Kwaheri Aprili, Mei Hii Yaja na Mazito
Kuna Ishara Za Matukio Makubwa Yatakayoweza Kubadili Mwenendo Wa Taifa
Naomba nianze #BaruaYaChahali kwa kumshukuru Mungu kwa kunisuru tena sijui kwa mara ya ngapi. Muda huu unaposoma Barua hii ningekuwa marehemu. Kwa kifupi, Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa, Mchungaji Modestus Kipilimba alimtuma “afisa muuaji wa Kitengo” anaitwa Allan (naomba nihifadhi jina la pili kwa sababu maalum) kuja kuniua hapa Uskochi.