Barua Ya Chahali

Share this post
Kamilisha Wikiendi Yako na #UziwaTwita Huu Kuhusu #UshindiMdogoMdogo
www.baruayachahali.com

Kamilisha Wikiendi Yako na #UziwaTwita Huu Kuhusu #UshindiMdogoMdogo

Evarist Chahali
Jun 21, 2020
Share this post
Kamilisha Wikiendi Yako na #UziwaTwita Huu Kuhusu #UshindiMdogoMdogo
www.baruayachahali.com

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
#UziwaTwita mfupi wa kuhitimisha wikiendi yako. Uzi huu unahusu "kusherehekea ushindi mdogo mdogo" kwa kimombo wanasema "celebrating small wins."
Image

June 21st 2020

1 Like

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Kabla ya kuingia kwenye uzi, nitumie fursa hii katika #FathersDay hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijalia baba bora kabisa, marehemu Mzee Chahali. Alinifundisha mengi lakini matatu makubwa ni πŸ‘‰ Kumcha Mungu πŸ‘‰ Utu na upendo πŸ‘‰ Kujenga na kustawisha AKILI. Rest in peace, dad!

June 21st 2020

1 Like

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Twende kwenye mada. Mara kadhaa nimeongelea umuhimu wa kusherehekea #UshindiMdogoMdogo. Pamoja na faida nyinginezo nyingi, kufanya hivyo husaidia kuleta "ushindi mkubwa."
Image
Image
Image

June 21st 2020

1 Like

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Yaani "ushindi mdogomdogo + ushindi mdogomdogo + ushindi mdogomdogo + ushindi mdogo mdogomdogo, nk, nk = hatimaye USHINDI MKUBWA. This is no rocket science 😊

June 21st 2020

1 Like

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Mara kadhaa nimekuwa nikiweka hadharani matukio mbalimbali ya ushindi mdogomdogo. Lakini bila haja ya kuyarudia matukio hayo, nielekee kwenye ushindi mdogomdogo mpya niliopata wikiendi hii

June 21st 2020

1 Like

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Nikurudishe nyuma kidogo. Licha ya mahaba yangu makubwa kwenye masuala ya kompyuta, eneo moja ambalo sikuwahi kuligusa ni kuprogramu kumpyuta (computer programming), yaani kwa kifupi "kuilisha kompyuta maelekezo ya kutekeleza jukumu flani."
Image

June 21st 2020

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Kitu pekee kinachokaribiana na programming ni wakati najifunza kublogu, nililazimika kuelewa "lugja ya kompyuta katika utengenezaji wa blogu," yaani HTML. Japo "wataalamu" wanasema hii sio lugha ya kuprogramu lakini kwangu ilikuwa ni kitu kinachokaribiana na hicho
Image

June 21st 2020

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Baada ya kuingia kwa kina kwenye #UsalamaWaMtandaoni, moja ya mahitaji muhimu yamekuwa ni msisitizo kwenye kuzimidu lugha za kuprogramu (programming languages), hususan PYTHON. Na niwe mkweli, jina hilo lenye maana ya CHATU kwa Kiswahili liliniogopesha
Image

June 21st 2020

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Lakini kadri nilivyozidi kuzama kwenye #UsalamaWaMtandaoni nikabaini mapema kuwa sio ni muhimu kujifunza Python bali kwa namna flani kama ni lazima. Sasa wikiendi hii nimeanza rasmi zoezi hilo. Si lengo la uzi huu kueleza kwa kina kuhusu kuprogramu au Python bali my small win
Image

June 21st 2020

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Hata hivyo, nimefanikiwa kuelewa masuala kadhaa ya kuvutia kuhusu kuprogramu. Moja ni jinsi ya kujifunza na kuboresha uelewa kuhusu kuprogramu. Njia kuu na pengine rahisi ni kwa kutumia mtandao. Kwa upande wa Python, kuna jamii (community) kubwa iliyo tayari kutoa sapoti

June 21st 2020

1 Like

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Mwanafunzi wa kuprogramu anakumbushwa kuwa hakuna mtu mmoja mwenye kujua kila kitu kuhusu programming, na hiyo inawafanya hata nguli wa kuprogramu kuendelea kuwa kama wanafunzi. Na hii huondoa dharau kwa wanafunzi halisi pindi wakiuliza "maswali ya kitoto."

June 21st 2020

1 Like

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Nimejifunza pia njia kadhaa za kuuliza maswali "ki-smati" kuhusiana na kuprogramu. Zipo njia nyingi lakini hizi chache ndio zilizonivutia zaidi

June 21st 2020

1 Like

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
πŸ‘‰ Uliza kuhusu ulichotaka/unachotaka kufanya, na sio tu nini ulichofanya hadi ukakwama. Hii itamsaidia "mwalimu" kujua kama upo njia sahihi au la

June 21st 2020

1 Like

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
πŸ‘‰ Tanabaisha sehemu ambapo ulikutana na kasoro (error) husika. Je ilitokea mwanzoni mwa programu au baada ya kufanya hatua flani?

June 21st 2020

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
πŸ‘‰ Copy na paste ujumbe mzima unaoashiria kasoro (error) na "code" yako kwenye tovuti hii
pastebin.com au gist.github.com.Discover gistsGitHub Gist: instantly share code, notes, and snippets.gist.github.com

June 21st 2020

2 Likes

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
πŸ‘‰Eleza nini ulichokwishajaribu kufanya kutatua tatizo husika. Hii huonyesha kuwa wewe si mzembe bali umekwama tu baada ya kujituma

June 21st 2020

2 Likes

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
πŸ‘‰Taja toleo la programu husika. Kuna tofauti katinya toleo la pili la Python na la tatu. Pia tanabaisha OS (Operating System) unayotumia, kama ni Windows au Mac OS au Linux
Image

June 21st 2020

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
πŸ‘‰Elezea kama kasoro yajitokeza ukifanya hatua flani tu au katika kila hatua unayofanya.

June 21st 2020

1 Like

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Ofkoz kuna njia zaidi lakini kwa mtazamo wangu, hizi nilizotaja zinafanya zoezi zima la kuuliza na kupewa msaada ulipokwama kiwa rahisi.

June 21st 2020

1 Like

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Kuna tovuti mbalimbali zinazoeleza jinsi ya kuomba msaada pindi ukikwama kwenye kuprogramu. Hizo ni pamoja na πŸ‘‰
autbor.com/help/ πŸ‘‡reddit.com/r/learnprogram… πŸ‘‡ reddit.com/r/cscareerques…index - cscareerquestionsr/cscareerquestions: A subreddit for those with questions about working in the tech industry or in a computer-science-related job.reddit.com

June 21st 2020

3 Likes

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Wanasema kwamba "programming isn't brain surgery" yaani kuprogramu sio sawa na upasuaji wa ubongo ambao hauna fursa ya kosa japo kiduchu. Kwenye kuprogramu, makosa ni sehemu ya kujifunza.

June 21st 2020

3 Likes

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Ni matarajio yangu kuwa uzi huu utakuhamasisha kuhusu πŸ‘‰ Ushindi mdogomdogo πŸ‘‰ Fursa ya kujifunza kuhusu kompyuta hususan #UsalamaWaMtandaoni na pengine kuprogramu pia. Ukihitaji ushauri, usisite kuwasiliana nami

June 21st 2020

4 Likes

Twitter avatar for @ChahaliEvarist Chahali @Chahali
Good evening
Image

June 21st 2020

2 Likes

Ndimi kocha wako (life coach),

Evarist Chahali

Comment
Share
Share this post
Kamilisha Wikiendi Yako na #UziwaTwita Huu Kuhusu #UshindiMdogoMdogo
www.baruayachahali.com

Create your profile

0 subscriptions will be displayed on your profile (edit)

Skip for now

Only paid subscribers can comment on this post

Already a paid subscriber? Sign in

Check your email

For your security, we need to re-authenticate you.

Click the link we sent to , or click here to sign in.

TopNewCommunity

No posts

Ready for more?

Β© 2022 Evarist Chahali
Privacy βˆ™ Terms βˆ™ Collection notice
Publish on Substack Get the app
SubstackΒ is the home for great writing