Barua Ya Chahali

Share this post
Dear Fatma Karume, pole kwa kutukanwa na baadhi ya wana-Chadema. Hata hivyo, wewe na Maria "mmewalea" sana hawa watukanaji mtandaoni
www.baruayachahali.com

Dear Fatma Karume, pole kwa kutukanwa na baadhi ya wana-Chadema. Hata hivyo, wewe na Maria "mmewalea" sana hawa watukanaji mtandaoni

Evarist Chahali
Jun 3
2
Share this post
Dear Fatma Karume, pole kwa kutukanwa na baadhi ya wana-Chadema. Hata hivyo, wewe na Maria "mmewalea" sana hawa watukanaji mtandaoni
www.baruayachahali.com

Nianze kwa kutoa pole kwa matusi ambayo mwanaharakati Fatma Karume amekuwa ukivurumishiwa na baadhi ya wana Chadema ambao hawakupendezwa na uamuzi wake wa kwenda kutoa maoni kwenye Kikosi Kazi cha Rais kuhusu masuala ya siasa.

Read Barua Ya Chahali in the new Substack app
Now available for iOS

Hata hivyo, huenda wahuni hao wasingeweza kuwa na jeuri ya kumtukana mwanasheria huyo laiti yeye na mwenzie Maria wangechukizwa na tabia ya matusi ya baadhi ya wafuasi wa Chadema ambao pia walikuwa ni mashabiki wakubwa wa akinadada hao.

Share

Pengine Fatma amesahau, lakini huko nyuma wakati mie nina mawasiliano nae (yalivunjika baada ya yeye kunisemea ovyo), niliwahi kumtumia DM kuhusu matusi ya Kigogo dhidi ya Mama Samia lakini sikupata jibu. In fact wakati Kigogo anamkebehi na kumtusi Mama Samia mfululizo, sio tu hakuwahi kumshauri aache kumkosea heshima Rais bali pia alimmwagia sifa kama twiti hii inavyoonyesha

Twitter avatar for @fatma_karumefatma karume aka Shangazi @fatma_karume
Nadhani watu wanamu-underestimate sana Kigogo. Mkim-study mtaelewa yafuatayo: *Ni mtu moja - kuna wakati ilibidi apumzike na akapotea. Ingekuwa ni watu wengi wangechukuwa zamu. *Ni INTELLIGENT sana - msione ni RAHISI kufanya anachokifanya na kubaki mafichioni *Ni CONSISTENT

June 24th 2021

167 Retweets1,776 Likes

Lakini si matusi ya Kigogo kwa Mama Samia tu ambayo both Fatma na Maria hayakuwasumbua, mvua ya matusi na udhalilishaji tuliofanyiwa na mtu huyo haikuwasumbua pia na waliendelea kuwa maswahiba.

Nilitatizwa sana na hali hiyo kwa sababu naamini kuwa laiti wangemshauri mpenda matusi huyo kwamba aache matusi na awasilishe ujumbe wake kwa lugha ya kistaarabu basi huenda asingeendelea kutukana.

Kilichonisikitisha zaidi ni ukweli kwamba both Fatma na Maria walikuwa wahanga wa matusi ya Musiba, yule mpambe wa Mwendazake ambaye kila kukicha alizusha hili kama sio lile. Kwa maana hiyo, katika mazingira ya kawaida ungetarajia akinadada hao wachukizwe na mtu yeyote aliyefanya mambo kama ya Musiba. Lakini kwa sababu wanazozijua wao, walikaa kimya.

Barua Ya Chahali
Juma Thomas ZANGIRA: Mtanzania wa Kwanza Kushtakiwa Nchini Tanzania Kwa Kosa La UJASUSI (kuna kijitabu cha kurasa 15 kuhusu kesi hiyo)
Pakua kijitabu hicho cha bure HAPA…
Read more
8 months ago · 2 likes · Evarist Chahali

Yayumkinika kutanabaisha bila shaka kuwa umaarufu na kukubalika kwa Kigogo kulichangiwa kwa kiasi fulani na ukweli kwamba alikuwa akikubalika kwa akinadada hawa wawili wanaoheshimiwa na Watanzania wengi.

Akinadada hao wanafahamu vema kuwa Musiba alianza kutuandama watu wachache tu kabla hajaota mapembe na kusambaza hujuma zake hadi kwa baadhi ya wana-CCM. Funzo hapo ni hili: MCHAWI AKIMALIZA KUROGA MTAA MZIMA HUHAMIA KWENYE FAMILIA YAKE.

Barua Ya Chahali
Dear Mama @SuluhuSamia, mabalozi hawa wawili wanakuhujumu
Inatanabaishwa kuwa moja ya dhambi kuu kwenye taaluma ya intelijensia ni kushindwa kutahadharisha. Hii inachangiwa na ukweli kwamba taaluma hiyo inatarajiwa zaidi kubaini matishio ya kiusalama kabla hayajasababisha madhara. Makala hii ya kiintelijensia inaeleza kuhusu hujuma za mabalozi wawili wa Tanzania wanavyomhujumu Rais Samia Suluhu pamoja na Tanzania kwa ujumla…
Read more
19 days ago · 1 like · Evarist Chahali

Kwa maana hiyo kama ambavyo ilikuwa suala la muda tu kabla Musiba hajaanza kuwavaa wana-CCM wenzie, kwa Kigogo nae ilikuwa suala la muda tu kabla hawaanza kuwavaa watu waliokuwa wanamsapoti ikiwa ni pamoja na Fatma na Maria.

Na ndivyo ilivyokuwa. Mara baada ya Kigogo kutibuana na Chadema na kujipeleka CCM, amekuwa mkosoaji mkubwa dhidi ya both Maria na Fatma. Watu walewale waliomuenzi, wamegeuka wahanga wake.

Read Barua Ya Chahali in the new Substack app
Now available for iOS

Kwahiyo ungetegemea kuwa development ya Musiba from kutushambulia sie “watu hatari” hadi kuwavamia akina Kinana, na hiyo ya Kigogo from kumtukana Mama Samia na sie wengine hadi sasa kuwageukia akina Maria na Fatma ingekuwa funzo kwa akinadada hao dhidi ya viumbe wote wanaofanya unyanyasaji mtandaoni kwa njia ya matusi. Lakini kwa vile matusi hayo yalitulenga wengine, akinadada hao waliendelea kuwa comfortable.

Katika moja ya twiti zake, Fatma anasema

Twitter avatar for @fatma_karumefatma karume aka Shangazi @fatma_karume
Sipendi UNAFIK. Ukifanywa ya CDM au ACT au CCM! UNAFIK ni UNAFIK tu. CDM wana-attack wenzao kwa kuongea na Kikosi Kazi cha Rais lakini wako BIZEEEE kumualika Rais kwa Sugu na kujisifia haya ndio mambo CHANYA! Please ……….. Tuheshimiane na tuache UDIKTETA UCHWARA!

Yuzuu @Yuzuumwakisunga

@fatma_karume Auntie mbona Leo uko very furiously 😂😂✌️🤔

June 1st 2022

75 Retweets529 Likes

Lakini anakwepa kuongelea UNAFIKI WA WANAHARAKATI ambao sio tu wanakalia kimya ukiukwaji wa haki za watu mbalimbali wanaotukanwa mtandaoni kwa vile tu hawaafikiani na hoja za watu flani bali pia wana uswahiba na watukanaji hao.

Majuzi tumeshuhudia Mheshimiwa Freeman Mbowe akiwatolea uvivu viongozi wenzie na wanachama wengine wa Chadema na kuwaeleza bayana kuwa matusi hayakubaliki, sambamba na kukemea lugha isiyo ya kistaarabu dhidi ya viongozi wa vyama vingine. Japo hakuvitaja vyama hivyo, ninaamini alikuwa akiongelea ukosefu wa nidhamu miongoni mwa wana-Chadema wengi dhidi ya Mama Samia na Mheshimiwa Zitto Kabwe, kiongozi mkuu wa ACT-Wazalendo.

Barua Ya Chahali
Uchaguzi TLS: Ushindi wa Prof Hosseah unaashiria kuporomoka kwa nguvu ya ushawishi wa Chadema, waliweza kumuingiza madarakani 2021 wameshindwa kumzuwia asirudi madarakani 2022
Kwanza Jasusi anaomba ajipongeze kwa kubashiri kuwa Profesa Edward Hosseah angeshinda kinyang’anyiro cha urais wa TLS uliofanyika jana huko Arusha. Katika makala hii iliyochambua kuhusu uchaguzi huo, Jasusi alitanabaisha haya pichani…
Read more
13 days ago · 3 likes · Evarist Chahali

Both Fatma na Maria wanafahamu kuwa jambo pekee linalohitajika kwa maovu kushamiri ni kwa watu wazuri kama wao kukaa kimya. Ndio maana naamini kwa dhati kabisa kuwa laiti wanaharakati hawa wangekuwa mstari wa mbele kukemea matusi kama tunavyofanya wengine, basi huenda tabia hiyo isiyopendeza ingepungua sana.

Kama sauti muhimu kwenye ajenda ya katiba mpya, ungetegemea wanaharakati hao wawakumbushe wafuasi wao wanaoendekeza matusi kwamba “matusi yananajisi mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya”. Ni hivi, kama hawa wanaopigania katiba mpya ni madikteta ambao usipoafiki hoja zao wanakutukana, je wakiingia madatrakani si watanyonga kila mtu?

Nimalizie kwa kutumaini kuwa labda experience hii isiyopendeza ya matusi dhidi ya Fatma itamsaidia sio tu kutambua tena kuwa “MCHAWI AKIMALIZA KUROGA MTAA MZIMA HUVAMIA KWENYE FAMILIA YAKE” yaani hao wapenda matusi wakishamaliza kumtukana Mama Samia na akina sie watawageukia haohao akina Fatma na Maria (na mfano hai ni Kigogo wa leo vs Kigogo yule aliyekuwa swahiba wa both Maria na Fatma) bali pia itampa jasiri wa kuwakumbusha “fans wake” pindi wanapoanza kutumia matusi kama nyenzo ya kuzuwia maoni wasiyotaka kuyasikia.

Watanzania tuna kasumba ya kuvumilia maovu. Hakuna anayekumbuka wala kujali yaliyojiri zama za ufisadi katika wamu ya Jk kama hakuna anayesumbuliwa na yaliyojiri zama za udikteta wa Mwendazake. Ni kama hakuna baya lililojiri huko nyuma.

Na ni katika namna hiyohiyo, ni watu wachache tu wanaotatizwa na tabia inayozidi kushamiri ya matusi mtandaoni. Kwa watu wengi tu, tatizo hilo haliwahusu kwa sababu wao sio wahanga. Lakini wanachosahau kuwa kushamiri kwa matusi mtandaoni kunamfanya kila mtumiaji wa mtandao kuwa mhanga mtarajiwa.

Mwisho, ni matumaini yangu kuwa Fatma ataichukulia makala hii kwa mtazamo chanya na ikiwezekana kufanyia kazi ushauri uliomo.

TANZANIA BILA MATUSI INAWEZEKANA.

Jumma Mubarak!

Share this post
Dear Fatma Karume, pole kwa kutukanwa na baadhi ya wana-Chadema. Hata hivyo, wewe na Maria "mmewalea" sana hawa watukanaji mtandaoni
www.baruayachahali.com
TopNewCommunity

No posts

Ready for more?

© 2022 Evarist Chahali
Privacy ∙ Terms ∙ Collection notice
Publish on Substack Get the app
Substack is the home for great writing