Hongera Mama @SuluhuSamia, Mwanamke wa Kwanza Kuwa Rais wa Tanzania, kwa Kuendelea na Teuzi za Kihistoria, Hongera Zuhura Yunus (@venusnyota), Mwanamke wa Kwanza Kuwa Mkurugenzi Mawasiliano Ikulu
Nianze makala hii kwa pongezi zangu za dhati kwa Zuhura Yunus, sio tu kuteuliwa na Mama Samia Suluhu Hassan kuwa Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, bali pia kwa kuandika historia ya kuwa mwanamke wa kwanza kabisa katika historia ya Tanzania kushika wadhifa huo muhimu.
Pongezi pia kwa Mama Samia, sio tu kwa vile Machi mwaka jana aliingia kwenye vitabu vya k…