Barua Ya Chahali

Share this post
Magufuli Akosolewa Na Swahiba Yake Mkuu Raila Kuhusu Korona Tanzania
www.baruayachahali.com

Magufuli Akosolewa Na Swahiba Yake Mkuu Raila Kuhusu Korona Tanzania

Evarist Chahali
May 7, 2020
Comment
Share

Kuna makala ya uchambuzi wa kiintelijensia kuhusu suala la korona nchini Tanzania na mustakabali wa utawala wa Rais John Magufuli, na ninachoweza “kukuibia” msomaji ni mtazamo wangu kuwa “korona itaondoka na Magufuli” (si kwa maana ya gonjwa hilo kuchukua uhai wake -siwezi kumwombea mtu maambukizi ya ugonjwa huo hata awe adui yangu mkubwa — bali “uhai wa utawala wake.”)

Na miongoni mwa mambo niliyoongelea ni uwezekano mkubwa kwa Magufuli kutengwa na nchi jirani kwa sababu mzaha wake katika kushughulikia janga la korona una athari kwa majirani wa Tanzania pia. Endapo nchi hizo zitafanikiwa kudhibiti janga hilo, zitalazimika kuidhibiti Tanzania, kwa sababu kinyume chake watajikuta wanarudishwa nyuma.

Taarifa kutoka Uganda na Rwanda zinaeleza kuwa tayari kuna dalili za chuki dhidi ya Watanzania, hali inayoweza kusambaa kwa nchi nyingine majirani zetu.

Na pengine ishara kubwa zaidi ya “yajayo,” ni mahojiano haya aliyofanyiwa swahiba mkubwa wa Magufuli, mwanasiasa maarufu wa Kenya, Raila Odinga, ambaye bila kuuma maneno amemlaumu rafiki yake “kidiplomasia” kwa kusema “anashauriwa vibaya.”

Kwa upande mwingine, upuuzi alioongea Magufuli Jumapili kuhusu “papai liitwalo Elizabeti Anne”

Twitter avatar for @JamiiForumsJamii Forums @JamiiForums
Rais Magufuli: Sampuli ya Fenesi iliyopewa jina la Sara Samweli matokeo yake yalikuwa 'inconclusive' - Sampuli ya Papai tukaipa jina ya Elizabeth Anne, majibu yakawa Positive kwamba lina Corona kwamba maji ya ndani ya papai yana #COVID19 #JFLeo #coronavirusTanzania #Corona

May 3rd 2020

5 Retweets40 Likes

na madudu mengine kama hayo, na hatimaye kusimamishwa kazi kwa Mkuu wa Maabara Kuu ya Serikali Dkt Nyambura Moremi,

Twitter avatar for @JamiiForumsJamii Forums @JamiiForums
WAZIRI UMMY MWALIMU AAGIZA MKURUGENZI MAABARA YA TAIFA YA AFYA KUSIMAMISHWA KAZI > Dkt. Nyambura Moremi na Meneja Uthibiti na Ubora, Jacob Lusekelo wamesimamishwa kupisha uchunguzi > Pia, ameunda Kamati kuchunguza mwenendo wa maabara hiyo Soma
jamii.app/WaziriAgizoKus… #JFLeo
Image

May 4th 2020

14 Retweets104 Likes

tamko la Bashite kuwa wabunge wa Chadema walioji-isolate warudi Dodoma ndani ya masaa 24

Twitter avatar for @HabariSpeciallyHabari Specially @HabariSpecially
Makonda Atoa Masaa 24 Kwa Wabunge wote waliogoma kushiriki vikao vya Bunge na kwenda Dar Warudi Bungeni....,Vinginevyo Watakamatwa
Image

May 6th 2020

na tangazo la Mtu Mfupi Ndugai kuwa Mwambe arejee Bungeni,

Twitter avatar for @raizeronlineRaizer Online Media @raizeronline
Spika Job Ndugai, amemuagiza Mbunge wa Ndanda, Cecil Mwambe, kurejea Bungeni na kuendelea na shughuli zake za kawaida, kwa kuwa barua ya Katibu Mkuu wa @ChademaTz @jjmnyika ya kutomtambua Mbunge huyo kutokuwa na maana yoyote na kwamba haina uthibitisho wa vikao halali.
Image

May 6th 2020

1 Retweet1 Like

kwa pamoja ni jitihada za makusudi za serikali ya Magufuli kuwatoa relini, msitafakari kuhusu uhuni unaofanywa na serikali hiyo kwenye janga la korona, mbaki mnajadili upuuzi wao.

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Mwendelezo wa vita ya kisaikolojia ya @MagufuliJP ambapo anafanya kila kitihada "kuwaondoa Watanzania relini" kwenye janga la korona linaloendelea kugharimu uhai wa ndugu, jamaa na rafiki kwa wingi. Japo nina imani kuwa huu ni mwanzo wa mwisho wa Magufuli, vioja zaidi vyaja

Evarist Chahali @Chahali

@MagufuliJP's psychological warfare continues https://t.co/SPFRvLBFuL

May 6th 2020

16 Likes

Unfortunately, it is working maana Watanzania kwa kudakia matukio hawajambo.

Enewei, chukua tahadhari dhidi ya korona, jikinge na uwakinge wenzio pia.

Ndimi mtumishi wako,

Evarist Chahali

CommentComment
ShareShare

Create your profile

0 subscriptions will be displayed on your profile (edit)

Skip for now

Only paid subscribers can comment on this post

Already a paid subscriber? Sign in

Check your email

For your security, we need to re-authenticate you.

Click the link we sent to , or click here to sign in.

TopNewCommunity

No posts

Ready for more?

© 2022 Evarist Chahali
Privacy ∙ Terms ∙ Collection notice
Publish on Substack Get the app
Substack is the home for great writing