Huyu Hapa Kijana Anayetumiwa na WASIOJULIKANA Kufanya Ulawiti kwa Wanaotekwa | Ajigamba Kuwa ni Afisa wa Idara ya Usalama wa Taifa
Kijarida hiki kimefahamishwa kuwa kija huyo pichani anatumiwa na genge la WATU WASIOJULIKANA kufanya vitendo vya kiharamia dhidi ya watu mbalimbali wanaotekwa na genge hilo.
Jana, baada ya kuletewa taarifa husika, Jasusi aliweka mabandiko kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii kuuliza kuhusu identity ya kijana huyo.
Muda mfupi baadaye, wadau mbalimbali waliwasilisha taarifa zilizomtambua kijana huyu hatari.
Taarifa zilizopatikana baadaye zilieleza kuwa jina kamili la kijana huyu ni REUBEN EMMANUEL MBOYA, na amekuwa akijitambulisha kuwa ni Afisa wa Idara ya Usalama wa Taifa na “rafiki wa karibu wa Bashite”.
Hadi kufikia hatua ya kuchapisha taarifa hii, kijarida hiki kimejiridhisha kuhusu tuhuma dhidi ya kijana huyo kwamba amekuwa akitumiwa na genge la WASIOJULIKANA kuwalawiti watu mbalimbali wanaotekwa na genge hilo (kwa mujibu wa taarifa, Wasiojulikana huwatumia watu wao mbalimbali kufanya vitendo vichafu dhidi ya waliowateka). Kadhalika, taarifa zimeeleza kuwa kijana huyo ameshawakamatisha watu kadhaa akiwa kama mtoa habari wa genge hilo la kiharamia.
Ikumbukwe kuwa unyama wote unaoendelea nchini Tanzania unafanywa na WATU WANAOFAHAMIKA japo hutajwa kuwa WATU WASIOJULIKANA. Wanafahamika kwa sababu mnaishi nao mtaani, ni ndugu, jamaa au marafiki zenu na wengine mnawafahamu kutokana na mienendo yao.
Kuna wanaojidanganya kuwa wao hawawezi kufanyiwa unyama na maharamia hawa kwa vile tu sio wanaharakati au hawajihusishi na siasa. Endeleeni kujidanganya.



