Barua Ya Chahali

Share this post
Japo Nyakati Hizi za Janga La Korona Zahimiza Kuwajali Wenzetu, Ni Muhimu Kutosahau Kujijali Wewe Mwenyewe Pia.
www.baruayachahali.com

Japo Nyakati Hizi za Janga La Korona Zahimiza Kuwajali Wenzetu, Ni Muhimu Kutosahau Kujijali Wewe Mwenyewe Pia.

Evarist Chahali
Mar 26, 2020
1
Share this post
Japo Nyakati Hizi za Janga La Korona Zahimiza Kuwajali Wenzetu, Ni Muhimu Kutosahau Kujijali Wewe Mwenyewe Pia.
www.baruayachahali.com

Mada hii inahusu umuhimu wa kunijali mwenyewe ili uweze kuwajali wengine pia.

Mie nitakuwa mtu wa mwisho kukushawishi "uwe mtu mbaya" au katili (kama Bashite) au uwe na "roho mbaya" (kama Babake Bashite).

Kwa sababu uzuri kidogo wa sayari hii pekee tunayoishi unachangiwa na japo matone kidogo tu ya upendo, huruma, roho ya kusaidia wengine, nk.

Siwezi kusema "mie nina roho nzuri kweli" au "nina huruma mno" au "najali sana shida za wengine." Wa kusema hayo, au kinyume chake, ni nyie naowatumikia.

Ninachoweza kusema bila shaka ni kwamba kila siku najibidiisha kufanya japo kidogo kwa ajili ya wengine. Iwe kumkumbusha Jiwe kuhusu hili au lile, au kumkemea mwanae, Bashite, ambaye haishiwi drama, au kukuhamasisha uwe mtu bora, na kama tayari upo bora basi uwe bora zaidi.

Lakini mada hii inaweza kuonekana tofauti na hicho nachojibidiisha kukifanya na ninachojitahidi kukuhamasisha ukifanye - kuwa mtu mwema, mwenye upendo, mwenye huruma, mwenye kusaidia wengine, nk.

Mada hii inakushauri "uwe mbinafsi" Japo kidogo. Lengo si kujijali wewe tu bali kukusanya nguvu, nishati na muda wa kujali wengine.

Dada zangu wenye watoto mwafahamu hili. Usipojipa muda wa kupumzika pindi nafasi ikipatikana utaishia kulala badala ya kupika, kunyonyesha mtoto au kutimiza majukumu mengine ya mama.

Sasa nyakati hizi za janga la korona ni muhimu "kubalansi" kati ya kujali wengine na kujijali mwenyewe. Na ni muhimu kutambua kuwa huwezi kujali wengine bila kujijali mwenyewe kwanza. Huwezi kuwapa watu upendo kama hujipendi mwenyewe.

Ili kujua kama "unabalansi" kujijali na kujali wengine, jiulize maswali haya yafuatayo

👉 Unajiskia vibaya kusema "no" hata kama ni lazima iwe hivyo?
👉 Unajilaumu kusema "yes" kwa vile inakuathiri kwa namna flani?
👉 Huna muda kwa ajili yako mwenyewe?
👉 Unaona hustahili kushughulikia mahitaji yako kwa vile mahitaji ya wengine ni muhimu zaidi muda wote?
👉 Unadhani "dunia itakutenga" pindi ukishindwa kumjali/kumsaidia mtu kwa sababu umetingwa au huna uwezo wa kusaidia?

Maswali ni mengi zaidi ya hayo lakini haya yanaweza kusaidia kwa kuanzia.

Kumbuka, kujali wengine haimaanishi usijijali wewe mwenyewe pia.

Take care!

Ndimi mtumishi wako,

Evarist Chahali

Comment
Share
Share this post
Japo Nyakati Hizi za Janga La Korona Zahimiza Kuwajali Wenzetu, Ni Muhimu Kutosahau Kujijali Wewe Mwenyewe Pia.
www.baruayachahali.com

Create your profile

0 subscriptions will be displayed on your profile (edit)

Skip for now

Only paid subscribers can comment on this post

Already a paid subscriber? Sign in

Check your email

For your security, we need to re-authenticate you.

Click the link we sent to , or click here to sign in.

TopNewCommunity

No posts

Ready for more?

© 2022 Evarist Chahali
Privacy ∙ Terms ∙ Collection notice
Publish on Substack Get the app
Substack is the home for great writing