Mama Samia vs Askofu Gwajima: Uchambuzi wa Kiintelijensia Kuhusu Mtifuano Mkubwa wa Kisiasa Ndani ya CCM
Mnamo Mei 30, 2025, Rais Samia Suluhu Hassan alizungumza waziwazi na kauli yake ilionekana kumlenga Askofu Josephat Gwajima moja kwa moja. Hii ilitokea baada ya Gwajima, ambaye ni Mbunge wa CCM na pia mjumbe muhimu wa chama, kusema hadharani akilalamikia matukio ya utekaji nyara wa watu wasiojulikana, akihusisha vyombo vya serikali.
Kauli ya Rais Samia imeleta mjadala mkubwa. Uchambuzi huu w kiintelijensia unatoa tafsiri pana ya sakata hili, kwa nini Rais alisema vile, na pamoja na mambo mengine, nini matokeo yake kwa usalama na kwa maisha ya Gwajima ndani ya CCM.
Kauli ya Rais Samia: Maana Yake Rahisi
Maneno Muhimu ya Rais Samia
Kwenye hotuba yake, Rais Samia alisema maneno haya:
"Anayefaa aambiwe anafaa, asiyefaa tuseme huyu ana kasoro moja, mbili, tatu. Hatufai kwa huko mbele tunako kwenda."
"Tukitoa mwanya ndugu zangu tukipitisha wanaotafuta tu na mie niwemo. Ndio tunapata wale wanaokwenda huko. Chama kinakuwa 'Gwajima-nised'."
"Kwa hiyo kwa vyovyote vile, tusi-'Gwajima-nise' hiki chama chetu. 'Magwajima' tuyaache nje. Hamna kuoneana aibu wala haya."
"Wajua kule Zanzibar kuna mtu aliomba mcheza ngoma si yake lazima ataharibu. Akasema hawi sawa na wenzake. Yeye anakuwa 'Majudhubu'. 'Majudhubu' ni mtu ambaye hazimo hazimo hivi. Kwa hiyo ukicheza ngoma si yako utaharibu na utajulikana tu. Lazima utasema mie siye jamani ndo haya yanayotokea."