Mchungaji Msigwa 'Aamuriwa' na Lema Kufuta Twiti Iliyoshauri Kuwa Chenge Ndio Anafaa Kuwa Spika, Aifuta, Kisha Airejesha 'Kiaina.'
Majuzi, Mbunge wa zamani wa jimbo la Iringa Mjini kwa tiketi ya Chadema, Mchungaji Peter Msigwa, “aliamuriwa” na kiongozi mwenzie wa chama hicho, Godbless Lema, Mbunge wa zamani wa jimbo la Arusha Mjini, kufuta twiti iliyoshauri kuwa mwanasiasa mkongwe wa CCM, Andrew Chenge, ndiye anafaa kuwa spika.