Dear Mama Samia, Kesi Ya Mbowe ni ya Kisiasa Na Inatia Doa Utawala Wako, Ushauri wa TISS Kuwa "Mbowe Afungwe Kisha Umsamehe ili Upate Political Capital" ni Fyongo. Hujachelewa, Chukua Hatua Stahili.
Nitanabaishe mapema kuwa bado ninamuunga mkono Mama Samia Suluhu, sio kwa sababu za “kusubiri uteuzi” au “kujikomba,” bali kwa sababu mbili kuu. Ya kwanza na ya msingi kabisa ni ukweli kwamba kufanikiwa kwake ni kufanikiwa kwetu sote.
Sawa, ni Rais anayetokana na CCM, ambayo naichukia with passion, lakini ni Rais wa Watanzania wote, at least theoretical…