Barua Ya Chahali

Share this post
Kwaheri Aprili, Mei Hii Yaja na Mazito
www.baruayachahali.com

Kwaheri Aprili, Mei Hii Yaja na Mazito

Kuna Ishara Za Matukio Makubwa Yatakayoweza Kubadili Mwenendo Wa Taifa

Evarist Chahali
Apr 30, 2019
20
Share this post
Kwaheri Aprili, Mei Hii Yaja na Mazito
www.baruayachahali.com

Naomba nianze #BaruaYaChahali kwa kumshukuru Mungu kwa kunisuru tena sijui kwa mara ya ngapi. Muda huu unaposoma Barua hii ningekuwa marehemu. Kwa kifupi, Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa, Mchungaji Modestus Kipilimba alimtuma “afisa muuaji wa Kitengo” anaitwa Allan (naomba nihifadhi jina la pili kwa sababu maalum) kuja kuniua hapa Uskochi.

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Idara ya Usalama wa Taifa chini ya Mchungaji Feki Kipilimba yaendelea kuchezea mamilioni ya fedha za walipakodi kwa ajili ya operesheni zake fyongo kuwinda watu huku nje ili wauawe. Hawajawahi kufanikiwa kwa sababu hawa wazembe ni DHAIFU mno. However, unayeumia ni wewe mlipakodi.
Image

April 26th 2019

14 Likes

Bahati nzuri, mie “paka mwenye roho tisa” nikasalimika kwa mapenzi ya Mungu.

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Dear Mchungaji KIPILIMBA, I'm a cat with 9 lives 😊V
Image

April 26th 2019

4 Likes

Awali, huyo muuaji Allan alishatumwa nchi mmoja ya Skandinavia kwenda kumuua Mtanzania flani lakini bahati nzuri msamaria mwema flani aliisikia hiyo ishu akamshtua mhusika, ambaye nae ikabidi aitangaze ishu hiyo hadharani, na kupelekea muuaji huyo kuachana na mpango huo wa kishetani.

Kipilimba sio tu ni kiongozi wa dini lakini pia ni mkuu wa kanisa analomiliki.

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
#Tanzania is only country in the world whose intelligence agency chief, Dr Modestus Kipilimba, is also a head of a self-made pentecostal church | Tanzania ndio nchi pekee duniani ambayo mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa, Mchungaji Kipilimba pia ni mkuu wa kanisa lake binafsi 😊7
Image

April 26th 2019

13 Retweets109 Likes

Kwamba anaweza kumtuma afisa wake Allan (au mwingine) kuja huku kwa dhamira ya kutuua, ni ishara kuw serikali ya Magufuli inaongozwa na mashetani. Na yeye Magufuli mwenyewe ni shetani pia kwa sababu aliridhia mpango huo wa Allan kuja kuniua. Hata hivyo, Mungu wangu ni mwema sana, na kamwe hawa majahili hawatofanikiwa katika azma zao za kishetani.

Kuna shetani anaitwa Jack Zoka, alikuwa Naibu Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa, zama za Kikwete, alitumia muda wake wote ofisini kujaribu kuniangamiza, akaishia kuondoka madarakani bila azma yake hiyo ya kishetani kutimia. Akapewa ubalozi Canada lakini akaishia kutumbuliwa baada ya serikali ya nchi hiyo kutoafiki utendaji kazi wake.

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
I just published “Balozi Wa Tanzania nchini Canada, shushushu mstaafu Jack Zoka ‘Amaliza Muda Wake.’ Je Ametumbuliwa?”
Balozi Wa Tanzania nchini Canada, shushushu mstaafu Jack Zoka “Amaliza Muda Wake.” Je Ametumbuliwa?Balozi wa sasa wa Tanzania nchini Canada, aliyekuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa zamani wa Idara ya Usalama wa Taifa, Jack Zoka, anarudi…medium.com

March 30th 2018

7 Retweets65 Likes

Mrithi wake, Robert Msalika Makungu, nae akaendeleza aliposhia Zoka, akafanya jitihada kadhaa za kutaka kunidhuru, akaishia kutumbuliwa na Magufuli, na sasa anahangaika kama RAS huko Tabora.

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
#BreakingNews President @MagufuliJP demotes Deputy Director General of Tanzania Intelligence Service to become Tabora Regional Administrative Secretary
Image

April 20th 2018

5 Retweets22 Likes

Huyu shetani kwa kushirikiana na “m-Kanda wa Ziwa” mwenzake, ambaye nae ni RAS kama yeye, Eliakim Maswi, walitumia toilet paper ya Musiba kuandika habari ya kunichafua.

Kabla ya kumtuma huyo muuaji Allan, Kipilimba alijaribu kumtumia Diwani mmoja wa Chadema ambaye sio tu ni pandikizi la Idara ya Usalama wa Taifa bali ni afisa mwandamizi wa taasisi hiyo. Diwani huyo anasoma PhD yake hapa Uskochi, na kwa takriban miaka miwili amekuwa kwenye jitihada endelevu za kunidhuru akishirikiana na binti mmoja ambaye hadi majuzi niliposhtukia mpango huo dhalimu, alikuwa rafiki yangu wa karibu kwa kama miaka minne hivi.

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Ndugu zangu wa upinzani, naomba kuwatahadharisha kuwa kuna Diwani wa Chadema ni Afisa wa Idara ya Usalama wa Taifa, ana kificho cha hali ya juu (deep cover). Hivi sasa ana assignment mbili, moja kunichafua mtandaoni na nyingine endelevu ya kuniua. Anasoma hapa Uingereza

January 16th 2019

6 Retweets75 Likes

Tunaingai Mwezi Mei baada ya Aprili kusheheni kila aina ya madudu - kuanzia Magufuli kupokea ripoti ya CAG kimya kimya

Twitter avatar for @zittokabweZitto Kabwe Ruyagwa @zittokabwe
Ripoti za CAG zilivyopokelewa miaka ya nyuma na ilivyopokelewa mwaka 2019 ( picha ya 4 😁😁😁 ). Kuongoza ni MAARIFA wazee......! Wang’amuzi wa mambo walipoona tu Ripoti ya TAKUKURU na Sarakasi za kutaifisha majumba walijua kuna kitu chafichwa. Kumbe Ripoti ya CA
Image
Image
Image
Image

March 29th 2019

99 Retweets769 Likes

hadi Mtu Mfupi Ndugai kutangaza kuwa Bunge lake halitofanya kazi na CAG,

Twitter avatar for @bbcswahiliBBC News Swahili @bbcswahili
Bunge la Tanzania laazimia kutofanya kazi na CAG baada ya kumtia 'hatiani' kwa kudharau mhimili huo
Bunge la Tanzania lamtia ‘hatiani’ CAGKiongozi wa Upinzani Bungeni Freeman Mbowe amelieleza Bunge kuwa hatua hiyo dhidi ya CAG ni kuminya mawazo ya watu.bbc.in

April 2nd 2019

20 Retweets197 Likes

kabla ya kufahamishwa kuwa serikali ya Magufuli imefanya ufisadi wa kutisha kama ulivyotanabaishwa kwenye ripoti hiyo ya CAG,

Twitter avatar for @IsmailJussaIsmail Jussa @IsmailJussa
"Shilingi 4.8 Trilioni zimetumika bila kupita kwenye Mfuko Mkuu wa Hazina. Ripoti ya CAG (Uk. 91) inasema: Ikilinganishwa taarifa ya kutoa fedha (exchequer issue report) na taarifa ya fedha zilizopokelewa na kuripotiwa katika taarifa za fedha za Mafungu husika." @zittokabwe
Image

April 14th 2019

23 Retweets96 Likes

na tukapata ahueni baada ya kupatikana taarifa kuwa jitihada za kumng’oa CAG Prof Assad zimegonga mwamba,

Twitter avatar for @UhurubilamipakaMwanaHALISI Digital @Uhurubilamipaka
Prof. Assad agoma kujiuzulu >>>
mwanahalisionline.com/prof-assad-ago…
Image

April 19th 2019

50 Retweets360 Likes

Twitter avatar for @zittokabweZitto Kabwe Ruyagwa @zittokabwe
CAG agoma rasmi kujiuzulu adai hakuna kipengele kwenye Katiba alichovunja kinachomlazimu ajiuzulu - JamiiForums
jamiiforums.com/threads/cag-ag… via @JamiiForumsCAG agoma rasmi kujiuzulu adai hakuna kipengele kwenye Katiba alichovunja kinachomlazimu ajiuzulu - JamiiForumsMKAGUZI na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Mussa Assad, amegoma kujiuzulu kutoka kwenye wadhifa wake. Anaripoti Saed Kubenea … (endelea). Taarifa kutoka kwa watu waliokaribu na kiongozi huyo, wakiwamo baadhi ya watendaji serikalini na katika Chama Cha Mapinduzi (CCM), zinaeleza...jamiiforums.com

April 19th 2019

73 Retweets593 Likes

na mwezi ukahitimishwa na kituko cha karne kwa Mbilikimo Ndugai kuendeleza mashambulizi yake dhidi ya CAG Assad

Twitter avatar for @Kwanza_TVKwanza TV @Kwanza_TV
"Watu wanawaaminisha Watanzania kuwa kila kilichoandikwa na CAG au ofisi yake ni ukweli asilimia 100. Sio hivyo, yapo mambo mle si kweli hata kidogo. Zile ni hoja, ndio maana kamati za PAC na LAAC zinachambua kila kitu."- Spika wa Bunge, Job Ndugai. #KwanzaHabari
Image

April 26th 2019

5 Retweets39 Likes

huku mmoja wa mawaziri wa ovyo kabisa katika historia ya Tanzania, mvaa mabendera Kangi Lugola akitishia kuvua nguo kufuatia tuhuma za ufisadi katika Wizara yake kama zilivyotanabaishwa na CAG na kuthibitishwa na Magufuli.

Twitter avatar for @swahilitimesSwahili Times @swahilitimes
"Sijawahi kuona mtu muongo kama CAG, anawasilisha taarifa ya uongo kwa Rais. Sare za Polisi anazodai ni hewa zipo. Kama nasema uongo, najivua nguo, tuambatane na maofisa wa CAG wakaangalie makontena zaidi 15 (40ft) na 'ma-godown' 5 yaliyosheheni sare hizo."- Waziri Kangi Lugola
Image

April 25th 2019

26 Retweets208 Likes

Kuna ishara kwamba mwezi huu wa Mei utatawaliwa na matukio mazito sana, ambayo yanaweza kuutikisa mno utawala wa kidikteta wa Magufuli.

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
May is going to redefine #Tanzania

April 27th 2019

3 Likes

Naomba nisieleze kwa undani zaidi ya kuwakumbusha kuwa USHIRIKA WA WACHAWI HAUDUMU, na likitokea la kutokea, msikose kunipa pongezi zangu kwa “kuwatonya mapema.”

Nakutakia siku na wiki njema, na pia nakutakia mwezi Mei mwema.

Mtumishi wako,

Evarist Chahali

Comment
Share
Share this post
Kwaheri Aprili, Mei Hii Yaja na Mazito
www.baruayachahali.com

Create your profile

0 subscriptions will be displayed on your profile (edit)

Skip for now

Only paid subscribers can comment on this post

Already a paid subscriber? Sign in

Check your email

For your security, we need to re-authenticate you.

Click the link we sent to , or click here to sign in.

TopNewCommunity

No posts

Ready for more?

© 2022 Evarist Chahali
Privacy ∙ Terms ∙ Collection notice
Publish on Substack Get the app
Substack is the home for great writing