Askofu Gwajima vs Mama Samia, Je Nini Kinafuata? - Ubashiri wa Kiintelijensia (Intelligence Outlook)
Hakuna haja ya kuuma maneno katika yanayoendelea huko CCM. Kwa sababu ni wazi kwamba baada ya Rais Samia Suluhu kujibu press conference ya Askofu Gwajima aliyoifanya Mei 24 mwaka huu ambapo aliinyooshea kidole serikali ya Rais Samia kuhusu janga la utekaji, ilitarajiwa aidha Askofu Gwajima “aogope” na kutojibu, au ajibu na iwe “vita kamili”. Kila aliyesikiliza hotuba ya Askofu Gwajima jana anafahamu kilichojiri.
Uchambuzi huu unajikita kwenye eneo moja kuu, nalo ni ubashiri wa kiintelijensia kuhusu yajayo mbeleni. Jasusi alibashiri kwa usahihi kwamba Askofu Gwajima sio tu angemjibu Rais Samia bali pia “angetembelea” jina jipya la Gwajimanization, na ndivyo ilivyotokea.
📌Je Askofu Gwajima atadumu ndani ya CCM au atafukuzwa?
📌Je akidumu, ataendelea na ukosoaji au atanyamazishwa?
📌Je akifukuzwa, atapunguza kasi au ndio itakuwa “balaa” zaidi?
📌Je Watu Wasiojulikana wanaweza “kumpitia”?
📌Je yupo peke yake au kuna watu nyuma yake?
Ubashiri wa Kiintelijensia (Intelligence Outlook) Kuhusu Yajayo
Mara kwa mara Jasusi amekuwa akieleza kuwa ni wajibu wa kiintelijensia kubashiri yajayo kabla hayajatokea. Na ni kwa muktadha huo, uchambuzi huo unajikita kwenye jukumu hapa chini.