Maafisa kadhaa wa Idara ya Usalama wa Taifa "wajiumbua" kwa kutaja nyadhifa zao serikalini katika orodha ya wahudhuriaji wa mkutano wa tabia-nchi (COP28) huko Dubai
Japo msingi wa taaluma ya intelijensia ni usiri, kitu ambacho chayumkinika kuwa ni siri kuu zaidi ni utambulisho (identity) wa Afisa wa Idara ya Usalama wa Taifa ya nchi yoyote ile.
Kuna sababu kadhaa za kulinda ID ya Afisa wa Idara ya Usalama wa Taifa, lakini moja ya msingi ni ukweli kwamba kila Idara ya Usalama wa Taifa duniani hujihangaisha kuwafahamu maafisa wa Idara za Usalama wa Taifa za nchi nyingine kwa lengo moja muhimu: kuwarubuni waweze kuzisaliti nchi zao na kuwa “majasusi ndumilakuwili”, kwa kimombo/kiintelijensia double agents.
Nini kimetokea?
Baada ya kusambaa kwa taarifa kuwa nchi mbalimbali za Afrika zimepeleka lundo la wajumbe kwenye mkutano wa tabia-nchi huko Dubai, unaofahamika kama COP28, wafuatiliaji mbalimbali mtandaoni waliibuka na orodha za wajumbe walioalikwa kwenye mkutano huo, ikiwa ni pamoja na orodha ya wajumbe wa Tanzania.
Kama inavyoonekana kwenye orodha, kila mjumbe ameandika jina kamili na wadhifa alionao (angalia picha zenye orodha hiyo hapa chini)