Kada Chadema Ashauri Chama Hicho Kiwaondoe Mawakili Wanaomtetea Mbowe Ili "Kama CCM Wameamua Kumfunga (Mbowe) Wamfunge tu" Ni Baada ya Jaji Kuonyesha Upendeleo wa Waziwazi kwa Mawakili wa Serikali
Niwe mkweli. Haikuwa rahisi kunukuu bandiko hili la kada huyu kinadkindaki wa Chadema huko Jamii Forums.
Haikuwa rahisi kwa sababu kama walivyo makada wengi wa CCM, kwa makada wa Chadema nao utakuwa mtu poa ukiongea yale tu yanayowapendeza, lakini ukiongea wasichopenda, utamwagiwa matusi. Mtu ninayemnukuu ameshanitusi mara kadhaa huko Jamii Forums kila …