Dkt Slaa aliyemlaumu Zitto kuongelea ufisadi uliotajwa kwenye ripoti ya CAG aumbuliwa na Kinana aliyesema Mama Samia awachukulie hatua waliotajwa kwenye ripoti hiyo.
Hadi hivi karibuni, nilikuwa nikimchukulia Dokta Wilbrord Slaa, Katibu Mkuu wa zamani wa Chadema na balozi wa zamani wa Tanzania nchini Sweden, kuwa mmoja ya Watanzania wazalendo kupita maelezo.
Na nilikuwa na sababu za msingi za kumchukulia hivyo. Miaka kadhaa huko nyuma, yeye Dokta Slaa, Mheshimiwa Zitto Kabwe na Mheshimiwa Freeman Mbowe waliunda “timu…