe na Kimombo
www.baruayachahali.com

Create your profile

0 subscriptions will be displayed on your profile (edit)

Skip for now

Only paid subscribers can comment on this post

Already a paid subscriber? Sign in

Check your email

For your security, we need to re-authenticate you.

Click the link we sent to , or click here to sign in.

TopNewCommunity

No posts

Ready for more?

© 2022 Evarist Chahali
Privacy ∙ Terms ∙ Collection notice
Publish on Substack Get the app
Substack is the home for great writing